Hii inazungumzia kuhusu kuwa karibu na kupofuka kana kwamba macho yalikuwa taa na mwanga ulikuwa ukitoweka. "alikaribia kupofuka" au "kidogo apofuke"
"Na Esau akajibu"
"Nipo hapa" au "Ninasikiliza'
"Kisha Isaka akasema"
Msemo wa "tazama hapa" unaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata. "Sikiliza kwa makini"
Inasemekana Isaka anajua atakufa hivi karibuni. "Naweza kufa siku yoyote toka sasa"
Hii ina maana ya kifo cha mwili.
Isaka anaendelea kutoa maelekezo kwa mwanae mkubwa Esau.
"vifaa vyako vya kuwindia"
Podo ni kasha la kushikilia mishale. "podo lako la mishale"
"winda mnyama pori kwa ajili yangu"
Neno "kitamu" lina maana ya kitu chenye ladha nzuri sana. "Nipikie nyama tamu ninayoipenda"
Kipindi cha Biblie, baba mara nyingi hutamka baraka juu ya watoto wake.
Neno "basi" linaonyesha badiliko la msisitizo kwa Rebeka na Yakobo.
"Rebeka alimsikia Isaka akizungumza na mwanawe Esau"
Neno "kwa hiyo" inaweza kuongezwa kuonyesha ya kwamba Rebeka anazungumza na Yakobo kwa sababu ya kile alichosikia, na anaongea naye wakati Esau ameondoka. "Kwa hiyo Esau alipokuwa ameondoka ...kuja nayo"
Esau na Yakobo walikuwa wote wawili watoto wa Isaka na Rebeka. Wanaitwa "mtoto wake" na "mwanawe" kusisitiza ya kwamba mzazi mmoja alimpendelea mtoto mmoja juu ya mtoto mwingine.
Msemo "tazama hapa" unaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata. "Sikiliza kwa makini"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika hali isiyo moja kwa moja. Alimwambia Esau "kuwinda mnyama pori, na kumtengenezea nyama tamu anayoipenda". Kisha kabla hajafa, Isaka atambariki Esau mbele ya Yahwe.
"Niletee mnyama pori utakayemwinda na kumuua"
"nipikie nyama tamu ninayoipenda"
"kukubariki mbele ya Yahwe"
"kabla sijafa"
Rebeka anaendelea kuzungumza kwa mtoto wake mdogo Yakobo.
Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.
Rebeka alisema "sauti yangu" kumaanisha kile alichokuwa akisema. "unitii na ufanye kile nachokuambia"
Neno "kitamu" ina maana ya kitu chenye ladha nzuri sana.
"Kisha peleka kwa baba yako"
"na atakapokila, atakubariki"
Neno "kubariki" lina maana ya baraka maalumu ambayo baba hutamka kwa watoto wake.
"kabla hajafa"
"Mimi ni mwanamume mwenye ngozi laini" au "Mimi sina manyoya"
"na atafikiri ya kwamba mimi ni muongo" au "atajua ya kwamba ninamdanganya"
Kulaaniwa au kubarikiwa inazungumziwa kana kwamba laana na baraka ni vitu vinavyowekwa juu ya mtu. "Kisha kwa sababu ya hili, atanilaani na hatanibariki"
"acha laana yako na iwe juu yangu, mwanangu". Kulaaniwa inazungumziwa kana kwamba laana ni kitu kinachowekwa juu ya mtu. "acha baba yako anilaani badala yako, mwanangu"
Rebeka akasema "sauti yangu" kumaanisha kile alichokuwa akizungumza. "utii kile ninachokuambia" au "unitii"
"niletee mwanambuzi mchanga"
Neno la "kitamu" lina maana ya kitu chenye ladha nzuri sana.
Ngozi ya mbuzi ilikuwa bado ina manyoya juu yao.
"Alimpatia mtoto wake Yakobo chakula kitamy na mkate aliokuwa ameandaa"
"Na baba yake akajibu" au "Isaka akajibu"
"ndio, nasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"
"Nimefanya kile ulichonimbia kufanya"
Neno "windo" lina maana ya wanyama pori ambayo mtu huwinda na kuua.
"Yakobo alijibu"
Hii ni lahaja yenye maana ya kwamba Mungu alisababisha itokee. "alinisaidia kufanikiwa nilipokuwa nawinda"
"kama kweli wewe ni mwanangu Esau"
"Yakobo alimkaribia Isaka baba yake"
Isaka anafananisha sauti ya Yakobo na Yakobo mwenyewe. "Unasikika kama Yakobo"
Isaka analinganisha mikono ya Esau kwa Esau mwenyewe. "lakini mikono yako inaonekana kama mikono ya Esau"
Isaka anauliza swali hili kabla hajambariki mwanawe. "Lakini kwanza Isaka alimuuliza Isaka"
Neno "windo" lina maana ya mnyama pori ambaye watu huwinda na kuua.
"na Isaka akainywa"
Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba nguo zilinuka kama nguo za Esau. "alinusa nguo zake na zilinuka kama nguo za Esau, kwa hiyo Isaka akambariki"
"na Isaka akanusa"
"marashi"
"na kisha akambariki". Hii ina maana ya baraka maalumu ambayo baba hutamka kwa watoto wake.
Neno "tazama" linatumika kama msemo wa mkazo kumaanisha "ni kweli". Hakika, harufu ya mwanangu"
Hapa neno "alilolibariki" lina maana ya Yahwe alisababisha mambo mazuri kutokea kwenye shamba na ikawa na matunda. "ambayo Yahwe amesababisha kuzaa sana"
Hii ni baraka ya Isaka. Alifikiri alikuwa akizungumza na Esau, lakini alikuwa akizungumza na Yakobo.
Hapa "akupe" ni katika hali ya umoja na ina maana ya Yakobo. Lakini baraka ingeweza kuhusika kwa vizazi vya Yakobo.
"umande" ni matone ya maji yanayounda juu ya mimea wakati wa usiku. Hii inaweza kuwekwa wazi. "umande wa usiku kutoka mbinguni kumwagilia mimea yako"
Kuwa na nchi yenye mbolea inazungumziwa kana kwamba nchi ilikuwa nene au tajiri. "udongo mzuri kwa ajili ya kuzaa mimea"
Kama "nafaka" na "mvinyo" havijulikani, vinaweza kuwekwa kwa ujumla zaidi. "chakula na kinywaji kingi"
Hapa hivi viwakilishi vipo katika umoja na vina maana ya Yakobo. Lakini baraka pia inalenga vizazi vya Yakobo.
Hapa "mataifa" ina maana ya watu. "watu kutoka mataifa yote yainame"
Hii ina maana ya kuinama na kutoa heshima na taadhima ya unyenyekevu kwa mtu.
"Kuwa bwana juu ya ndugu zako"
Isaka anazungumzia baraka hii moja kwa moja kwa Yakobo. Lakini, inahusika kwa vizazvi vya Yakobo ambao watatawala vizazi vya Esau na vizazi vya ndugu yeyote wa Yakobo ambaye anaweza kuwa naye.
"na wana wa mama yako watakusujudu"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Mungu alaani kila mtu anayekulaani"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Mungu abariki kila mtu anayekubariki"
"ameondoka tu katika hema la Isaka baba yake"
"nyama tamu nayoipenda"
Hapa "ya mwanao" ilikuwa njia ya upole ya Esau kumaanisha chakula chake mwenyewe alichokiandaa.
Neno "windo" lina maana ya wanyama pori ambao watu huwinda kwa ajili ya kula.
Hii ina maana ya baraka maalumu ambayo baba hutamka kwa watoto wake.
"akamwambia Esau"
"Isaka akaanza kutetemeka"
Windo ina maana ya mnyama pori ambao watu huwinda na kuua.
Uchungu wa Esau ulikuwa sawa na ladha ya kitu kichungu. "alilia kwa sauti kubwa"
Huu ni msemo wenye maana ya Yakobo alichukua kilichokuwa cha Esau. "Nimembariki badala yako"
Esau anatumia swali kuweka msisitizo juu ya hasira yake kwa Yakobo. "Yakobo ni jina sahihi kwa kaka yangu!"
Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema: "Jina la Yakobo lina maana ya "yeye akamataye kisigino". Katika lugha ya asili jina la "Yakobo" linatamkika kama neno la "mdanganyifu"
Hii inazungumzia kuhusu haki ya mzaliwa wa kwanza kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kukichukua. "Alinidanganya kumpatia mara mbili ya urithia ambayo ningepaswa kupokea kama mzawa wa kwanza!"
Hii inazungumzia juu ya baraka kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kuchua. "na sasa amekudanganya kumbariki yeye badala yake"
Esau anajua ya kwamba baba hawezi kumbariki na vitu vile vile alivyombariki Yakobo. Esau anauliza kama kuna kitu kinachosalia kusemwa kwake ambacho Isaka hakusema alipokuwa akimbariki Yakobo.
Isaka anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hakuna kilichobaki atakachofanya. "Hakuna kitu kingine nachoweza kufanya kwako!"
Hii inaweza kuelezwa kwa njia ya chanya. "Baba yangu, je hauna baraka moja zaidi kwa ajili yangu"
"akasema kwa Esau"
Hii inaongeza msisitizo kwa kile Isaka anachosema baadae. "Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachokwenda kukuambia"
Huu ni msemo unaomaanisha nchi yenye rutuba. "mbali na udongo wenye rutuba"
Katika 27:39-40 hivi viwakilishi vipo katika umoja na vina maana ya Esau, lakini kile Isaka anachosema pia kinaashiria kwa vizazi vya Esau.
"umande" ni matone ya maji yanayounda juu ya mimea wakati wa usiku. Hii inaweza kuwekwa wazi. "umande wa usiku kutoka mbinguni kumwagilia mimea yako"
Hapa "upanga" ina maana ya vurugu. "Utaiba na kuua watu ili kupata kile unachohitaji kuishi"
Hii inazungumzia juu ya mtu kuwa na bwana kana kwamba utawala wa bwana juu ya mtu ulikuwa ni nira ambayo mtu anaweza kubeba. "utajifanya huru kutoka kwa utawala wake"
Hapa "moyoni" ina maana ya Esau mwenyewe. "Esau alijisemea mwenyewe"
Hii ina maana ya idadi ya siku mtu huomboleza pale ambapo mmoja wa familia anapokufa.
Hapa "maneno" yana maana ya kile Esau alichosema. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu alimwambia Rebeka kuhusu mpango wa Esau"
"Sikiliza" au "Vuta nadhari"
"anajifanya ajisikie vizuri"
Hii haimaanishi "katika muda huu", lakini inatumika kuvuta nadhari kwa jambo muhimu linalofuata.
"ondoka hapa haraka na uende kwa Labani"
"kwa kipindi cha muda"
"hadi kaka yako atakapopoa"
Kutokuwa na hasira inazungumziwa kana kwamba hasira hugeukia upande tofauti kutoka kwa mtu. "hadi pale atakapokuwa hana hasira na wewe"
Rebeka anatumia swali kuweka msisitizo juu ya mawazo yake kwa suala hili. "Sitaki kuwapoteza wote wawili katika siku moja!"
Inasemekana ya kwamba iwapo Esau atamuua Yakobo, basi watamuua Esau kama muuaji.
Hii ni njia ya upole inayomaanisha wanawe kufa.
Rebeka anatia chumvi kuweka msisitizo jinsi alivyofadhaishwa kuhusu mwanamke Mhiti ambaye Esau alimuoa. "Nimefadhaishwa sana"
"hawa wanawake wahiti" au "vizazi vya Wahiti"
Msemo "binti wa nchi" ina maana ya wanawake wenyeji. "kama wanawake hawa wanaoishi katika nchi hii"
Rebeka anatumia swali kuweka msisitizo jinsi atakavyofadhaishwa iwapo Yakobo atamuoa mwanamke Mhiti". "Maisha yangu yatakuwa mabaya!"