Neno "basi" inaweka alama ya sehemu mpya ya simulizi.
Yakobo anatumia swali kukaripia watoto wake kwa kutofanya kitu chochote kuhusu nafaka. "Msikae hapo tu!"
Ilikuwa kawaida kuzungumza kuhusu kwenda kutoka Kaanani mpaka Misri kama kwenda "chini"
Hapa "Misri" ina maana ya watu kuuza nafaka. "kutoka kwa wale wauzao nafaka ndani ya Misri"
Benyamini na Yusufu walikuwa na baba mmoja na mama. Yakobo hakutaka kuthubutu kumtuma mwanawe wa mwisho wa Raheli.
Neno "wakaja" inaweza kutafsiriwa kama "kwenda". Pia, maneno "nafaka" na "Misri" inaeleweka. "Wana wa Israeli walikwenda kununua nafaka pamoja na watu wengine waliokwenda Misri"
"Basi" inaweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa maelezo ya nyuma kuhusu Yusufu.
Hapa "nchi" ina maana ya Misri. "juu ya Misri"
Hapa "nchi" inajumlisha Misri na nchi zingine zinayoizunguka. "watu wote wa mataifa yote waliokuja kununua nafaka"
Hapa "wakaja" inaweza kutafsiriwa kama "walikwenda"
Hii ni njia ya kuonyesha heshima.
"Yusufu alipowaona ndugu zake, aliwatambua"
"alijifanya kana kwamba hakuwa kaka yao" au "hakuwafahamisha ya kwamba alikuwa kaka yao"
Hili halikuwa swali la balagha ingawa Yusufu alijua jibu. Ilikuwa sehemu ya maamuzi yake kuficha utambulisho wake kwa ndugu zake.
Wapelelezi ni watu ambao kwa siri hujaribu kupata taarifa kuhusu nchi ili kuisaidia nchi nyingine.
Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Mmekuja kujua ni wapi hatulindi nchi yetu ili kwamba muweze kutushambulia"
Hii ni njia ya kuonyesha heshima kwa mtu.
Ndugu hawa wanajitambulisha kama "watumishi". Hii ni njia maalumu ya kuongea na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. "Sisi, watumishi wako, tumekuja" au "Tumekuja"
"Yusufu akawaambia ndugu zake"
Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Hapana, mmekuja kujua ni wapi hatujalinda nchi yetu ili kwamba muweze kutuvamia"
"ndugu 12"
"Tusikilize, mdogo". Neno "Tazama" linatumika kusisitiza kile walichosema baadae.
"kwa sasa ndugu yetu mdogo yupo na baba yetu"
"kama nilivyotangulia kusema, nyinyi ni wapelelezi"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hivi ndivyo nitakavyowajaribu"
Msemo huu unaashiria kiapo maalumu.
"Chagueni mmoja wenu kumfuata mdogo wenu"
"Mliosalia mtabaki gerezani"
Hapa "maneno" ina maana ya kile alichosema. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba niweze kujua kama mnaniambia ukweli"
"gerezani"
Neno "tatu" ni mpangilio wa namba."baada ya siku ya pili"
Taarifa inayotambulika inaweza kuwekwa wazi. "Kama utafanya kile nilichosema, nitakuruhusu uishi"
Hii ina maana ya kumheshimu Mungu kwa dhati na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii yeye.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "muache mmoja wa ndugu zako hapa gerezani"
Hapa "ninyi" ni wingi na ina maana ya ndugu wote ambao hawatakaa gerezani. "lakini ninyi mliosalia"
Hapa "nyumba" ina maana ya familia. "beba nafaka hadi nyumbani kusaidia familia zenu wakati wa njaa hii"
Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili niweze kujua kile mnachosema ni kweli"
Hii inaashiria ya kwamba Yusufu angewafanya maaskari wake kuwaua ndugu iwapo angetambua ya kwamba walikuwa wapelelezi.
Neno "nafsi" ina maana ya Yusufu. "kwa sababu tuliona jinsi gani Yusufu alivyotaabika" au "kwa sababu tuliona ya kwamba Yusufu aliteseka"
Nomino inayojitegemea "taabu" inaweza kuwekwa kama kitenzi "kuteseka" "Ndio maana tunateseka hivi sasa"
Rubeni anatumia swali kuwakaripia ndugu zake. "Niliwaambia kutomuumiza kijana, lakini hamkunisikiliza!"
Hii inaweza kuwa nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Je sikuwaambia msimtendee dhambi kijana" au "Niliwaambia msimdhuru kijana"
Hapa "basi" haimaanishi "katika muda huu" lakini yote maneno "Sasa" na "tazama" yanatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.
Hapa "damu" ina maana ya kifo cha Yusufu. Ndugu zake walidhani Yusufu alikufa. Msemo "inatakiwa juu yetu" una maana wanatakiwa kuadhibiwa kwa kile walichokifanya. "tunapata kile tunachostahili kwa kifo chake" au"tunateseka kwa kumuua yeye"
Hii inabadilisha kutoka kwenye simulizi kuu kwenda kwenye taarifa ya nyuma ambayo inaelezea kwa nini ndugu walidhani Yusufu hakuweza kuwaelewa.
"Mkalimani" ni mtu ambaye hutafsiri kile mtu anazungumza katika lugha nyingine. Yusufu aliweka mkalimani kati yake na ndugu zake kufanya ionekane kana kwamba hakuzungumza lugha yake.
Inasemekana ya kwamba Yusufu alilia kwa sababu alipatwa na hisia baada kusikia walichosema ndugu zake.
Yusufu aliendelea kuzingumza katika lugha nyingine na kutumia mkalimani kuzungumza na ndugu zake.
Hapa "macho" ina maana ya machoni mwao. "alimfunga machoni mwao" au "alimfunga huku wakitazama"
"kuwapatia mahitaji waliyohitaji"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Watumishi walifanya kwao kila kitu ambachoYusufu aliwaamuru"
"Waliposimama mahali usiku huo, mmoja wa ndugu alifungua gunia lake kupata chakula kwa ajili ya punda wake. Ndani ya gunia akakuta fedha!"
Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa inayoshangaza inayofuata.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu amerudisha fedha yangu"
"Tazama ndani ya gunia langu!"
Kuwa na hofu inazungumziwa kana kwamba mioyo yao ilikuwa ikizama. Hapa "mioyo" ina maana ya ujasiri. "Wakawa na hofu sana"
"bwana wa Misri"
"aliongea kwa jazba"
Wapelelezi ni watu ambao kwa siri hujaribu kupata taarifa kuhusu nchi ili kuisaidia nchi nyingine.
Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Tulimwambia ya kwamba sisi ni watu waaminifu na sio wapelelezi. Tulisema kwamba tu ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu, na kwamba ndugu yetu hayupo hai tena ... nchi ya Kaanani"
Neno "ndugu" linaeleweka. "Ndugu mmoja hayupo hai tena"
Neno "ndugu" linaeleweka. "ndugu yetu mdogo yupo na baba yetu kwa sasa"
"bwana wa Misri"
Hapa "nyumba" ina maana ya "familia". "chukua nafaka isaidie familia yenu wakati wa njaa"
"nendeni nyumbani" au "ondokeni"
"na nitawaruhusu mnunue na kuuza katika nchi hii"
Msemo huu unatumika hapa kuweka alama kwa tukio muhimu katika simulizi.
"kwa mshangao wao". Neno "tazama" hapa inaonyesha ya kwamba ndugu walishangazwa kwa kile walichokiona.
"umeninyima watoto wangu" au "umesababisha kupoteza watoto wangu wawili"
"mambo haya yote yaliniumiza"
Hili ni ombi la Rubeni kumchukua Benyamini pamoja naye na kumtunza katika safari hiyo. "Niweke kama msimamizi juu yake" au "Niache nimtunze"
Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" walipokuwa wakizungumzia safari ya Kaanani kuelekea Misri. "Mwanangu, Benyamini, hatakwenda nawe hadi Misri"
Hapa "nanyi" ni wingi na ina maana ya wana wa yakobo wakubwa.
Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Kwa maana mke wangu, Raheli, alikuwa na watoto wawili pekee. Yusufu amekufa na Benyamini amebaki mwenyewe tu"
"utakapokuwa ukisafiri kwenda Misri na kurudi" au "utakapokuwa mbali". Hapa "njia" ina maana ya kusafiri.
"mtakapozishusha ... kuzimu" ni njia ya kusema watamsababisha afariki na kushuka kuzimu. Anatumia neno "chini" kwa sababu iliaminika kuzimi ni sehemu chini ya ardhi. "basi mtanisababisha, mtu mzee, kufariki na huzuni"
Hii ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "mimi, mtu mzee"