Hapa neno hili linatumika kuweka alama kwa sehemu mpya ya simulizi.
Hili ni jina la binti wa Lea.
Hili li jina la kundi la watu.
Hii ina maana ya Hamori na sio Shekemu. Pia "mwana wa mfalme" hapa haimaanishi mtoto wa mfalme. Ina maana ya Hamori alikuwa kiongozi wa watu katika eneo hilo.
Shekemu alimbaka Dina.
"Alivutiwa sana na yeye". Hii inazungumzia juu ya Shekemu kumpenda Dina na kutaka kuwa naye kana kwamba kuna jambo lililokuwa likimlazimisha kwenda kwa Dina. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Alitaka sana kuwa na Dina"
Hii ina maana aliongea naye kwa upole kumuaminisha ya kwamba alimpenda na kwamba alimtaka pia ampende yeye.
"basi" inatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Yakobo.
Neno "alikuwa" lina maana ya Shekemu
Hii ina maana ya kwamba Shekemu alivunja sana heshima na kumuabisha Dina kwa kumlazimisha alale naye.
Hii ni namna ya kusema ya kwamba Yakobo hakusema au kufanya jambo kuhusu suala hili.
"Hamori ... akaenda kuongea na Yakobo"
"Wanamume walikasirika"
Hii inaweza kuwekwa kama nukuu ya moja kwa moja iliyozungumzwa na wana wa Yakobo.
Hapa neno la "Israeli" lina maana ya kila mtu katika familia ya Yakobo. Israeli kama kundi la watu liliabishwa."ameabisha familia ya Israeli" au "ameleta aibu juu ya watu wa Israeli"
"kumvamia binti wa Yakobo"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa maana hakupaswa kufanya jambo baya kama hilo"
"Hamori alizungumza na Yakobo na wanawe"
Hapa neno "anampenda" lina maana ya upendo wa kimahaba kati ya mwanamume na mwanamke. "anampenda na anataka kumuoa"
Katika baadhi ya tamaduni, wazazi huamua watoto wao wataolewa na nani"
Kuoana ni kuoa mtu wa jamii, kabila, au dini tofauti. "Ruhusu ndoa kati ya watu wako na wetu"
"nchi itakuwa wazi kwako"
"Shekemu alimwambia baba yake Dina Yakobo"
Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Kama utanipa kibali, basi nitakupa chochote utakachokiomba"
Katika baadhi ya tamaduni, ni kawaida kwa mwanamume kutoa fedha, mali, ng'ombe, na zawadi zingine kwa familia ya mwanamke katika kipindi cha ndoa.
Nomino inayojitegemea ya "hila" inaweza kuwekwa kama kitenzi cha "kudanganya". "Lakini wana wa Yakobo walimdanganya Shekemu na Hamori walipowajibu"
Hii ina maana ya kwamba Shekemu aliwavunjia heshima sana na kumuabisha Dina kwa kumlazimisha kulala naye.
"wana wa Yakobo waliwaambia Shekemu na Hamori"
"Hatuwezi kukubali kumtoa Dina katika ndoa"
"kwa maana hiyo itasababisha aibu kwetu". Hapa "kwetu" ina maana ya wana wa Yakobo na watu wote wa Israeli.
Hii ina maana wataruhusu mtu kutoka familia ya Yakobo kuoa mtu anayeishi katika nchi ya Hamori.
Hapa "maneno" ina maana ya kile kilichosemwa. "Hamori na mwanawe Shekemu walikubali na kile ambacho wana wa Yakobo walisema"
"kufanyiwa tohara"
"binti wa Yakobo Dina"
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba Shekemu alijua wanamume wengine wangekubali kufanyiwa tohara kwa sababu walimheshimu sana. "Shekemu alijua wanamume wote katika nyumba ya baba yake watakubaliana naye kwa sababu alikuwa akiheshimiwa zaidi kati yao"
Ilikuwa kawaida kwa viongozi kukutana katika lango la mji kufanya maamuzi rasmi.
"Yakobo, wanawe, na watu wa Israeli"
Hapa "nasi" inajumlisha Hamori, mwanawe na watu wote waliozungumza nao langoni mwa mji.
"waruhusu waishi na kufanya biashara katika nchi"
Shekemu anatumia neno "kweli" kuongeza msisitizo kwa kauli yake. "kwa sababu, hakika, nchi ni kubwa ya kutosha kwa ajili yao" au "kwa sababu, haswa, kuna nchi ya kutosha kwa ajili yao"
Hii ina maana ya ndoa kati ya wanawake wa kundi moja na wanamume wa kundi lingine.
Hamori na Shekemu mwanawe wanaendelea kuzungumza na viongozi wa mji.
"Kwa sharti hili pekee iwapo kila mwanamume kati yetu atafanyiwa tohara, kama wanamume wa Israeli walivyotahiriwa, ndipo watakubali kusihi miongoni mwetu na kujiunga nasi kama kundi moja"
Shekemu anatumia swali kusisitiza ya kwamba mifugo wa Yakobo na mali zitakuwa za watu wa Shekemu. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Wanyama wao wote na mali zitakuwa zetu"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa hiyo Hamori na Shekemu wakawa na mtu wa kufanya tohara kwa wanamume wote"
"tatu" ni nambari za mpango kwa namba tatu. Inaweza kuwekwa bila nambari za mpango. "Baada ya siku mbili"
"wakati wanamume wa mji walipokuwa bado na maumivu"
"wakachukua panga zao"
Hapa "mji" una maana ya watu. "waliwashambulia watu wa mji"
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "ulinzi. Simoni na Lawi waliwaua wanamume wote wa mji ule"
Hapa "makali" yana maana ya ubapa wa upanga. "kwa ubapa wa panga zao" au "kwa upanga wao"
"maiti ya Hamori, Shekemu na wanamume wao"
"waliiba kila kitu chenye thamani katika mji ule"
Shekemu pekee alimnajisi Dina, lakini wana wa Yakobo walichukulia familia yote ya Shekemu na kila mtu katika mji kuhusika na tendo hili.
Hii ina maana ya kwamba Shekemu alimvunjia heshima na kumuabisha sana Dina kwa kumlazimisha kulala naye.
"wana wa Yakobo wakachukua mifugo ya watu wale"
"mali zao zote na fedha"
"Waliwakamata watoto wao na wake zao wote"
Kusababisha mtu kupitia shida inazungumziwa kana kwamba shida ilikuwa kitu kinacholetwa na kuwekwa juu ya mtu. "mmesababisha shida kubwa kwangu"
Kusababisha watu katika maeneo yanayozunguka kumchukia Yakobo inazungumziwa kana kwamba wana wa Yakobo walimfanya anuke vibaya kihalisia. Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Mmenifanya nionekane kwa kinyaa kwa watu wanaoishi katika nchi"
Hapa maneno "Mimi" na "yangu" yana maana ya nyumba yote ya Yakobo. Yakobo anasema "Mimi" au "yangu" kwa maana yeye ni kiongozi. "Nyumba yangu ni ndogo ... dhidi yetu na kutuvamia, kisha watatuangamiza sisi wote"
"wataunda jeshi na kunishambulia" au "wataunda jeshi na kutushambulia"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wataniangamiza" au "watatuangamiza"
Simoni na Lawi wanatumia swali kusisitiza ya kwamba Shekemu alifanya kosa na alistahili kufa. "Shekemu hakupaswa kumtenda dada yetu kama kahaba!"