Neno hili linatumika kuweka alama kwa sehemu mpya ya simulizi.
"kukawa na njaa" au "kukawa na njaa nyingine"
Unaweza kusema wazi ya kwamba nchi inayozungumziwa. "katika nchi ambayo Isaka na familia yake waliishi"
Msemo "katika siku" ina maana ya wakati ambapo Abrahamu alikuwa hai. "ambayo ilitokea wakati wa uhai wa Abrahamu"
Yahwe anaanza kuzungumza na Isaka.
"akamtokea Isaka"
Ilikuwa kawaida kuzungumzia kuondoka nchi ya ahadi kama "kushuka chini" kwenda sehemu nyingine.
"kwa maana nitakupa nchi hizi zote kwako na kwa uzao wako"
"Nitafanya kile nilichoahidi kwa Abrahamu baba yako kukifanya"
Yahwe anaendelea kuzungumza na Isaka
"Nitasababisha uwe na uzao mwingi"
Hii inazungumzia kuhusu uzao wa Isaka kana kwamba walikuwa sawa na idadi ya nyota.
Hii ina maana ya kila kitu juu ya dunia ikijumlisha jua, mwezi na nyota.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitabariki mataifa yote ya dunia"
Misemo hii "alitii sauti yangu" na "kutunza maelekezo yangu, amri zangu na sheria zangu" zina maana moja. "Abrahamu alinitii na kufanya kila kitu nilichomuamuru kufanya"
Hapa "sauti" ina maana ya Yahwe. "Alinitii"
Isaka pekee ndiye aliyetajwa kwa sababu ni kiongozi wa familia, lakini familia yake yote ilikuwa pamoja naye. "Kwa hiyo Isaka na familia yake walikaa Gerari"
Hapa "aliogopa" ina maana ya hisia isiyofaa inayompata mtu wakati akipata tishio la kudhuriwa kwake au kwa wengine. "Aliogopa kusema"
"ili kwamba wamchukue Rebeka"
Neno "tazama" linaonyesha ya kwamba kile alichokiona Abimeleki kilimshangaza. "Na alishangazwa kuona ya kwamba Isaka"
Maana zaweza kuwa 1) alikuwa akimgusa kwa njia ambayo mume humgusa mkewake au 2) alikuwa akicheka na kuzungumza pamoja naye kwa namna ambayo mume huzungumza na mkewe.
Yawezekana Abimeleki alimtuma mtu kumwambia Isaka ya kwamba alihitaji kumuona. "Abimeleki alimtuma mtu kumleta Isaka kwake"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuelezwa kama nukuu isiyokuwa moja kwa moja. "Kwa nini ulisema ya kwamba ni dada yako?"
"ili amchukue"
Abimeleki alitumia swali hili kumkaripia Isaka. "Haukupaswa kufanya jambo hili kwetu!"
Hii inazungumzia kuhusu kumsababisha mtu kuwa na hatia kana kwamba "hatia" ilikuwa ni kitu kinachowekwa juu ya mtu. "ungeweza kusababisha tuwe na hatia ya kuchukua mke wa mtu"
Hapa "yetu" ina maana ya Abimeleki na watu wake.
Hapa "atakayemgusa" ina maana ya kumgusa kwa namna ya kumdhuru. "Yeyote atakayemdhuru mwanamume huyu"
Inawezekana Abimeleki alikusudia kumwambia mtu kumuua yeyote ambaye angemdhuru Isaka au Rebeka. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitamuua" au "Nitawaamuru wanamume wangu kumuua"
Hii inaanza sehemu mpya ya simulizi. Inabadilisha kutoka kueleza kuhusu Isaka kumuita Rebeka dada yake, na inaanza kuelezea kuhusu jinsi Isaka alivyokuwa tajiri na Wafilisti wakawa na wivu kwake.
"Gerari"
Hii ina maana ya "mara mia zaidi ya alivyopanda"/Inaweza kuelezwa kwa ujumla zaidi kama "zao kubwa sana"
"Isaka akawa tajiri" au "Akawa tajiri"
"na akapata zaidi na zaidi hadi akawa tajiri sana"
Hii inaweza kujumuisha mbuzi pia.
Hapa "familia" ina maana ya wafanya kazi au watumishi. "watumishi wengi"
"Wafilisti walikuwa na wivu kwake"
Hapa neno hili halimaanishi "katika kipindi hiki". Inaonyesha wapi matukio ya simulizi yanapoanzia. Inaweza kutafsiriwa kwa neno unganishi "Kwa hiyo" kuonyesha ya kwamba hii ni tokeo la kilichotokea katika 26:12.
Msemo wa "katika siku za" ina maana ya maisha ya mtu. "wakati Abrahamu, baba yake, alipokuwa akiishi"
Maana zaweza kuwa 1) hili ni tukio lingine kumlazimisha Isaka na watu wake kuondoka. "Kisha Abimeleki akasema" au "Hatimaye Abimeleki akasema" au 2) Abimeleki alifanya uamuzi huu kwa sababu aliona ya kwamba watu wake walikuwa na wivu na walitenda uhasama dhidi ya Isaka. "Basi Abimeleki akasema"
"mwenye nguvu zaidi ya sisi"
Isaka pekee ametajwa kwa sababu yeye ni kiongozi, lakini familia yake na watumishi wake walienda naye. "Kwa hiyo Isaka na nyumba yake waliondoka"
Hapa "Isaka" ina maana ya Isaka na watumishi wake. "Isaka na watumishi wake wakachimba"
"ambao watumishi wa Abrahamu walichimba"
Msemo "katika siku za" ina maana ya maisha yote ya binadamu. "ambapo Abrahamu, baba yake, alipokuwa anaishi"
Hii ndio ilikuwa sababu ya Isaka kuvichimba. Njia kadhaa za kutafsiri hii ni 1) Kwa kuwa hili lilitokea kwanza, sentensi hii inaweza ikaja kabla ya sentensi juu ya Isaka kuvichimba au 2) Sentensi hii inaweza kuanza na "Isaka alifanya hivi kwa sababu Wafilisti waliwazuia"
"walizijaza na udongo"
Msemo huu una maana ya chemichemi ya maji ya asili waliyofunua walipokuwa wakichimba kisima kipya. Ilitoa maji safi ya muendelezo kwa ajili ya kunywa.
"wanamume wanaotunza mifugo"
Hapa "yetu" ina maana ya wafugaji wa Gerari"
Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Eseki lina maana ya "malumbano" au "mabishano".
"Kisha watumishi wa Isaka wakachimba"
"wafugaji wa Gerari walibishana na wafugaji wa Isaka"
"kwa hiyo Isaka akakiita"
Watafsiri wanaweza kuweka maandishi mafupi yanayosema. "Jina la Sitna ina maana ya "kupinga" au "kushtaki"
Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Rehobothi lina maana ya "kuweka nafasi kwa ajili ya" au "nafasi wazi".
Isaka alikuwa akijizungumzia mwenyewe na nyumba yake.
Hapa "kwenda juu" inaweza kumaanisha kwenda kaskazini. "Isaka aliondoka pale na kwenda Beersheba"
"atasababisha vizazi vyako kuongezeka maradufu" au "atasababisha vizazi vyako kuwa wengi sana"
"kwa mtumishi wangu Abrahamu" au unaweza kuweka maana yote wazi zaidi. "kwa sababu nilimuahidi mtumishi wangu Abrahamu kuwa nitafanya hili"
Unaweza kuweka wazi kwa nini Isaka alijenga dhabahu. "Isaka alijenga dhabahu pale kutoa sadaka kwa Yahwe"
"Kuita" ina maana ya kuomba au kuabudu. Hapa "jina" lina maana ya Yahwe. "aliomba kwa Yahwe" au "alimuabudu Yahwe"
"akaenda kwa Isaka"
Hili ni jina la mwanamume.
Maana zaweza kuwa 1) "rafiki yake Abimeleki" au 2) "mshauri wa Abimeleki"
Hili ni jina la mwanamume.
Hii ina maana ya Abimeleki, Ahuzathi na Fikoli. Mmoja wao aliongea na wengine wawili walikubaliana na kile alichosema. Haikumaanisha waliongea kwa wakati mmoja. "mmoja wao alisema"
"Tunajua" au "Tuna uhakika"
"Kwa hiyo tunataka kufanya agano"
Hii inaweza kutafsiriwa kama mwanzo wa sentensi mpya. "Tumetenda mema tu kwako"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe amekubariki"
Kula chakula pamoja ilikuwa sehemu ya kufanya agano na mtu mwingine.
Hapa "akawaandalia" ina maana ya "Abimeleki, Ahuzathi na Fikoli"
Hapa "wakala" ina maana ya Isaka, Abimeleki, Ahuzathi, na Fikoli. "walikula wote"
"Waliamka mapema"
"Kwa hiyo alikiita kisima Shiba". Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Shiba linafanana na neno lenye maana ya "kiapo".
Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Beersheba inaweza kumaanisha "kisima cha kiapo" au "kisima cha saba"
Sehemu kubwa ya Mwanzo 26 inahusu Isaka. Mistari hii inamhusu mtoto wake mkubwa Esau.
"40"
"alioa". Unaweza kusema kwa uwazi ya kwamba alioa wanawake wawili. "alioa wake wawili"
Haya ni majina ya wake wa Esau.
Haya ni majina ya wanamume.
"vizazi vya Hethi" au "mzawa wa Hethi"
Hapa "wakamhuzunisha" ina maana ya Yudithi na Basemathi. Kumhuzunisha au kumsikitisha mtu inazungumziwa kana kwamba "huzuni" ni chombo ambacho mtu anaweza kukileta kwa mtu. "Walimfanya Isaka na Rebeka wawe na huzuni" au "Isaka na Rebeka walimsikitisha kwa sababu yao"