Hii inaanza baraka za mwisho za Yakobo kwa wanawe. Hii inaendelea hadi 49:27. Baraka za Yakobo zinaandikwa kwa namna ya shairi.
Sentensi mbili zinasema jambo moja kuweka msisitizo. "Njooni na msikilize kwa makini baba yenu"
Yakobo anajitambua katika lugha ya mtu wa utatu. Inaweza kusemwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "wanangu. Nisikilizeni, baba yenu"
Misemo ya "mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu" na "mwanzo wa uwezo wangu" zina maana moja. Maneno "uwezo" na "nguvu" yana maana ya uwezo wa Yakobo kuzaa watoto. Maneno "mzaliwa wa kwanza" na "mwanzo" ina maana ya kwamba Rubeni ni mwanawe wa kwanza. "mwanangu wa kwanza nilipokuwa mwanamume"
Hii inaweza kuwekwa kama sentensi mpya. "Wewe ni wa kwanza kwa heshima na nguvu" au "Unawapita wengine wote kwa heshima na nguvu"
Yakobo anamlinganisha Rubeni na maji yenye mkondo mwenye nguvu kusisitiza ya kwamba hawezi kujizuia hasirayake na hayupo imara.
"hautakuwa wa kwanza miongoni mwa ndugu zako"
Hapa "kitanda" na "juu ya kitanda changu" ina maana ya suria wa Yakobo, Bilha. Yakobo ana maanisha pale ambapo Rubeni alilala na Bilha. "kwa sababu ulipanda kitandani mwangu na kulala na Bilha suria wangu. Umeniaibisha"
Kaluli zote mbili zina maana moja.
Hii haimaanishi tu ya kwamba wao ni ndugu kwa kuzaliwa. yakobo anasisitiza ya kwamba walishirikiana pamoja kuwaua watu wa Shekemu.
"Wanatumia panga zao kudhuru na kuua watu"
Yakobo anatumia maneno "nafsi" na "moyo" kujitambulisha na kusema ya kwamba watu wengine, na labda Mungu pia, wanamheshimu sana ya kwamba hatamani kujiunga na wale wanaopanga kufanya uovu.
Misemo hii miwili ina maana moja. Yakobo anaunganisha kuweka msisitizo ya kwamba hataki kushirikiana katika mipango yao miovu. "hakika sitajiunga nao kufanya mipango yoyote"
Hii ina maana ya Simoni na Lawi kulemaza ng'ombe kwa starehe tu.
Hii ina maana ya kukata visigino vya miguu ya wanyama ili isiweze kutembea.
Mungu kumlaani Simoni na Lawi inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa akilaani hasira na ukali wao. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Bwana anasema, 'Nitawalaani kwa sababu ya hasira yao kali na ukali wao mkatili" au "Mimi, Bwana, nitawalaani kwa sababu ya hasira ya kali na ukali wao mkatili"
Katika unabii, nabii mara nyingi huzungumza maneno ya Mungu kana kwamba Mungu mwenyenwe alikuwa akizungumza. Hii inasisitiza ukaribu ulivyo kati ya nabii na Mungu.
Neno "nitalaani" linaeleweka. "nami nitalaani ukali wao, maana ulikuwa katili"
Neno "Nitawagawa" lina maana ya Mungu. Neno "kuwatawanya" lina maana ya Simoni na Lawi lakini ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wao. Maneno "Yakobo" na "Israeli" ni lugha nyingine yenye maana ya watu wote wa Israeli. "Nitawagawanya uzao wao na kuwasambaza miongoni mwa watu wote wa Israeli"
Kauli hizi mbili zina maana moja.
Sentensi ya pili inaeleza sababu ya sentensi ya kwanza. Neno "kwa" au "kwa sababu" linaweza kuongezwa kuweka hii wazi. "nitakusifu wewe. Kwa mkono wako" au "nitakusifu kwa sababu mkono wako"
Hii ni njia ya kusema. "Utawashinda adui zako"
Hii ina maana kuinama kwa unyenyekevu kuonyesha heshima na taadhima kwa mtu.
Yakobo anamzungumzia Yuda kana kwamba alikuwa mtoto wa simba. Yakobo anasisitiza nguvu ya Yuda. "Yuda ni kama mwana wa simba"
"Wewe, mwanangu, umerudi kutoka kula windo lako"
Yakobo anamlinganisha Yuda na simba jike. Simba jike ni mwindaji na mlinzi wa msingi wa watoto wake.
Yakobo anatumia swali kusisitiza jinsi Yuda anavyotisha watu wengine. "Hakuna atakaye kumuamsha"
"Fimbo" na "fimbo ya utawala" ni miti iliyopambwa ambayo wafalme hubeba. Hapa ni lugha nyingine yenye maana ya nguvu ya utawala. Na "Yuda" ina maana ya uzao wake. "Nguvu ya kutawala daima itakuwa ndani ya uzao wa Yuda"
Maana zawezekana kuwa 1) "Shilo" ina maana "shukrani". "hadi pale mataifa yatamtii na kuleta shukrani kwake" au 2) "Shilo" ina maana ya mji wa Shilo. "hadi pale mtawala atakuja Shilo. Kisha mataifa yatamtii." Watu wengi huchukulia hili kama unabii kuhusu Mesia ambaye ni uzao wa Mflame Daudi. Daudi ni uzao wa Yuda.
Hapa "mataifa" ina maana ya watu. "Watu wa mataifa watamtii"
Kauli zote mbili zina maana moja. Inasemekana ya kwamba mizabibu imejaa zabibu ambayo bwana hajali kama punda inavila baadhi yao.
Maana za muonakano wa "wake" au "amefua" ni 1) ina maana ya uzao wa Yuda. "wake ... wame" au 2) ina maana ya mtawala katika 49:10, ambayo inaweza kumaanisha Mesia.
Kauli zote mbili zina maana moja. Inasemekana ya kwamba kuna zabibu nyingi sana hadi wanaweza kufua nguo zao kwa maji yake.
Mara nyingi katika unabii matukio yatakoyotokea hapo baadae yanaelezwa kama jambo lililokwisha tokea zamani. Hii inasisitiza ya kwamba tukio hili hakika litatokea. "watafua" au "atafua"
HIi inazungumzia kuhusu maji ya zabibu kana kwamba yalikuwa damu. Hii inasisitiza jinsi gani maji yalikuwa mekundu.
Hii ina maana ya rangi ya macho ya mtu kulinganisha na rangi ya mvinyo mwekundu. Maana zaweza kuwa 1) macho meusi ina maana macho yenye afya au 2) macho ya watu yatakuwa mekundu kutokana na kunywa mvinyo mwingi
Hii inalinganisha rangi ya meno ya watu kwa weupe wa rangi ya maziwa. Hii inasemekana ya kwamba kutakuwa na ng'ombe wengi wenye afya na kuwa na maziwa mengi ya kunywa.
Hii ina maana ya uzao wa Zabuloni.
Hapa "atakuwa" ina maana ya miji ya baharini ambayo watu wa Zabuloni wataishi au kujenga. Miji hii itatoa hifadhi kwa meli.
sehemu ya bahari ambayo ipo karibu na nchi na ipo salama kwa ajili ya meli.
Yakobo anazungumzia kuhusu Isakari na uzao wake kana kwamba walikuwa punda. Hii inasisitiza ya kwamba watafanya kazi kwa bidii. "Uzao wa Isakari utakuwa kama punda mwenye nguvu"
Mara nyingi katika unabii matukio ambayo yatatokea baadae inaelezwa kama kitu ambacho tayari kinaendelea. Hii inasisitiza ya kwamba tukio litatokea hakika. Inaweza kuwekwa kwa lugha ya baade. "Isakari atakuwa" au "Uzao wa Isakari utakuwa"
Hapa "Isakari" ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wake. "Uzao wa Isakari ... Wanaona .. Wataona"
Maana zaweza kuwa 1) "ajilazaye chini katikati ya kundi walizokuwa wakibeba" au 2) "ajilazaye chini katikati ya zizi la kondoo".Kwa namna yoyote ile, Yakobo anazungumzia kuhusu uzao wa Isakari kana kwamba walikuwa punda ambao wamefanya kazi kwa bidii na wamejilaza chini kupumzika.
"sehemu ya kupumzikia ambayo ni nzuri na kwamba nchi inapendeza"
Msemo huu "Atainamisha bega lake kwa mzigo" ni njia ya kusema "fanya kazi kwa bidii kubeba mzigo"
"watafanya kazi kwa wengine kama watumwa"
Hapa "Dani" ina maana ya uzao wake. "Uzao wa Dani utawaamua watu wake"
Maana zinazowezekana za "watu wake" ni 1) "watu wa Dani" au 2) "watu wa Israeli"
Yakobo anazungumza kuhusu Dani na uzao wake kana kwamba walikuwa nyoka. Ingawa nyoka ni mdogo, inaweza kumshusha aongozaye farasi chini ya farasi wake. Kwa hiyo Dani, ingawa kabila dogo, ni la kutisha sana kwa adui zake. "Uzao wa Dani utakuwa kama nyoka kando ya barabara"
Nomino inayojitegemea "wokovu" inaweza kutafsiriwa kama "kuokoa". "Ninakusubiri, Yahwe, kunikoa"
Neno "Ninaungoja" ina maana ya Yakobo.
Hawa ina maana ya vizazi vya kila mwanamume.
Hapa "visigino" ina maana ya wavamizi ambao wanatoroka kutoka kwa uzao wa Gadi.
Hapa "vingi" ni njia ya kusema "vitamu"
Yakobo anazungumzia kuhuus uzao wa Naftali kana kwamba walikuwa paa wa kike ambaye yupo huru kukimbia. Hii inaweza kusisitiza ya kwamba watakuwa wajumbe wepesi. "Uzao wa Naftali utakuwa kama paa aliyeachiwa huru"
"mtoto wa paa". Maana kwa lugha ya Kihebrania haipo wazi. Baadhi ya tafsiri hutafsiri kama "ana maneno mazuri" au "kuzungumza mambo mazuri"
Hapa "Yusufu" ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wake. Yakobo anazungumzia uzao kana kwamba walikuwa shina la mti lizaalo matunda mengi. Hii inasisitiza ya kwamba wataongezeka sana kwa idadi.
shina kuu la mti
Shina ambalo litakuwa na kusambaajuu ya ukuta inazungumziwa kana kwamba ilikuwa inapanda.
Yakobo anaendelea kumbariki Yusufu na uzao wake.
Mtu anayeshikilia upinde kwa umakini inazungumziwa kana kwamba uoinde mwenyewe utakuwa imara. Inasemekana anaushikilia kwa ustadi anapopima kwa adui wake. "ataushika upinde wake kwa uimara anapolenga adui wake"
Hapa "wake" ina maana ya Yakobo anayesimama badala ya uzao wake. "upinde wake .. mikono yake"
Hapa "mikono" ina maana ya mikono ya mtu anaposhikilia upinde wake kwa makini. "mikono yake utabaki imara anapolenga upinde wake"
"mikono" inaelezea nguvu ya Yahwe. "nguvu ya Mwenye Nguvu"
Hapa "jina" lina maana ya mtu mzima. "kwa sababu ya Mchungaji"
Yakobo anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa "mchungaji". Hii inasisitiza ya kwamba Yahwe anawaongoza na kuwalinda watu wake.
Yakobo anazungumzia kuhusu Yahwe kana kwamba alikuwa "Mwamba" ambao watu wanaweza kuupanda kutafuta usalama kutoka kwa maadui. Hii inasisitiza ya kwamba Yahwe hulinda watu wake.
Yakobo anaendelea kumbariki Yusufu na uzao wake.
Hapa "atakusaidia" ina maana ya Yusufu inayomaanisha uzao wake. "saidia uzao wako ... wabariki"
Hapa "mbinguni juu" ina maana ya mvua ambayo husaidia mazao kuota.
Hapa "chini" ina maana ya maji chini ya ardhi ambayo hutosheleza mito na visima.
Hapa "maziwa na tumbo" ina maana ya uwezo wa mama kupata watoto na kuwanyonyesha maziwa.
Yakobo anaendelea kumbariki Yusufu na uzao wake.
Maana ya lugha asili haipo wazi. Baadhi ya tafsiri za Biblia zina "mababu zangu" badala ya "milima ya zamani"
Hapa "viwe" ina maana ya baraka za baba yake.
Yakobo anatamani kwa baraka hizi kupitishwa hata kwa wale wazawa muhimu. "juu ya kichwa cha mzawa muhimu wa Yusufu"
"mtu muhimu wa ndugu zake"
Hapa "Benyamini" ni lugha nyingine ya uzao. Yakobo anazungumzia juu ya uzao wa Benyamini kana kwamba ulikuwa mbwa mwitu wenye njaa. Hii inasisitiza ya kwamba watakuwa wapiganaji hodari. "Uzao wa Benyamini watakuwa kama mbwa mwitu"
"Haya" ina maana ya wana wa Yakobo waliotajwa katika 49:1-27. Kila mwana alikuwa kiongozi wa kabila lake mwenyewe.
Hapa neno "alipowabariki" lina maana ya kuongelea baraka rasmi.
"Akawapa kila mtoto baraka inayomstahili"
"akawaamuru"
Hii ni njia ya upole ya kusema ya kwamba amekaribia kufa. "Nimekaribia kufa"
Yakobo ana maanisha pale ambapo nafsi yake utakwenda atakapokufa. Anategemea kuwaunga Abrahamu na Isaka katika maisha ya baadae.
Hili ni jina la mwanamume. "Mhiti" ina maana ya "uzao wa Hethi".
Makpela lilikuwa jina la eneo au mahali.
Hili lilikuwa jina lingine la mji wa Hebroni. Inawezekana lilitajwa baada ya Mamre, rafiki wa Abrahamu aliyeishi kule.
Yakobo anaendelea kuzungumza na wanawe.
Ununuzi unaweza kuwekwa wazi. "ndani mwake ulinunuliwa na Abrahamu"
"kutoka kwa Wahiti"
"alimaliza kuwaagiza wanawe" au "alimaliza kuwaamuru wanawe"
Yakobo alikuwa amekaa juu ya kitanda. Sasa, Yakobo anageuka na kuweka miguu yake kitandani ili aweze kulala chini.
Hii ni njia ya upole ya kusema mtu amekufa.
Baada ya Yakobo kufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile kama ndugu zake waliokufa kabla yake.