"katika nchi ya Kaanani ambapo baba yake aliishi"
Sentensi hii inatambulisha habari ya watoto wa Yakobo katika Mwanzo 37:1-50:26. Hapa "Yakobo" ina maana ya familia yake nzima. "Hii ni habari ya familia ya Yakobo"
"umri wa miak 17"
Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.
Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.
"suria". Wanawake hawa walikuwa watumishi wa Lea na Raheli waliopewa kwa Yakobo kumzalia watoto.
"taarifa mbaya kuhusu kaka zake"
Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Israeli na Yusufu.
Hii ina maana ya upendo wa kindugu au upendo wa kirafiki au kifamilia. Huu ni upendo wa kawaida wa binadamu kati ya marafiki na ndugu.
Hii ina maana ya kwamba Yusufu alizaliwa wakati Israeli alikuwa mzee. "aliyezaliwa wakati Israeli alipokuwa mtu mzee"
"Israeli alimshonea Yusufu"
"joho zuri"
"hawakuweza kuongea kwa namna ya upole kwake"
Huu ni ufupi wa matukio ambayo yatatokea katika 37:6-11.
"Na kaka zake Yusufu walimchukia zaidi ya walivyomchukia hapo awali"
"Tafadhali sikilizeni ndoto hii niliyoipata"
Yusufu anaeleza kaka zake kuhusu ndoto yake.
Neno la "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa ya kushangaza inayofuata.
Neo "tulikuwa" ina maana ya Yusufu na inajumuisha kaka zake wote.
Nafaka inapovunwa inafungwa katika makundi na kupangwa katika rundo hadi muda wa kuzitenga nafaka kutoka kwa majani makavu.
Hapa neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yusufu alishangazwa na kile alichokiona.
Hapa miganda ya nafaka inasimama wima na kupiga magoti kana kwamba ilikuwa watu. Miganda hii inawakilisha Yusufu na kaka zake.
Misemo hii miwili ina maana moja. Kaka zake Yusufu wanatumia swali kumkejeli Yusufu. Inaweza kuandikwa kama kauli. "Hutaweza kuwa mfalme wetu, na hatutainama chini kwako!"
Neno la "yetu" lina maana ya kaka zake Yusufu lakini sio Yusufu.
"kwa sababu ya ndoto yake na kile alichokisema"
"Yusufu akapata ndoto nyingine"
"nyota 11"
"Israeli alimkaripia, akisema"
Israeli anatumia swali kumrekebisha Yusufu. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Ndoto hii uliyoota sio ya kweli. Mama yako, kaka zako, na mimi hatutainama chini mbele yako!"
Hii ina maana kuwa na hasira kwa sababu mtu mwingine amefanikiwa au ana umaarufu zaidi.
Hii ina maana ya kwamba aliendelea kufikiria kuhusu maana ya ndoto ya Yusufu. "aliendelea kufikiria kuhusu maana ya ndoto ile"
Israeli anatumia swali kuanza mazungumzo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Ndugu zako wanachunga kundi huko Shekemu".
Hapa inasemekana ya kwamba Israeli anamuomba Yusufu kujiandaa kuondoka kuonana na ndugu zake. "Jiandae"
Yupo tayari kuondoka. "Nipo tayari kuondoka"
"Israeli akamwambia Yusufu"
Israeli anamtaka Yusufu kurudi na kumuambia kuhusu kaka zake na hali ya mifugo. "njoo uniambie utakakikuta" au "niletee taarifa"
"kutoka bondeni"
"Mtu mmoja akamkuta Yusufu akizunguka kondeni"
Hii inaweka alama mwanzo wa tukio jingine katika simulizi kuu. Inaweza kuhusisha watu tofauti kuliko matukio ya nyuma.
"Ni nini unatafuta"
"Tafadhali niambie wapi"
"wakichunga kundi"
Hili ni jina la mahali ambalo lipo kama kilomita 22 kutoka Shekemu.
"Ndugu zake Yusufu wakamwona alipokuwa bado yupo mbali"
"wakafanya njama ya kumuua"
"anakuja yule mwenye ndoto zile"
Msemo huu unaonyesha ya kwamba kaka zake walitekeleza mipango yao. "Kwa hiyo sasa"
"mnyama wa hatari" au "mnyama mkali"
amemla kwa hamu
Ndugu zake walipanga kumuua, kwa hiyo ni kejeli kuzungumzia kuhusu ndoto zake kuwa kweli, maana angekuwa amekwisha kufa. "Kwa njia hiyo tutahakikisha ndoto zake haziji kuwa kweli"
"alisikia walichokuwa wakisema"
Msemo "mikono yao" una maana ya mipango ya kaka zake ya kumuua. "kutoka kwao" au "kutoka kwa mipango yao"
Msemo wa "kuondoa uhai wake" ni tasifida kwa kumuua mtu. "Tusimuue Yusufu"
Ukanushaji unaweza kuwekwa juu ya kitenzi. Pia "kumwaga damu" ni tasifida ya kuua mtu. "Usimwage damu yoyote" au "Usimuue"
Hii ina maana ya kumdhuru au kumjeruhi. "msimdhuru"
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Rubeni alisema hivi ili aweze kumuokoa Yusufu"
Msemo wa "mikononi mwao" una maana ya mpango wa kaka zake kumuua. "kutoka kwao" au "kutoka kwa mipango yao"
"na kumrudisha"
Msemo huu unatumika hapa kuweka alama juu ya tukio muhimu la simulizi.
"walichana joho lake zuri kutoka kwake"
"joho zuri"
"Mkate" ni lugha nyingine kwa "chakula". "Walikaa chini kula chakula" au "Ndugu zake Yusufu walikaa chini kula"
Hapa kuangalia juu inazungumziwa kana kwamba mtu aliinua macho yake juu kihalisia. Pia, neno "tazama" linatumika hapa kuvuta nadhari ya msomaji kwa kile walichokiona wanamume hawa. "Walitazama juu na ghafla wakaona msafara"
"umebeba"
vikolezo
kitu chenye mafuta chenye harufu tamu kinachotumiwa kwa ajili ya kuponya na kulinda ngozi. "dawa"
"kuwaleta mpaka Misri". Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "kuwaleta chini hadi Misiri kuviuza"
Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Hatupati faida yoyote kumuua ndugu yetu na kufunika damu yake"
Huu ni msemo wenye maana ya kuficha kifo cha Yusufu. "kuficha mauaji yake"
"kwa wanamume hawa ambao ni vizazi vya Ishmaeli"
Hii ina maana ya kutomdhuru au kumjeruhi. "msimuumize"
Neno la "nyama" ni lugha nyingine lenye maana ya ndugu. "ni ndugu wetu wa damu"
"Kaka zake na Yuda walimsikiliza" au "Kaka zake Yuda walikubaliana naye"
Majina yote mawili yana maana ya kundi moja la wafanyabiashara ambao ndugu zake Yusufu walikutana nao.
"kwa bei ya vipande 20 vya fedha"
"wakampeleka Yusufu Misri"
"Rubeni alirudi kwenye shimo, na akashangazwa kuona ya kwamba Yusufu hakuwepo mle" Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Rubeni alishangazwa kukuta ya kwamba Yusufu aliondoka.
Hili ni tendo la mawazo na uchungu mkubwa. Hii inaweza kuandikwa kwa uwazi zaidi. "Alikuwa na majonzi mpaka akararua nguo zake"
Rubeni anatumia maswali kuweka msisitizo kwa tatizo ambalo Yusufu hapatikani. Hivi vinaweza kuandikwa kama kauli. "Kijana ametoweka! Siwezi kurudi nyumbani sasa!"
Hii ina maana ya joho zuri ambalo baba yake alimtengenezea.
"damu ya mbuzi"
"walileta joho lile"
"amemla"
Yakobo anadhani ya kwamba mnyama pori amerarua mwili wa Yusufu vipande vipande. "hakika imemchana Yusufu katika vipande vipande"
Hili ni tendo la mawazo na uchungu mkubwa. Hii inaweza kuandikwa kwa uwazi zaidi. "Yakobo alikuwa na majonzi mpaka akararua nguo zake"
Hapa "viuno" ina maana ya sehemu ya katikati ya mwili au kiuno. "akavaa magunia"
Hapa ujio wa watoto kwa baba yao inazungumziwa kama "kuinuka juu". "wakaja kwake"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "lakini hakutaka wamfariji"
Hii ina maana ataomboleza kutoka sasa hadi pale atakapokufa. "Kweli nitakapokufa na kwenda kuzimu bado nitakuwa naomboleza"
"Wamidiani walimuuza Yusufu"
"kiongozi wa wanajeshi waliokuwa wakimlinda mfalme"