Neno "Kaanani" linaeleweka. Taarifa hii inaweza kuwekwa wazi. "Njaa ilikuwa kali katika nchi ya Kaanani"
Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
"Yakobo na familia yake walipokuwa wamekula"
"wana wakubwa wa Yakobo walileta"
Hapa "mtununulie" ina maana ya Yakobo, wanawe, na familia yake iliyobaki.
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"
Hii ina maana ya Yusufu, lakini ndugu hawakujua alikuwa Yusufu. Walimtaja kama "mtu" au "yule mtu, bwana wa nchi" kama katika 42:29.
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"
"alikuwa na hali ya ukali alipotuonya, akisema"
Yuda anatumia msemo huu mara mbili katika 43:3-5 kuweka msisitizo kwa baba yake ya kwamba hawawezi kurudi Misri bila Benyamni. Msemo "uso wangu" una maana ya yule mtu, ambaye ni Yusufu. "Hamtaniona"
Yuda ana maana ya Benyamini, mtoto wa Raheli wa mwisho kabla yeye hajafa.
Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.
"Kwa nini mlinisababishia matatizo makubwa hivi"
"Yule mtu aliuliza maswali mengi"
Hapa "yetu" inajitegemea na ina maana ya ndugu waliokwenda Misri na kuzungumza na"yule mtu".
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Alituuliza kwa kuzunguka kama baba yetu alikuwa bado yu hai na kama tuna ndugu mwingine".
"Tulimjibu maswali aliyotuuliza"
Wana hawa wanatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hawakujua ni kitu gani yule mtu angewaambia kufanya. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hatukujua ya kwamba angetuambia ... chini!"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "angetuambia kumfuata ndugu yetu huku chini Misri"
Ilikuwa kawaida kutumia neno la "chini" katika kuzungumzia safari ya kutoka Kanaani kwenda Misri.
Misemo hii "ili kwamba tuishi" pamoja na "tusife" ina maana moja. Yuda anaweka msisitizo ya kwamba wanalazimu kununua chakula Misri ili kwamba waishi. "Tutakwenda Misri na kupata nafaka ili familia yetu yote iweze kuishi"
Hapa "tutainuka" ina maana ya ndugu ambao watasafiri kwenda Misri.
Hapa "tuishi" ina maana ya ndugu, Israeli na familia nzima.
Hapa "sisi" ina maana ya hawa ndugu.
Hapa "wewe" ni umoja na ina maana ya Israeli.
Hapa "wetu" ina maana ya hawa ndugu. Hii ina maana ya watoto wadogo ambao wangeweza kufa katika kipindi cha njaa.
Nomino inayojitegemea "mdhamini" inaweza kuwekwa kama kitenzi "ahidi". "Ninaahidi kumrudisha"
Jinsi ambavyo Yakobo atamuwajibisha Yuda inaweza kuwekwa wazi. "Utanifanya niwajibike kwako kuhusu kitakachotokea kwa Benyamini"
Hii inazungumzia kuhusu "lawama" kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kubeba. "Unaweza kunilaumu"
Yuda anaelezea jambo ambalo lingetokea hapo nyuma lakini halikutokea. Yuda anamkaripia baba yake kwa kusubiri muda mrefu sana kuwatuma wanawe Misri kufuata chakula zaidi.
"tungekuwa tumerudi mara mbili"
"Iwapo huu ni uchaguzi wetu pekee, basi fanyeni"
Ilikuwa kawaida kutumia neno "chini" katika kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.
kitu chenye mafuta chenye harufu tamu kinachotumiwa kwa ajiliya kuponya na kulinda ngozi. "dawa"
vikolezo
karanga ndogo, itokayo kwenye mti wa kijani
karanga ya mti yenye ladha tamu
Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. "Chukua mara mbili ya pesa pamoja nawe"
Hapa "mikononi" ina maana ya mtu mzima. Msemo wa "iliyorudishwa" unaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "pesa iliyowekwa kwenye magunia yenu na mtu, muirudishe Misri"
"Mchukueni pia Benyamini"
"mrudi"
Nomino inayojitegemea "rehema" inaweza kuwekwa kama kivumishi "huruma". "Mungu mwenye uwezo asababishe yule mtuawe na huruma kwenu"
"Simoni"
"Kama nikipoteza watoto wangu, basi nipoteze watoto wangu". Hii ina maana ya kwamba Yakobo anajua inapaswa akubali kitakachotokea kwa watoto wake.
Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Wakachukua"
Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.
"Benyamini pamoja na ndugu wa Yusufu wakubwa"
"Mtunzaji" aliwajibika na kusimamia matukio ya nyumba ya Yusufu.
Hapa "akawaleta" inaweza kutafsiriwa kama "kuwachukua"
"ndani ya nyumba ya Yusufu"
"Ndugu wa Yusufu waliogopa"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "walikwenda ndani ya nyumba ya Yusufu" au "mtunzaji aliwapeleka ndani ya nyumba ya Yusufu"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtunzaji anatuleta ndani ya nyumba kwa sababu ya pesa ambayo mtu alirudisha ndani ya magunia yetu"
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Anasubiria nafasi ya kutushtaki, ili kwamba aweze kutukamata"
Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.
Ndugu wanaendelea kuzungumza na mtunzaji wa nyumba.
Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio muhimu la simulizi.
"tulipofika mahali ambapo tulikwenda kukaa usiku ule"
Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba ndugu walishangazwa kwa kile walichokiona.
"kila mmoja wetu alikuta pesa kamili katika gunia lake"
Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Tumerudisha pesa pamoja nasi"
Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Tumekuja na pesa zaidi pia kununua chakula zaidi"
Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.
Nomino inayojitegemea "Amani" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "Tulia" au "Tulieni"
Mtunzaji hazungumzi kuhusu Mungu wawili tofauti. "Mungu wenu, Mungu ambaye baba yenu anamwabudu"
Utamaduni huu ulisaidia wasafiri waliochoka kujiburudisha baada ya kutembea umbali mrefu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.
"malisho" ni chakula kilichokauka ambacho huwekwa kando kwa ajili ya wanyama.
Hapa "mikononi" ina maana ya mtu mzima. "ndugu hawa walileta zawadi ambazo walikuwa nazo"
Hii ni njia ya kuonyesha heshima na taadhima.
Walimuelezea baba yao kama "Mtumishi wako" kuonyesha heshima. "Baba yetu anayekutumikia"
Maneno haya yana maana moja. Walilala chini mbele ya yule mtu kumuonyesha heshima. "Waliinama chini mbele yake"
Hii ina maana "alitazama juu"
Hii inaweza kutafsiriwa na sentensi mpya. "mwana wa mamaye. Yusufu akamwambia"
Maana zaweza kuwa 1) Yusufu anauliza kwa dhati swali kupata uthibitisho ya kwamba mtu huyu ni Benyamini, au 2) ni swali la balagha. "Kwa hiyo huyu ndiye ndugu yenu mdogo ... mliyesema?"
Hii ni njia ya kirafiki mtu huzungumza kwa mtu mwingine wa cheo cha chini. "kijana"
"aliharakisha nje ya chumba"
Msemo "aliguswa sana" una maana ya kuwa na huruma kubwa au hisia ambapo jambo muhimu hutokea. "kwa maana alipatwa na hisia kali za huruma kwa nduguye" au "kwa maana akawa na hisia za upendo kwa ndugu yake"
Inaweza kuwekwa wazi ni kwa nani Yusufu anazungumza. "na akasema kwa watumishi wake"
Hii ina maana ya kusambaza chakula ili kila mtu aweze kula.
Hii ina maana ya kwamba Yusufu, ndugu zake, na Wamisri wengine wanakula katika sehemu tatu tofauti ndani ya chumba kimoja. "Watumishi walimhudumia Yusufu peke yake na ndugu zake peke yao na Wamisri, ambao walikuwa wakila naye, peke yao"
Inawezekana hawa ni maafisa Wamisri wengine ambao walikula pamoja na Yusufu, lakini bado waliketi tofauti kutoka kwake na ndugu zake wa Kiebrania.
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Walifanya hivi kwa sababu Wamisri walidhani ilikuwa aibu kula pamoja na Waebrania"
Hapa "mkate" ina maana ya chakula kwa ujumla.
Inasemekana ya kwamba Yusufu alipanga ni wapi kila ndugu angeketi. Unaweza kuweka wazi taarifa iliyodokezwa. "Ndugu walikaa upande wa pili na yule mtu, kulingana na jinsi alivyopanga nafasi zao"
"mzaliwa wa kwanza" na "mdogo kuliko wote" inatumika pamoja kumaanisha ya kwamba ndugu wote walikaa kulingana na umri wao.
"Hawa watu walishangazwa walipogundua hili"
Msemo "mara tano" unaweza kuwekwa kwa ujumla zaidi. "Lakini Benyamini alipokea sehemu ambayo ilikuwa kubwa zaidi ya kile walichopokea ndugu zake"