Hii ina maana hakuweza kuzuia hisia zake. Inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "alikuwa akitaka kuanza kulia"
"karibu naye"
Hapa "nyumba" ina maana ya watu katika kasri ya Farao. "kila mtu ndani ya kasri ya Farao"
"walimuogopa"
Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "ambaye mlimuuza kama mtumwa kwa wafanyabiashara walionileta huku Misri"
"msihuzunike" au "msiteseke"
Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "ya kwamba mliniuza kama mtumwa na kunituma huku Misri"
Hapa "uhai" ina maana ya watu ambao Yusufu aliwaokoa na kifo wakati wa njaa. "Ili niweze kuokoa maisha ya wengi"
"kutakuwa na miaka mitano zaidi bila ya kupanda au kuvuna". Hapa "bila ya kupanda au kuvuna" ina maana ya ukweli kwamba mimea haitaota kwa sababu ya ukame. "na njaa itadumu kwa miaka mitano zaidi"
"ili kwamba wewe na familia yenu msipotee kutoka duniani" au "kuhakikisha vizazi vyako vinaendelea kuishi"
Nomino inayojitegemea "ukombozi" inaweza kuwekwa kama "kuokoa". "kukuweka hai kwa kuwaokoa kwa njia ya juu"
Yusufu kumshauri na kumsaidia Farao inazungumziwa kana kwamba Yusufu alikuwa baba wa Farao. "amenifanya niwe kiongozi kwa Farao" au "amenifanya kuwa mshauri mkuu kwa Farao"
Hapa "nyumba" ina maana ya watu wanaoishi ndani ya kasri yake. "miongoni mwa nyumba yake yote" au "kati ya wote wa kasri yake"
Hapa "nchi" ina maana ya watu. "mtawala juu ya watu wote wa Misri"
Hapa Yusufu anamanisha ya kwamba yeye ni mtawala katika nafasi ya pili kutoka kwa Farao, mfalme wa Misri. Taarifa hii inayoeleweka inaweza kuwekwa wazi.
Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri. "kurudi kwa baba yangu"
Hii ni nukuu yenye madaraja matatu. Inaweza kurahisishwa katika madaraja mawili. "muambieni ya kwamba hivi ndivyo nilivyosema: "Mungu amenifanya ... yote uliyonayo"
Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri. "Njooni hapa kwangu"
Hii inazungumzia kuhusu "uhitaji" kana kwamba ilikuwa kikomo cha safari. "kupotea bure" au "kushinda njaa"
Neno "macho" ina maana ya mtu mzima. "Nyie wote na Benyamini mnaweza kuona"
Neno "kinywa" ina maana ya mtu mzima. "ya kwamba mimi, Yusufu, nazungumza na nyinyi"
"jinsi watu wa Misri wanavyoniheshimu sana"
Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri. "baba yangu huku kwangu"
"Yusufu alimkumbatia ndugu yake Benyamini, na wote wakalia"
Katika kipindi cha zamani cha Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimia jamaa kwa busu.
Hii ina maana ya Yusufu alilia alipowabusu.
Awali walikuwa na hofu juu yake. Sasa walijisikia wanaweza kuongea naye kwa uhuru. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Baada ya hapo ndugu zake waliongea naye kwa uhuru"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. Pia hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kila mtu katika kasri ya Farao alisikia ya kwamba ndugu zake Yusufu walikuja"
Hii ina maana ya kasri ya Farao
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Waambie ndugu zako kupakiza wanyama wao na kwenda Kaanani kumfuata baba yao na familia zao. Waambie waje hapa, nami nitawapa ardhi nzuri katika Misri na chakula bora tunachoweza kutoa"
"Nitawapa sehemu bora ya nchi ya Misri"
Chakula bora ambacho nchi huzaa inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni sehemu nene ya nchi. "utakula chakula bora katika nchi"
Farao anaendelea kumwambia Yusufu kipi cha kuwaambia ndugu zake.
Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "pia waambie kuchukua mikokoteni kutoka katika nchi ya Misri kwa ajili ya watoto na wake zao, na kumchukua baba yao aje hapa. Hawatakiwi kuwa na wasiwasi kuhusu kuleta mali zao, kwa maana nitawapatia mambo mazuri tuliyonayo ndani ya Misri"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nami nakuamuru kuwaambia" au "pia waambie"
"Mikokoteni" ni gari dogo la abiria na mizigo lenye magurudumu mawili au manne. Wanyama huvuta mikokoteni.
"na kuwapa walichohitaji kwa ajili ya safari yao"
Kila mtu alipokea idadi ya nguo mbili isipokuwa kwa Benyamini aliyepokea idadi ya nguo tano.
"vipande 300"
Punda walijumlishwa kama sehemu ya zawadi.
Maana zaweza kuwa 1) "msibishane" na 2) "msiwe na hofu"
Ilikuwa kawaida kutumia neno "panda" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.
Hapa "nchi ya Misri" ina maana ya watu wa Misri. "anatawala watu wote wa Misri"
Hapa "moyo" ina maana ya mtu mzima. "na alishtuka" au "na alishangazwa sana"
"hakupokea kile walichosema kilikuwa ni cha kweli"
"Wakamwambia Yakobo"
Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "kila kitu ambacho Yusufu alikisema kwao"
Neno la "roho" lina maana ya mtu mzima. "Yakobo baba yao alipona" au "Yakobo baba yao akawa na furaha sana"