Msemo "panda" unatumika kwa sababu Betheli ipo sehemu ya juu kuliko Shekemu.
Mungu anaongea kuhusu yeye mwenyewe katika lugha ya utatu. "Jenga madhabahu pale kwangu, Mungu wako"
"akwaambia familia yake"
"Tupa mbali sanamu zenu" au "Zitokomeze miungu yenu ya uongo"
Hii ilikuwa utamaduni wa kujitakasa kimaadili na kimwili kabla ya kwenda kumuabudu Mungu.
Kuvaa mavazi mapya ilikuwa ishara ya kwamba walijifanya safi kabla ya kumkaribia Mungu.
Maana za "siku" zaweza kuwa 1) siku ambayo Yakobo alimtoroka Esau au 2) "siku" ina maana ya kipindi ambacho Yakobo alikuwa na mawazo. "nilipokuwa katika kipindi kigumu" au "nilipokuwa katika shida"
"kwa hiyo kila mmoja katika nyumba ya Yakobo akatoa" au "kwa hiyo kila mtu katika familia na watumishi walitoa"
Hapa "mikononi mwao" ina maana ya kile walichomiliki. "kilichokuwa mali yao" au "walivyokua navyo"
"heleni zao". Maana zaweza kuwa 1) dhahabu katika heleni zingeweza kutumika sanamu zingine au 2) walichukua heleni hizi kutoka kwenye mji wa Shekemu baada ya kuishambulia na kuwaua watu wote. Heleni zingewakumbusha juu ya dhambi yao.
Mungu kusababisha watu wa miji kumuogopa Yakobo na familia yake inazungumziwa kana kwamba "hofu" ilikuwa kitu kilichoanguka juu ya miji. Nomino inayojitegemea "hofu" inaweza kuwekwa kama "kuogopa". "Mungu aliwafanya watu waliozunguka miji kumuogopa Yakobo na wote aliokuwa nao"
Hapa "miji" ina maana ya watu wanaoishi katika miji.
Inasemekana ya kwamba hakuna mtu aliyeshambulia familia ya Yakobo. Lakini wana wawili, Simoni na Lawi walishambulia ndugu wa Wakaanani wa Shekemu baada ya kumkamata na kulala na binti wa Yakobo. Yakobo aliogopa wangelipiza kisasi katika 34:30. "Familia ya Yakobo" au "Nyumba ya Yakobo"
Hili ni jina la mji.
"Jina la El Betheli lina maana ya "Mungu wa Betheli"
"pale Mungu alijifunua kwa Yakobo"
Hili ni jina la mwanamke.
Mlezi ni mwanamke ambaye humtunza mtoto wa mwanamke mwingine. Mlezi aliheshimika na alikuwa muhimu sana kwa familia.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walimzika chini kutoka Betheli"
Msemo "chini kutoka" unatumika kwa sababu walimzika katika eneo ambalo lilikuwa chini kwa mwinuko kuliko Betheli.
"Jina la Aloni Bakuthi lina maana ya "Mwaloni ambapo kuna maombolezo"
Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba walikuwa Betheli. "Baada ya Yakobo kuondoka Padani Aramu, na wakati alipokuwa Betheli"
Hapa "kubariki" ina maana ya kutamka baraka maalumu juu ya mtu na kusababisha mambo mazuri kutokea juu ya mtu huyo.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena"
"Mungu akamwambia Yakobo"
Mungu akamwambia Yakobo kuzaa watoto ili kwamba waweze kuwa wengi wao. Neno "kuongezeka" unaelezea jinsi anavyotakiwa "kuzaa".
Hapa "taifa" na "mataifa" yana maana ya vizazi vya Yakobo ambao wataunda mataifa haya.
Hapa "akapanda kutoka" inatumika kwa sababu Mungu anapoishi inafikiriwa kuwa juu au juu ya dunia. "Mungu akamuacha"
Hii ni nguzo ya ukumbusho ambayo ilikuwa jiwe au jabali kubwa iliyowekwa mwishoni pake.
Hii ni ishara ya kwamba anaweka wakfu nguzo kwa Mungu.
"Jina la Betheli lina maana ya "nyumba ya Mungu".
Hili ni jina lingine la mji wa Bethelehemu.
"Alikuwa na wakati mgumu wakati alipokuwa akimzaa mtoto"
"Uchungu ulipokuwa katika hatua mbaya zaidi"
mtu anayemsaidia mwanamke anapojifungua mtoto
"pumzi yake ya mwisho" ni pumzi ya mwisho ya mtu kabla mtu hajafa. "Hata kabla hajafa, alipovuta pumzi yake ya mwisho"
"Jina la Benoni lina maana ya "mtoto wa majonzi yangu""
Watafsiri wanaweza kuweka maandishi mafupi yasemayo "Jina la Benyamini lina maana ya "mtoto wa mkono wa kuume". Msemo wa "mkono wa kulia" unalenga sehemu yenye upendeleo maalumu.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na wakamzika"
"pembeni mwa barabara"
"inaweka alama juu ya kaburi la Raheli mpaka siku hii"
"mpaka wakati huu wa leo." Hii ina maana hadi wakati ambapo mwandishi alikuwa akiandika haya.
Inasemekana ya kwamba familia ya Israeli na watumishi wake wako pamoja naye. Maana kamili ya taarifa hii inaweza kuwekwa wazi.
Hii ni jina la mtumishi wa Raheli wa kike.
Sentensi hii inaanza ibara mpya, ambayo inaendeleza mistari inayofuata.
"watoto 12"
Hili ni jina la mtumishi wa Raheli wa kike.
Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.
Inasemekana ya kwamba hii haimjumlishi Benyamini aliyezaliwa katika nchi ya Kaanani karibu na Bethelehemu. Inataja Padani Aramu tu kwa maana hapo ndipo wengi wao walizaliwa. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi. "ambao walizaliwa kwake Padani Aramu, isipokuwa Benyamini ambaye alizaliwa katika nchi ya Kaanani"
Hapa "akaja" inaweza kuweka kama "akaondoka"
Hili lilikuwa jina lingine la mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale. Hii ilikuwa jina la mwanamume aliyemiliki miti ya mwaloni.
Hili ni jina la mji.
"miaka 180"
"Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa". Misemo ya "alivuta pumzi ya mwisho" na "akafa" ina maana ya kitu kimoja. "Abrahamu alikufa"
Hii ni njia ya upole ya kusema mtu alikufa.
Hii ina maana ya kwamba baada ya Isaka kufa, roho yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alijiunga na familia yake waliokuwa wamekufa"
Misemo ya "mtu mzee" na "amejaa siku" zina maan moja. Zinasisitiza ya kwamba Isaka aliishi muda mrefu sana. "baada ya kuishi muda mrefu sana na kuzeeka sana"