Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
Miaka miwili ilipita baada ya Yusufu kutafsiri kwa usahihi ndoto za mnyweshaji wa Farao na mwokaji, ambao walikuwa gerezani pamoja na Yusufu.
Neno "tazama" hapa linaweka alama ya mwanzo wa tukio jipya katika simulizi kuu.
"Farao alikuwa amesimama"
"Ghafla". Neno la "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa kwa kile alichokiona.
"wenye afya na wanene"
"walikuwa wakila nyasi kando kando ya mto"
nyasi ndefu, nyembamba ambazo huota katika maeneo ya unyevunyevu
Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa tena kwa kile alichokiona.
"wagonjwa na wembamba"
"kando kando ya mto" au "kando ya mto". Hii ni sehemu ya juu ya ardhi pembeni mwa mto.
"dhaifu na nyembamba"
"yenye afya na iliyolishwa vizuri"
"aliamshwa"
Neno "mara ya pili" ni mpangilio wa namba. "tena"
Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa kwa kile alichokiona.
Vichwa ni sehemu ya mmea wa mahindi ambao mbegu huota.
"yaliota katika shina moja" Shina ni sehemu nene au ndefu ya mmea.
"katika mche mmoja na ilikuwa yenye afya na nzuri"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo ilikuwa nyembamba na kuchomwa kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"
Upepo kutoka mashariki ulivuma kutoka jangwani. Joto la upepo wa mashariki mara kwa mara ulikuwa wenye uharibifu.
"yaliota" au "kukua"
Maneno "ya mbegu" inaeleweka. "Vichwa vyembamba vya mbegu"
"wakala". Farao anaota ya kwamba mahindi ambayo hayana afya yanaweza kumeza mahindi yenye afya kama mtu anavyokula chakula.
"vichwa vyenye afya na vizuri"
"aliamshwa"
Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa na kile alichokiona.
"alikuwa akiota"
Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
Hapa neno "roho" lina maana ya utu wake na hisia zake. "alifadhaishwa ndani ya utu wake" au "alisononeshwa"
Inaeleweka ya kwamba aliwatuma watumishi. "Alituma watumishi wake kuwaita" au "Aliwatuma watumishi wake na kuwaita"
Wafalme wa zamani na watawala walitumia wachawi na wenye hekima kama washauri.
Mtu muhimu zaidi ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.
Neno "Leo" linatumika kuonyesha msisitizo. "makosa" yake ni kwamba alitakiwa kumwambia Farao kitu mapema zaidi lakini hakufanya hivyo. "Nimegundua ya kwamba nimesahau kukuambia jambo"
Mnyweshaji ana maana ya Farao katika mtu wa utatu. Hii ni njia ya kawaida ya mtu mwenye nguvu ya chini kuzungumza na mtu mwenye nguvu zaidi. "Wewe, Farao, ulikuwa na hasira"
Hapa "wake" ina maana ya Farao. Hapa "watumishi" ina maana ya mnyweshaji na mkuu wa waokaji. "na sisi, watumishi wako"
"kuniweka mkuu wa waokaji na mimi gerezani ambapo kapteni wa walinzi alikuwa msimamizi" hapa "nyumba" ina maana ya gereza.
Askari msimamizi wa walinzi wa kifalme.
Mtu muhimu zaidi ambaye alitengeneza chakula kwa ajili ya mfalme.
"Usiku mmoja wote wawili tulipata ndoto"
Hapa "Tuliota" ina maana ya mkuu wa mnyweshaji na mkuu wa waokaji.
"Ndoto zetu zilikuwa na maana tofauti"
Mkuu wa wanyweshaji anaendelea kuzungumza na Farao.
"Gerezani kulikuwa na mkuu wa waokaji na mimi"
Askari msimamizi wa walinzi wa kifalme.
"Tulimwambia ndoto zetu na kutueleza maana zake kwetu"
Hapa "yake" ina maana ya mnyweshaji na muokaji mmoja mmoja, sio kwa yule anayetafsiri ile ndoto. "Alifafanua kile kilichokuwa kinakuja kutokea kwetu wawili"
Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio muhimu la simulizi.
"alivyotafsiri kuhusu ndoto ndivyo kilichotokea hapo baadae"
Hapa mnyweshaji anatumia jina la Farao katika kuongea naye kama njia ya kumheshimu yeye. "Uliniruhusu nirudi katika kazi yangu!"
"mkuu wa waokaji"
Hapa "akamtundika" ina maana ya Farao. Na ina maana ya maaskari ambao Farao aliwaamuru kumnyonga mkuu wa waokaji. "uliwaamuru maaskari wako kumnyonga"
Inaeleweka ya kwamba Farao aliwatuma watumishi. "Farao aliwatuma watumishi wake kumfuata Yusufu"
"nje ya gereza" au "nje ya ile jela"
Ilikuwa utaratibu wa kawaida kunyoa ndevu na nywele za kichwani mnapoandaa kwenda mbele ya Farao.
Hapa "akaingia" inaweza kuwekwa kama "kwenda". "alikwenda mbele ya Farao"
"hakuna awezaye kueleza maana yake"
"unaweza kuelezea maana yake"
"Mimi siye ambaye naweza kueleza maana yake"
"Mungu atamjibu Farao kwa fadhila"
Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.
Hii ni ardhi iliyo juuzaidi katika ukingo wa Mto Nile.
Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.
"waliolishwa vizuri na wenye afya"
"walikuwa wakila nyasi kando ya mto"
Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.
"dhaifu, na wembamba"
Nomino inayojitegemea ya "kutotamanika" inaweza kutafsiriwa kwa kivumishi. "ng'ombe wabaya sana" au "ng'ombe wasiofaa kabisa"
"ng'ombe waliolishwa vizuri"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hakuna aliyeweza kutambua ya kwamba ng'ombe wembamba waliwameza ng'ombe wanene"
Farao anaendelea kumwambia Yusufu ndoto zake.
Hii inaanza sehemu inayofuata ya ndoto ya Farao baadaya kuamka na kurudi kulala. "Kisha nikaota tena"
Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.
Maneno "ya masuke" inaeleweka. "masuke saba"
"yakatoka katika bua moja". Shina ni sehemu ya mmea mnene na mrefu.
Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "yalinyauka, yamekaushwa, myembamba, na kukaushwa na jua kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"
"kuoza" au "nyauka"
Upepo unaotoka kutoka mashariki ulivuma kutoka jangwani. Joto la upepo wa mashariki mara kwa mara ulikuwa uharibifu kwa mazao.
"yakaota" au "kustawi"
Maneno "ya masuke" yanaeleweka. "masuke membamba"
"yakala". Farao anaota ya kwamba mahindi dhaifu yanaweza kumeza mahindi yenye afya kama mtu anavyokula chakula.
"hapakuwa na mtu mmoja ambaye" au "hakuna kati yao ambaye"
Inadokezwa ya kwamba maana zinafanana. "Ndoto zote mbili zina maana moja"
Yusufu anazungumza na Farao katika utatu. Kwa njia hii anaonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika upili wa mtu. "Mungu anakuonyesha kile atakachofanya hivi karibuni"
Maneno ya "masuke" yanaeleweka. "masuke saba mazuri"
Yusufu anaendelea tafsiri yake kwa ndoto za Farao.
"ng'ombe wembamba na dhaifu"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Masuke saba yaliyokaushwa na jua kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"
Yusufu anazungumzia kwa Farao katika utatu. Hii ni njia ya kuonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Matukio haya yatatokea kama nilivyokuambia ... imefunuliwa kwako, Farao"
"amefanya ijulikane"
hii inatumika kuweka msisitizo kile ambacho Yusufu anachosema baadae. "Vuta nadhari kwa kile nachosema"
Hii inazungumzia kuhusu miaka ya wingi kana kwamba muda ni kitu kinachosafiri na kufika mahali. "kutakuwa na miaka saba ambayo kutakuwa na chakula kingi katika nchi yote ya Misri"
Yusufu anaendelea tafsiri ya ndoto za Farao.
Hii inazungumzia kuhusu miaka saba ya njaa kana kwamba miaka ni kitu kinachosafiri na kufika mahali. "Kisha kutakuwa na miaka saba ambayo kutakuwa na chakula kichache"
Yusufu anaonyesha wazo kwa njia mbili kusisitiza umuhimu wake.
Hapa "nchi" ina maana ya watu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu wa Misri watasahau kuhusu miaka saba ambayo kulikuwa na chakula kingi"
Hapa "nchi" ina maana ya udongo, watu, na nchi nzima.
Hii inazungumzia kuhusu njaa kana kwamba ilikuwa kitu kinachosafiri na kufuata nyuma ya kitu kingine. "kwa sababu ya muda wa njaa utakaotokea hapo baadae"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu alikupatia ndoto mbili kukuonyesha ya kwamba hakika atasababisha mambo haya kutokea"
Yusufu anaendelea kuongea na Farao.
Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.
Yusufu anazungumza na Farao katika lugha ya utatu. Hii ni namna ya kuonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Wewe, Farao, unapaswa kutafuta"
Msemo "kumweka juu" una maana ya kumpatia mtu mamlaka. "kumpatia mamlaka juu ya ufalme wa Misri" au "kumpa usimamizi juu ya ufalme wa Misri"
Hapa "nchi" ina maana ya watu wote na kila kitu ndani ya Misri.
Neno "tano" ni sehemu. "Na wagawanishe nafaka ya Misri katika sehemu tano za kufanana, kisha wachukue moja ya sehemu hizo"
"katika miaka saba ambayo kutakuwa na wingi wa chakula"
Yusufu anaendelea kumshauri Farao.
"Waruhusu wageni kukusanya"
Hii inazungumzia miaka kana kwamba ni kitu kinachosafiri na kufikia mahali. "katika miaka mizuri ambayo hivi karibuni itatokea"
Msemo "chini ya mamlaka ya Farao" ina maana ya Farao kuwapa mamlaka. "tumia mamlaka ya Farao kutunza nafaka"
Hifadhi nafaka kwa muda wakati ambao kuna chakula kidogo. "Wasimamizi wanatakiwa kuwaacha walinzi pale kulinda nafaka"
Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Chakula hiki kitakuwa kwa ajili ya watu"
Hapa "nchi" ina maana ya watu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa njia hii watu hawatashinda njaa kipindi cha njaa"
Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Farao na watumishi wake walifikiri huu ulikuwa mpango mzuri"
Hii ina maana ya watumishi wa Farao.
"mtu kama vile Yusufu alivyomfafanua"
"ambaye Roho wa Mungu anaishi ndani mwake"
"hakuna mtu mwenye uwezo wa kufanya maamuzi"
Hapa "nyumba" ina maana ya kasri ya mfalme na watu ndani ya kasri. Msemo "utakuwa juu" una maana ya Yusufu kuwa na mamlaka juu ya. "Utakuwa na mamlaka juu ya kila mtu ndani ya kasri yangu"
Hapa "neno" lina maana ya amri au kilichosemwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utatawala juu ya watu wangu na wao watafanya kile unachoamuru"
Hapa "enzi" ina maana ya utawala wa Farao kama mfalme. "Katika nafasi yangu pekee kama mfalme"
Neno "Tazama" linaweka msisitizo kwa kile Farao anachosema baadae. "Tazama, nimekuweka"
Msemo "nimekuweka juu" una maana ya kutoa mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekuweka kuwa na mamlaka ya kila mtu ndani ya Misri"
Matendo haya yote yanaashiria ya kwamba Farao anampatia Yusufu mamlaka kufanya kila kitu ambacho Yusufu alipanga.
Pete hii ilikuwa na mhuri wa Mfalme uliochongwa juu yake. Hii ilimpatia Yusufu mamlaka na fedha iliyohitajika kutekeleza mipango yake.
"Kitani" ni kitambaa kilaini, kigumu kinachotengenezwa na mmea wa kitani.
Tendo hili linadhihirisha wazi kwa watu ya kwamba Yusufu ni wa pili tu kutoka kwa Farao.
"Inama chini na mheshimu Yusufu". Kupiga goti na kuinama chini ilikuwa ishara ya heshima na taadhima.
Msemo "kukuweka juu" una maana ya kumpatia mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekupa mamlaka juu ya kila mmoja ndani ya Misri"
Farao anasisitiza mamlaka yake. "Kama Farao, ninaamuru hivi mbali na wewe"
Hapa "nchi" na "mguu" zina maana ya matendo ya mtu. "hakuna mtu ndani ya Misri ataweza kufanya kitu chochote bila ruhusa yako" au "kila mtu ndani ya Misri lazima akuombe ruhusa kabla hajafanya jambo lolote"
Hapa "mtu" ina maana ya binadamu kwa ujumla, iwe wa kiume au wakike.
Jina la Zafenathi Panea kina maana ya "mfunuaji wa siri"
Makuhani wa Misri walikuwa tabaka la juu kabisa na upendeleo. Ndoa hii inaashiria nafasi ya Yusufu ya heshima na upendeleo.
"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Farao alimpatia Yusufu kuwa mke wake.
"Potifera" ni baba wa Asenathi.
Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.
Yusufu alisafiri katika nchi kusimamia maandalizi ya ujio wa ukame.
"umri wa miaka 30"
Hapa "aliposimama" ina maana ya Yusufu kuanza kumtumikia Farao. "alipoanza kumtumikia Farao"
Yusufu anakagua nchi anapoandaa kutekeleza mipango yake.
"Katika miaka mizuri saba"
"nchi ilizaa mavuno makubwa"
Hapa "Akakusanya" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwaamuru watumishi wake kukusanaya ... Wakaweka"
Hii inalinganisha nafaka na mchanga wa bahari kuweka msisitizo wa idadi yake kubwa. "Nafaka ambayo Yusufu alihifadhi ilikuwa nyingi kama mchanga wa baharini.
Hapa "Yusufu" na "akahifadhi" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwafanya watumishi wake wahifadhi ... wakaacha"
Hii inazungumzia kuhusu miaka saba kana kwamba ni kitu kinachosafiri na kuja kutulia mahali. "kabla ya miaka saba ya njaa kuanza"
"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Faro alimpatia Yusufu kama mke wake.
"Potifera" ni baba wa Asenathi.
Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.
"Jina la 'Manase' lina maana ya "kusababisha kusahau""
Hii ina maana ya baba wa Yusufu Yakobo na familia yake.
"Jina la 'Efraimu' lina maana ya 'kuwa na uzao' au 'kupata watoto'"
Hapa "uzao" ina maana ya kufanikiwa au kupata watoto.
Nomino inayojitegemea "mateso" inaweza kuwekwa kama "nimeteseka". "katika nchi hii ambayo nimeteseka".
Katika mataifa yanayozunguka mbele zaidi ya Misri, kujumuisha na nchi ya Kanaani.
Inasemekana ya kwamba kulikuwa na chakula kwa sababu Yusufu aliwaamuru watu wake kuhifadhi chakula katika kipindi cha miaka saba mizuri.
Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Ambapo Wamisri waliposhikwa na njaa"
Neno "uso" lina maana ya sehemu ya juu ya ardhi. "Njaa ilisambaa katika nchi yote"
Hapa "Yusufu" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwafanya watumishi wake kufungulia maghala yote na kuuza nafaka kwa Wamisri"
Hapa "dunia" ina maana ya watu kutoka maeneo yote. "Watu walikuwa wakija Misri kutoka maeneo yaliyozunguka"
"katika nchi yote". Inawezekana ya kwamba wafanyabiashara tofauti na mataifa ambayo yalikuwa sehemu ya njia za biashara na Misri yalioguswa na ukame walikuja Misri kwa ajili ya nafaka.