Sura 15

1 Wafarisayo na walimu wa Sheria wakamufikia Yesu kutoka Yerusalema. Basi wakamwuliza: 2 «Kwa sababu gani wanafunzi wako wanavunja desturi za babu zetu kwa kula chakula pasipo kunawa mikono? 3 Yesu akawajibu: “Na ninyi, kwa sababu gani munavunja amri ya Mungu kwa kufuata desturi zenu? 4 Kwa maana Mungu alisema: Uwaheshimu baba yako na mama yako.” Naye alisema vilevile: “Anayelaani baba yake au mama yake anapaswa kuuawa.” 5 Lakini ninyi munasema kwamba mtu akiwa na kitu ambacho angeweza kuwasaidia baba yake au mama yake, lakini akimwambia kwamba amekitoa sadaka kwa Mungu, 6 basi, hapaswi tena kumusaidia baba yake. Hivi munazarau Neno la Mungu kwa kufuata desturi zenu 7 Ninyi wanafiki! Isaya alitabiri vema juu yenu, wakati aliposema maneno haya: 8 “Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao. Lakini mioyo yao ni mbali nami. 9 Ibada wanayonifanyia ni ya bure, sababu mafundisho yao yanalingana na kanuni za watu tu.”» 10 Kisha Yesu akaita kundi la watu na kuwaambia: «Musikilize na kuelewa maneno nitakayowaambia. 11 Kitu kinachoingia ndani ya kinywa cha mtu hakiwezi kumuchafua. Lakini ni kile kinachotoka ndani ya kinywa chake ndicho kinachomuchafua. 12 Halafu wanafunzi wakamufikia na kumwuliza: “Unajua kwamba Wafarisayo walikwazwa kwa kusikia maneno hayo uliyosema?” 13 Yesu akajibu: “Wao ni kama mumea usiopandwa na Baba yangu wa mbinguni, utakaopaswa kuongolewa. 14 Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.” 15 15 Halafu Petro akamwambia: “Utuelezee maana ya mufano huu.” 16 Yesu akamujibu: “Hata ninyi vilevile hamuwezi kuelewa? 17 Hamuelewi kwamba kila kitu kinachoingia ndani ya kinywa, kinapita ndani ya tumbo na kisha kinatoka na kwenda katika choo? 18 Lakini vyote vinavyotoka ndani ya kinywa ni vyenye kutoka kwanza ndani ya moyo wake, navyo vinamuchafua mtu. 19 Kwa maana ndani ya moyo munatoka mawazo mabaya yanayoleta uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo na matukano. 20 Mambo haya ndiyo yanayomuchafua mtu! Lakini kula pasipo kunawa mikono hakuwezi kumuchafua mtu.”» 21 Yesu akaondoka pale na kwenda pande za karibu na mji wa Tiro na wa Sidona. 22 Mwanamuke mmoja Mukanana aliyeishi katika pande zile akamufikia, akilalamika, akisema: «Ee Bwana, mwana wa Daudi, unihurumie! Binti yangu anateswa sana na pepo. 23 Lakini Yesu hakumujibu hata neno moja. Halafu wanafunzi wake wakamufikia na kumusihi: “Umwambie aende kwa maana anatuuzi na makelele.” 24 Naye Yesu akajibu: “Nimetumwa tu kwa taifa la Waisraeli, wanaokuwa kama kondoo wanaopotea.” 25 Lakini mwanamuke yule akapiga magoti mbele yake na kumwambia: “Ee Bwana, unisaidie!” 26 Yesu akamujibu: “Si vizuri kukamata chakula cha watoto na kukitupia imbwa.” 27 Yule mwanamuke akasema: “Ndiyo, Bwana, unasema ukweli, lakini hata imbwa wanazoea kula makombo yanayoanguka chini ya meza ya wabwana wao.” 28 Halafu Yesu akamujibu: “Wewe mwanamuke, imani yako ni kubwa! Ifanyike kwako sawa ulivyoomba.”» Na binti yake akapona tangia saa ile ile. Yesu anawaponyesha watu wengi 29 Yesu akaondoka kule, akapita pembeni ya ziwa la Galilaya. Kisha akapanda kwenye kilima, naye akaikaa pale. 30 Halafu makundi mengi ya watu wakamufikia, wakimuletea vilema, vipofu, viwete na wabubu. Wakawaweka mbele ya Yesu, naye akawaponyesha. 31 Yale makundi ya watu wakashangaa sana wakati walipowaona wabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanatembea, na vipofu wanaona. Nao wakamusifu Mungu wa Waisraeli. 32 Yesu akawaita wanafunzi wake, na kuwaambia: «Ninawasikilia watu hawa huruma, kwa sababu wamekaa nami sasa kwa muda wa siku tatu, nao hawana chakula tena. Nami sitaki kuagana nao pasipo kula, kusudi wasiregee katika njia. 33 Nao wanafunzi wake wakamujibu: “Hapa katika pori, tutaweza kupata wapi chakula cha kushibisha kundi kubwa kama hili?” 34 Yesu akawauliza: “Muko na mikate ngapi?” Nao wakajibu: “Tuko na mikate saba na samaki ndogo chache.”» 35 Basi Yesu akawaamuru watu waikae chini. 36 Kisha akatwaa ile mikate saba na zile samaki, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake wavigawanye kwa watu. 37 Wote wakakula na wakashiba. Kisha wanafunzi wakaokota vipande vilivyobaki, wakajaza vitunga saba. 38 Watu waliokula walikuwa wanaume elfu ine, pasipo kuhesabu wanawake na watoto. 39 Kisha kuaga yale makundi ya watu, Yesu akaingia ndani ya chombo, na kwenda pande za Magadani.