Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio jipya la simulizi.
Huyu ni mtu ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.
Huyu ni mtu ambaye alitengeneza chakula cha mfalme.
"walimkwaza bwana wao"
""mnyweshaji kiongozi na mwokaji kiongozi"
"Akawaweka katika gereza liliokuwa katika nyumba ambayo ilisimamiwa na kapteni wa walinzi"
Mflame hakuwaweka gerezani lakini aliwaamuru wafungwe. "Akafanya wawekwe" au "Aliamuru walinzi wake kuwaweka"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hili lilikuwa gereza lile lile ambalo Yusufu alikuwemo" au "Hili lilikuwa gereza lile lile ambalo Potifa alimweka Yusufu"
"Walikaa kifungoni kwa muda mrefu"
"Yusufu akaja kwa mnyweshaji na mwokaji"
Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yusufu alishangazwa na kile alichokiona. "Alishangazwa kuona ya kuwa walikuwa na huzuni"
Hii ina maana ya mnyweshaji na mwokaji"
"Gerezani katika nyumba ya bwana wake". "Bwana wake" ina maana ya bwana wa Yusufu, kapteni wa walinzi.
Yusufu anatumia swali kuonyesha msisitizo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "tafsiri ni za Mungu!" au "Ni Mungu ambaye anaweza kusema maana ya ndoto!"
Yusufu anawaomba wamumbie ndoto zao. "Tafadhali niambieni ndoto"
Mtu muhimu zaidi ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.
"Katika ndoto yangu, tazama, kulikuwa na mzabibu mbele yangu!" Mnyweshaji anatumia neno "tazama" hapa kuonyesha ya kwamba alishangazwa kwa kile alichokiona katika ndoto yake na kumuamsha Yusufu avute nadhari.
"vichala vyake vikaiva kuwa zabibu"
Hii ina maana ya kwamba alikamua juisi kutoka kwao. "akakamua juisi kutoka kwao"
"Hivi ndivyo ndoto inavyomaanisha"
"Matawi matatu yanawakilisha siku tatu"
"Katika siku tatu zaidi"
Hapa Yusufu anaongea na Farao kumuachia mnyweshaji kutoka gerezani kana kwamba Farao alisababisha yeye kuinua kichwa chake. "atakuachia kutoka gerezani"
"atakurudishia kazi yako"
Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. "kama ulivyofanya ulipokuwa"
"na tafadhali unioneshe wema kwangu"
Yusufu ana maana ya mnyweshaji kumwambia Farao juu yake ili kwamba Farao amfungulie kutoka gerezani. "Nisaidie kutoka katika gereza hili kwa kumwambia Farao juu yangu"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Maana hakika watu walinichukua" au "Maana hakika Waishmaeli walinichukua"
"nchi ambayo Waebrania huishi"
"na pia nilipokuwa hapa Misri, sijafanya jambo lolote ambalo nastahili kuwekwa gerezani"
Hii ina maana ya mtu kiongozi aliyetengeneza chakula cha mfalme.
"Mimi pia nilipata ndoto, na ndani ya ndoto yangu"
"kulikuwa na vikapu vitatu vya mikate juu ya kichwa changu!" Mwokaji anatumia neno "tazama" hapa kuonyesha ya kwamba alishangazwa kwa kile alichokiona ndani ya ndoto yake na kumuamsha Yusufu kuvuta nadhari.
"alioka vyakula kwa ajili ya Farao"
"Hii ndio maana ya ndoto"
"Vikapu vitatu vinawakilisha siku tatu"
Yusufu pia alitumia msemo huu "atainua kichwa chako" alipoongea kwa mnyweshaji katika 40:12. Hapa ina maana tofauti. Maana zaweza kuwa 1) "atainua kichwa chako na kuweka kamba katika shingo yako" au 2) "atainua kichwa chako kukikata"
Hapa "mwili" una maana ya sehemu laini katika mwili wa mtu.
"Hapo baadae, katika siku ya tatu". msemo "ikawa" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio jipya katika simulizi.
"Akawa na sherehe"
Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa na kuhudumia vinywaji kwa mfalme.
Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa chakula kwa ajili ya mfalme.
"majukumu" wa mkuu wa wanyweshaji una maana ya kazi yake kama mkuu wa manyweshaji. "Alimrudishia mkuu wa wanyweshaji kazi yake"
Farao hakumnyonga mwokaji yeye binafsi, ila aliaamuru anyongwe. "Lakini aliamuru mkuu wa waokaji anyongwe" au "Lakini aliamuru walinzi wake kumnyonga mkuu wa waokaji"
Hii ina maana ya pale ambapo Yusufu alitafsiri ndoto zao. "kama vile Yusufu alivyosema kingetokea pale alipotafsiri ndoto za wanamume wale wawili"