Kusafiri kwenda Misri inasemekana mara kwa mara kama "chini" tofauti na kwenda "juu" katika nchi ya ahadi. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Muishmaeli alimchukua Yusufu mpaka Misri"
Hii ina maana ya kwamba Yahwe alimsaidia Yusufu na alikuwa pamoja naye mara zote. "Yahwe alimuongoza Yusufu na kumsaidia"
Hapa mwandishi anazungumzia kufanya kazi ndani ya nyumba ya bwana wake kana kwamba alikuwa akiishi ndani ya nyumba ya bwana wake. Watumishi wanaoaminiwa pekee waliruhusiwa kufanya kazi ndani ya nyumba ya bwana wao. "alifanya kazi ndani ya nyumba".
Yusufu sasa alikuwa mtumwa wa Potifa.
Hii ina maana ya kwamba bwana wake aliona jinsi Yahwe alivyokuwa akimsaidia Yusufu. "Bwana wake aliona ya kwamba Yahwe alikuwa akimsaidia Yusufu"
"Yahwe alisababisha kila kitu alichofanya Yusufu kufanikiwa"
"Kupata kibali" ina maana ya kukubalika na mtu. Nomino ya "machoni pake" ina maana ya maoni ya mtu. Maana zaweza kuwa 1) "Potifa alifurahishwa na Yusufu" au 2) "Yahwe alifurahishwa na Yusufu"
Hii ina maana ya kwamba alikuwa mtumishi wa binafsi wa Potifa.
"Potifa alimweka Yusufu kusimamia nyumba yake na kila kitu kilichokuwa cha Potifa"
Pale ambapo kitu "kinakuwa chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu anawajibika na utunzanji na uhifadhi wake. "alimfanya Yusufu kutunza"
Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
"Potifa alimweka Yusufu kuwa msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki"
Hapa "baraka" ina maana ya kusababisha mema na yenye manufaa kutokea kwa mtu au kitu kinachobarikiwa.
Hapa mwandishi anazungumzia baraka ambayo Yahwe alitoa kana kwamba ilikuwa mfuniko wa kihalisia uliofunika kitu. "Yahwe alibariki"
Hii ina maana ya nyumba na nafaka na mifugo yake. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Nyumba ya Potifa na nafaka na mifugo yake yote"
Kitu kinachokuwa "chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu huyo anawajibika kutunza na kulinda. "Kwa hiyo Potifa alimweka Yusufu kuwa mwangalizi wa kila kitu ambacho alikuwa nacho"
Hakuhitaji kuwaza juu ya jambo lolote katika nyumba yake; alipaswa kufanya maamuzi juu ya kile alichotaka kula. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "Potifa alitakiwa kuwaza kuhusu kile alichotaka kula tu. Hakuhitaji kuwaza juu ya kitu kingine ndani ya nyumba yake"
Neno "basi" linaweka alama ya pumziko katika simulizi ambapo mwandishi anatoa taarifa ya nyuma kuhusu Yusufu.
Maneno haya mawili yana maana moja. Yanalenga uzuri wa muenekano wa Yusufu. Yawezekana alikuwa mwenye sura nzuri na mwenye nguvu. "mwenye sura nzuri na nguvu"
"Na kwa hiyo". Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio jipya katika simulizi.
"Sikia". Yusufu anatumia neno hili kuvuta nadhari ya mke wa Potifa.
"bwana wangu hajishughulishi juu ya nyumba yake napokuwa msimamizi." Hii inaweza kuandikwa katika hali ya chanya. "bwana wangu ananiamini na nyumba yake"
Kitu kinachokuwa "chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu huyo anawajibika kutunza na kulinda. "Kwa hiyo Potifa alimweka Yusufu kuwa mwangalizi wa kila kitu ambacho alikuwa nacho"
Hapa mwandishi anazungumzia juu ya mamlaka kana kwamba yalikuwa ukubwa. "Nina mamlaka katika nyumba hii kuliko mtu yeyote yule"
Hii inaweza kusemwa katika hali ya chanya. "Amenipatia kila kitu isipokuwa wewe"
Yusufu anatumia swali kuonyesha msisitizo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Hakika siwezi kufanya jambo hili ovu na kutedna dhambi dhidi ya Mungu"
Hii ina maana ya kwamba aliendelea kumuuliza kulala naye. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Aliendelea kumuuliza Yusufu alale naye"
"kuwa karibu naye"
"Na kwa hiyo". Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya sehemu mpya ya tukio katika simulizi.
"hakuna mwanamume yeyote aliyefanya katika nyumba"
"na akakimbia nje haraka" au "na kwa haraka akakimbia nje ya nyumba"
"Kisha ... akawaita." Msemo "ikawa kwamba" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio lifuatalo katika simulizi.
"na kwa haraka alikimbia nje ya nyumba"
"wanamume waliofanya kazi katika nyumba yake"
"Sikiliza". Mke wa Potifa anatumia neno hili kuvuta nadhari ya watumishi wake.
Hapa mke wa Potifa anamtuhumu Yusufu kwa kujaribu kumkamata na kulala naye.
"Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha". Msemo "ikawa kwamba" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio lifuatalo la simulizi.
"Bwana wa Yusufu." Hii ina maana ya Potifa.
"Alielezea namna hii"
Neno hili "kwetu" ina maana ya Potifa, mke wake, na inamaanisha nyumba yake yote.
"alikuja ndani kunifanya mpumbavu". Hapa neno "dhihaki" ni tafisida ya "kumkamata na kulala naye". "alikuja nilipokuwepo na akajaribu kunilazimisha nilale naye"
"Kisha". Mke wa Potifa anatumiamsemo huu kuweka alama ya tukio linalofuata katika habari anayomwambia kuhusu Yusufu kujaribu kulala naye.
"alikimbia haraka nje ya nyumba"
"Na kwa hiyo". Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio jipya katika simulizi.
"Bwana wake Yusufu". Hii ina maana ya Potifa. Taarifa hii inaweza kuwekwa wazi. "Bwana wake Yusufu, Potifa"
"alimsikiliza mke wake akimuelezea kwake". Neno "wake" na "kwake" hapa yana maana ya Potifa.
"Potifa akawa na hasira sana"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mahali ambapo mfalme huweka wafungwa wake"
"Yusufu alikaa pale"
Hii ina maana ya namna Yahwe alivyomtunza Yusufu na kuwa mema kwake. "Lakini Yahwe alikuwa mwema kwa Yusufu" au "Lakini Yahwe alimtunza Yusufu"
Hii ina maana Yahwe alisababisha mlinzi wa gereza kumkubali Yusufu na kumtendea wema. "Yahwe alisababisha mlinzi wa gereza kufurahishwa na Yusufu"
"msimamizi wa gereza" au "mtu mwenye usamamizi na gereza"
Hapa "mkononi" unawakilisha nguvu ya Yusufu au uaminifu. "kumweka Yusufu juu ya"
"Yusufu alikuwa mwanaglizi wa kila kitu walichofanya pale"
Hii ina maana ya jinsi Yahwe alivyomsaidia Yusufu na kumuongoza. "kwa sababu Yahwe alimuongoza Yusufu"
"Yahwe alisababisha kila kitu ambacho Yusufu alifanya kufanikiwa"