Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
"mtu akamwambia Yusufu"
"Sikiliza, baba yako". Hapa neno "tazama" linatumika kuvuta nadhari ya Yusufu.
"Kwa hiyo Yusufu akaondoka"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu alipomuambia Yakobo"
"mwanao Yusufu amekuja kwako"
Hapa mwandishi anazungumzia juu ya Israeli kuhangaika kuketi kitandani kana kwamba alikuwa akikusanya "nguvu" kama vile mtu akusanyavyo vitu halisia. "Israeli alifanya bidii kubwa kukaa kitandani" au "Israeli alihangaika alipokaa juu kitandani"
Hili ni jina la mji.
Hii inaweza kutafsiriwa kwa sentensi mpya ikianzia katika sehemu mpya. "katika nchi ya Kaanani, na akanibariki. Na akasema kwangu"
Hii ina maana ya Mungu kutamka baraka rasmi kwa mtu.
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "na kusema kwangu ya kwamba angenifanya niwe na uzao mwingi na kunizidishia. Na akasema ya kwamba angenifanya kuwa kusanyiko la mataifa na angenipa nchi hii kwa uzao wangu kama milki ya milele".
Mungu alitumia neno hili "tazama" hapa kumuamsha Yakobo kuvuta nadhari kwa kile alichokuwa akitaka kumwambia.
Msemo "kukuzidishia" unaelezea jinsi ambavyo Mungu angemfanya Yakobo "kupata uzao". "Nitakupatia uzao mwingi sana"
Hapa "nitakufanya" ina maana ya Yakobo, lakini ina maana ya uzao wa Yakobo. "Nitafanya vizazi vyako kuwa mataifa mengi"
"milki ya kudumu"
Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.
Efrahimu na Manase kila mmoja atapokea sehemu ya nchi kama ndugu zake Yusufu.
Maana zinawezekana kuwa 1) watoto wale wengine wa Yusufu wangerithi nchi kama sehemu ya makabila ya Efrahimu na Manase au 2) Yusufu atatengewa nchi na Efraimu na Manase na watoto wengine wa Yusufu watarithi nchi hiyo. "na kwa urithi wao, utawaorodhesha chini ya majina ya ndugu zao"
Hili ni jina lingine la mji wa Bethlehemu.
Mwandishi huyu anatoa taarifa ya nyuma.
"Hawa ni watoto wa nani?"
Baba huwa anatamka baraka rasmi juu ya watoto au wajukuu wake.
Neno "Basi" linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwenye simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Israeli.
"Israeli aliwabusu"
Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "Kukuona mara nyingine"
Yusufu alipowaweka wanawe juu ya mapaja ya Israeli au magotini ilikuwa ishara ya kwamba Israeli alikuwa akiwachukua. Hii iliwapa watoto hawa urithi maalumu kutoka kwa Yakobo.
Yusufu aliinama chini kuonyesha heshima kwa baba yake.
Yusufu anawaweka wavulana ili kwamba Israeli aweze kuweka mkono wake wa kuume juu ya Manase. Manase alikuwa ndugu mkubwa na mkono wa kulia ilikuwa ishara ya kwamba angepokea baraka kubwa.
Kuweka mkono wa kulia juu ya kichwa cha Efraimu ilikuwa ishara ya kwamba angepokea baraka kubwa.
Hapa "Yusufu" pia ina maana ya Efraimu na Manase. Kwa kuwa Yusufu ni baba, ni yeye pekee anayetajwa hapa.
Kumtumikia Mungu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kutembea mbele za Mungu. "Mungu ambaye babu yangu Abrahamu na baba yangu Isaka alimtumikia"
Mungu alimtunza Israeli kama vile mfugaji anavyotunza kondoo wake. "ambaye alinitunza kama mfugaji atunzavyo wanyama wake"
Maana zinawezekana kuwa 1) hii ina maana ya malaika ambaye Mungu alimtuma kumlinda Yakobo au 2) hii ina maana ya Mungu aliyemtokea kama malaika kumlinda Yakobo.
"aliniokoa"
Hapa "jina" lina maana ya mtu mzima. Msemo "jina langu na litajwe kwao" ni lahaja ambayo ina maana ya kwamba mtu anakumbukwa kwa sababu ya mtu mwingine. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Watu wamkumbuke Abrahamu, Isaka, na mimi kwa sababu ya Efraimu na Manase"
Hapa "wawe" ina maana ya Efraimu na Manase, lakini ina maana ya uzao wao. "Na wawe na uzao mwingi ambao utaishi ulimwenguni kote"
Mkono wa kulia ulikuwa ishara ya baraka kubwa ambayo mwana mkubwa alitakiwa kupokea.
Hapa "yeye" ina maana ya Manase, lakini inahusu uzao wake. "Mwana wako mkubwa atakuwa na uzao mwingi, nao watakuja kuwa taifa kubwa"
Hapa "maneno" ina maana ya kile kilichosemwa. "siku hiyo, akisema"
"Watu wa Israeli watazungumza majina yenu pale wanapowabariki wengine"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "kwa majina yenu. Watamuuliza Mungu kuwafanya wengine kama Efraimu na kama Manase"
Israeli kusema jina la Efraimu kwanza ni njia nyingine anaonyesha ya kwamba Efraimu atakuwa mkubwa kuliko Manase.
Kumpatia Efraimu baraka kubwa na kumfanya awe wa muhimu kuliko Manase inazungumziwa kana kwamba Israeli amemuweka kihalisia wa mwili Efraimu mbele ya Manase.
Hapa "nanyi" na "zenu" ni wingi na ina maana ya watu wote wa Israeli.
Hii ni lahaja yenye maana ya Mungu atasaidia na kubariki watu wa Israeli. "Mungu atakusaidia" au "Mungu atakubariki"
Hapa "atawarudisha" inaweza kutafsiriwa kama "kuchukua"
"nchi ya mababu zenu"
Maana zinawezekana kuwa 1) Yusufu kuwa na heshima na mamlaka zaidi kuliko ndugu zake inazungumziwa kana kwamba alikuwa juu yao kiuhalisia wa kimwili. "Kwako, ambaye ni mkubwa kuliko ndugu zako, ninakupa mteremko wa mlima" au 2) Yakobo ana maanisha anatoa nchi zaidi kwa Yusufu kuliko anavyotoa kwa ndugu wa Yusufu. "Kwako, ninakupa kilima kimoja zaidi ya nayowapatia ndugu zako. Ninakupatia mteremko wa mlima"
Hapa "wewe" ni umoja na ina maana ya Yusufu.
Hapa "upanga" na "upinde" ina maana ya kupigana vitani. "sehemu ya nchi niliyopigania na kuchukua kutoka kwa Waamori"