Hii inaanza sehemu mpya ya tukio katika simulizi. Inawezekana hii ni asubuhi iliyofuata baada ya sherehe.
"msimamizi" alikuwa na wajibu wa kusimamia matukio ya nyumba ya Yusufu.
Pesa yao ilikuwa sarafu za fedha yawezekana ndani ya mfuko mdogo.
"katika gunia lake"
"Weka kikombe changu cha fedha"
Neno "ndugu" linaeleweka. "ndani ya gunia la ndugu mdogo"
"Mwanga wa asubuhi ulionekana"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "waliwatuma watu waondoke, pamoja na punda zao"
Swali hili linatumiwa kukaripia wale ndugu. "Mmetutendea vibaya, baada ya sisi kuwa wema kwenu!"
Swali hili linatumika kukaripia wale ndugu. "Tayari mnafahamu ya kwamba hiki ni kikombe ambacho bwana wangu hutumia kunywea na kwa uaguzi!"
Hii inarudia "mmefanya" kuonyesha msisitizo. "Kile mlichofanya ni kibaya sana"
Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "alizungumza kile Yusufu alichomuambia kusema"
Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. Ndugu wanataja msimamizi kama "bwana wangu". Hii njia maalumu ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Kwa nini unasema hivi, bwana wangu?"
Ndugu wanajitambua wenyewe kama "watumishi wako" na "wao". Hii ni njia maalumu ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. "Hatuwezi kufanya jambo kama hilo!"
Jambo ambalo mtu hawezi kufanya inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anataka kukiweka mbali nacho.
Hii inaongeza msisitizo kwa kile ndugu wanasema baadae.
"unajua pesa ambayo tumeipata ndani ya magunia yetu"
"tumerudisha kwako kutoka Kaanani"
Ndugu wanatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hawawezi kuiba kutoka katika bwana wa Misri. "Kwa hiyo hatuwezi kuchukua kitu chochote kutoka kwenye nyumba ya bwana wako!"
Maneno haya yanatumiwa pamoja kumaanisha ya kwamba hawawezi kuiba kitu chochote chenye thamani yoyote.
Ndugu wanajitambua wao kama "watumishi wako". Hii njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu mmoja. Pia, "kitakayeonekana" linaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Ukikuta ya kwamba mmoja wetu ameiba kikombe"
Msemo "bwana wangu" una maana ya mtunzaji. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Unaweza kutuchukua kama watumwa wako"
Hapa "basi" haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata. Pia "maneno" ina maana ya kile kilichosemwa. "Vizuri sana. Nitafanya kile ulichosema"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kama nikikuta kikombe ndani ya moja ya magunia yenu, mtu huyo atakuwa mtumwa wangu"
"akateremsha gunia lake"
Neno "ndugu" linaeleweka. "ndugu mkubwa ... ndugu mdogo wa wote"
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya na katika hali ya kutenda. "mdogo wa wote. Mtunzaji alikuta kikombe ndani ya gunia la Benyamini"
Neno "wakararua" ina maana ya wale ndugu. Kurarua nguo ilikuwa ishara ya dhiki na majonzi makubwa.
"na wakarudi"
"Yusufu alikuwa bado yupo pale"
"wakaanguka mbele yake". Hii ni ishara ya ndugu kutaka bwana awe na huruma kwao.
Yusufu anatumia swali kukaripia ndugu zake. "Hakika mnajua ya kwamba mtu kama mimi naweza kujifunza mambo kwa uaguzi!"
Maswali yote 3 yana maana moja. Wanatumia maswali haya kuweka msisitizo ya kwamba hakuna kitu wanaweza kusema kuelezea kilichotokea. "Hatuna kitu cha kusema, bwana wangu. Hatuwezi kuzungumza jambo lolote la maana. Hatuwezi kujithibitisha"
Hapa "bwana wangu" ina maana ya Yusufu. Hii njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "Tunaweza kusema nini kwako ... watumwa wako"
Hapa "ameona" haimaanishi Mungu ameona tu kile ndugu walichofanya. Ina maana Mungu sasa anawaadhibu kwa kile walichofanya. "Mungu anatuadhibu kwa dhambi zetu za zamani"
Ndugu wanajitambulisha wenyewe kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "dhambi zetu"
Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. Pia, "kimeonekana" inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "na yule ambaye alikuwa na kikombe"
Kitu ambacho mtu hawezi kufanya inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu mtu anataka kuweka mbali na yeye. "sio kawaida yangu kufanya jambo kama hili"
Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. Pia, "kimeonekana" inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "mtu aliyekuwa na kikombe changu"
"akakaribia"
Yuda anajitambulisha kama "mtumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza kwa mtu mwenye mamlaka zaidi. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "niruhusu mimi, mtumishi wako"
Hapa "neno" ni lugha nyingine yenye maana ya kile kilichosemwa. Na "masikio" ni lugha nyingine yenye maana ya mtu mzima. "kuzungumza na wewe, bwana wangu"
Hapa "bwana wangu" ina maana ya Yusufu. Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "kwako"
Kuwa na hasira inazungumzwa kana kwamba ilikuwa moto unawaka. "tafadhali usiwe na hasira na mimi, mtumishi wako"
Yuda anamlinganisha bwana yule na Farao kusisitiza nguvu kubwa ambayo bwana yule alikuwa naye. Pia anadokeza ya kwamba hakutaka bwana kuwa na hasira na kumuadhibu. "kwa maana wewe kama Farao mwenye mamlaka na unaweza kuwaamuru askari wako kuniua"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Bwana wangu alituuliza kama tuna baba na ndugu"
Yuda anamtambua Yusufu kwa maneno haya "bwana wangu" na "wake". Pia anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wake". "Wewe, bwana wangu, alituuliza, watumishi wako" au "Ulituuliza"
Yuda anaendelea kuzungumza mbele ya Yusufu.
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Nasi tukamwambia bwana wetu ya kwamba tuna baba ... baba yake anampenda"
Yuda anamtambua Yusufu kama "bwan wangu". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. "tulisema kwako, bwana wangu"
Hii ina maana ya upendo kwa rafiki au mmoja wa familia.
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Nawe ukasema kwa mtumishi wako ya kwamba tunapaswa kumleta ndugu yetu mdogo kwako ili uweze kumuona"
Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". "Kisha ulisema kwetu, watumishi wako"
Ilikuwa kawaida kutumia neno "chini" pale ilipozungumziwa safari ya kutoka Kanaani kwenda Misri. "Mleteni kwangu"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kwa kujibu, tulisema kwa bwana wangu ya kwamba kijana hawezi ... baba yake angekufa"
Inadokezwa ya kwamba baba yao angekufa kwa huzuni.
Yuda anaendelea simulizi yake kuhusu Yusufu.
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kisha ulisema kwa watumishi wako ya kwamba hadi pale ndugu yetu mdogo aje pamoja nasi, hatutaweza kukuona tena"
Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. "Kisha ukasema kwetu, watumishi wako"
Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.
Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "Hamtaniona tena"
Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kwenda" kuzungumzia safari kutoka Misri kwenda Kaanani.
Yuda anamtambua Yusufu kama "bwana wangu". Pia "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "tulimwambia ulichosema, bwana wangu"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Baba yetu alituambia kurudi tena Misri kununua chakula kwa ajili yetu na familia zetu"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kisha tukamwambia ya kwamba hatuwezi kushuka Misri. Tulimwambia ya kwamba iwapo ndugu yetu mdogo atakuwa pamoja nasi ... pamoja nasi"
Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "kumuona yule mtu"
Yuda anaendeleza simulizi yake kwa Yusufu
Hii ina madaraja mawili na daraja la tatu la nukuu. Yanaweza kuwekwa kama nukuu zisikzokuwa moja kwa moja. "akatuambia ya kwamba tunafahamu ya kuwa mke wake, Raheli, alimzalia watoto wawili tu, na kwamba mmoja wao alitoweka na mnyama alimrarua vipande vipande, na hajamuona tangu siku hiyo, kisha tutamfanya afe kwa huzuni"
Hapa "akatuambia" haimjumlishi Yusufu.
Hapa "mnajua" ni wingi na ina maana ya wale ndugu.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mnyama pori alimrarua vipande vipande"
Jambo baya linalotokea kwa mtu inazungumziwa kana kwamba "baya" lilikuwa kitu ambacho husafiri na kuja kwa mtu.
"kushusha ... Kuzimu" ni njia ya kusema watasababisha afariki na kushuka Kuzimu. Anatumia neno "shuka" kwa sababu iliaminika Kuzimu ilikuwa sehemu ya chini. "kisha mtanisababisha, mtu mzee, kufa kwa huzuni"
Hii ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "mimi, mtu mzee"
Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika hapa kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.
Yuda anaelezea kwa Yusufu suala la ukweli lakini la kubuni ambalo linatarajiwa kutokea kwa Yakobo atakaporudi bila Benyamini.
Hapa "nitakapokuja" inaweza kutafsiriwa kama "kwenda" au "kurudi".
"kijana hayupo pamoja nasi"
Baba anasema ya kwamba atakufa iwapo mwanawe atangekufa inazungumziwa kana kwamba maisha yao mawili yaliunganishwa pamoja kimwili. "kwa maana alisema angekufa iwapo kijana hangerudi"
Yuda anazungumzia kuhusu suala la kubuni katika wakati wa mbele kana kwamba ingetokea kweli.
"watazishusha ... Kuzimu" ni njia ya kusema watasababisha afariki na kushuka Kuzimu. Anatumia neno "shuka" kwa sababu iliaminika Kuzimu ilikuwa sehemu ya chini. "kisha mtanisababisha, mtu mzee, kufa kwa huzuni"
Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. "Nasi, watumishi wako" au " Na sisi"
Hapa "mvi" ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "baba yetu mzee"
Nomino hii inayojitegemea "mdhamini" inaweza kuwekwa kama kitenzi "aliahidi". "Maana nimuahidi baba yangu kuhusu kijana huyu"
Yuda anajitambulisha kama "mtumishi wako". "Kwa maana mimi, mtumishi wako" au "Kwa maana mimi"
Kuchukuliwa mwenye hatia inazungumziwa kana kwamba "hatia" ilikuwa kitu ambacho mtu hubeba. "kisha baba yangu anaweza kunilaumu"
Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.
Yuda anajitambulisha mwenyewe kama "mtumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. "niruhusu mimi, mtumishi wako" au "niruhusu mimi"
Yuda anamtambua Yusufu kama "bwana wangu". "kwako, bwana wangu" au "kwako"
Alikuwa akienda kutumia msemo wa "aende juu" pale alipozungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.
Yuda anatumia swali kuweka msisitizo wa majonzi ambayo angeyapata iwapo Benyamini asingerudi nyumbani. "Siwezi kurudi kwa baba yangu iwapo kijana hatakuwa pamoja nami"
Mtu anayeteseka vibaya inazungumziwa kana kwamba "uovu" ilikuwa kitu kinachokuja juu ya mtu. "Ninaogopa kumuona jinsi baba yangu atakavyoteseka"