Taarifa kuhusu Abrahamu.
Hii ina maana ya watu waliotajwa katika mistari ya 2-4.
"Isaka alirithi kila kitu alichomiliki Abrahamu". Ilikuwa kawaida kwa baba kugawanya utajiri wake alipokuwa mzee na sio kuacha hivyo kwa wengine kufanya baada ya yeye kufariki.
"Abrahamu aliishi miaka 175"
"Abrahamu alivuta pumzi yake ya mwisho na akafa". Misemo ya "alivuta pumzi ya mwisho" na "akafa" ina maana ya kitu kimoja. "Abrahamu alikufa"
Hii ni njia ya upole ya kusema mtu alikufa.
Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Abrahamu aliishi muda mrefu sana. "alipomaliza kuishi muda mrefu na akawa mzee sana"
Kuishi maisha marefu sana inazungumzwa kana kwamba maisha yalikuwa chombo kinachoweza kujaa.
Hii ina maana ya kwamba Abrahamu alikufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "aliwaunga familia yake ambao walikuwa wameshakufa"
Efroni alimiliki shamba Makpela na pango ambalo lilikuwa ndani ya hilo shamba. Abrahamu alinunua shamba lile kutoka kwa Efroni.
Makpela lilikuwa jina la eneo au sehemu.
Haya ni majina ya wanamume.
Makpela ilikuwa karibu na Mamre.
Hii ilikuwa jina jingine kwa mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale"
"Abrahamu alinunua shamba hili"
Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walimzika Abrahamu"
"Mwana wa Abrahamu"
Jina hili lina maana ya "kisima cha yule aliye hai anionaye mimi"
Hili neno linatumika kutambulisha sehemu mpya ya simulizi na taarifa kuhusu Ishameli.
Taarifa ya jumla
Hii inaweza kuwekwa kama sentensi mbili. "Haya yalikuwa majina ya wana kumi na wawili wa Ishmaeli. Waliongoza kabila ambazo ziliitwa baada yao, na kila mmoja wao alikuwa na vijiji vyao na kambi zao"
"12"
Hapa neno "maseyidi" ina maana ya wanamume waliokuwa viongozi au watawala wa makabila; haimaanishi ya kwamba walikuwa watoto wa mfalme.
"Ishmaeli aliishi miaka 137"
Msemo "akapumua pumzi yake ya mwisho" na "akafa" zina maana moja. "alikufa"
Hii ina maana ya kwamba ishmaeli alikufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alijiunga na familia yake ambao tayari walikuwa wamekufa"
"Uzao wake walikaa"
"kati ya Havila na Shuri"
Havila Ilikuwa mahali katika jangwa la Arabia.
"katika upande wa"
Maana zaweza kuwa 1) "hawakuishi kwa amani pamoja" au 2) "waliishi mbali kutoka kwa ndugu zao wengine"
Sentensi hii inatambulisha habari ya uzao wa Isaka katika Mwanzo 25:19-35:29. "Hii ni habari ya uzao wa Isaka, mwana wa Abrahamu"
"umri wa miaka 40"
"alipomuoa Rebeka"
Bethueli alikuwa baba wa Rebeka.
Hili lilikuwa jina lingine la eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo lile lile na Iraq ya sasa.
"hakuwa na uwezo wa kupata mimba"
Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba Rebeka alikuwa mimba na watoto wawili katika wakati mmoja. "Rebeka, mke wake, akawa mimba na mapacha"
"watoto ndani mwake wakaendelea kugusana baina yao" au "Watoto walisukumana dhidi yao wenyewe ndani mwake"
Rebeka alikuwa mimba na mapacha.
"Alienda kumuuliza Yahwe kuhusu suala hili". haipo wazi alienda wapi. Inawezekana alienda sehemu ya siri kuomba, au alienda sehemu kutoa sadaka.
"akamwambia Rebeka"
Hii ni lugha ya kishairi.
Hapa "mataifa mawili" yana maana ya watoto wawili. Kila mtoto atakuwa baba wa taifa moja. "Mataifa mawili yatakuja pamoja kutoka kwa mapacha ndani yako"
Hapa "mataifa mawili" ina maana ya watoto wawili. Kila mtoto atakuwa baba wa taifa moja. Hii inaweza kutafsiriwa kama kitenzi cha kutenda. "na utakapozaa hawa watoto wawili watakuwa wapinzani"
Maana zaweza kuwa 1) "mkubwa atamtumika mdogo" au 2) "uzao wa mkubwa utamtumikia uzao wa mdogo"
Neno la "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "naam"
Maana zaweza kuwa 1) ngozi yake ilikuwa nyekundu na alikuwa na nywele nyingi katika mwili wake au 2) alikuwa na nywele nyingi nyekundu katika mwili wake. "nyekundu na yenye nywele kama nguo iliyotengenezwa na nywele ya mnyama"
"Jina Esau linafanana na neno "nywele"
"kushika sehemu ya nyuma ya mguu wa Esau"
"Jina Yakobo lina maana ya "anashika kisigino"
"umri wa miak 60"
"akawa hodari katika uwindaji na kuua wanyama kwa chakula"
"mtu wa amani" au"mtu asiyekuwa na mambo mengi"
Hii inazungumzia kuhusu muda kana kwamba ilikuwa bidhaa ambayo mtu angetumia. "aliyebaki katika mahema sehemu kubwa ya muda"
Neno hili linatumika kuweka alama ya kubadili mwelekeo, kutoka katika simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Isaka na Rebeka.
Hapa neno "akampenda" ina maana "alimpendelea" au "kumpenda zaidi"
"kwa sababu alikula wanyama ambao Esau aliwinda" au "kwa sababu alifurahia kula wanyama pori ambao Esau alikamata"
Kwa kuwa huu ni mwanzo wa simulizi kuhusu jambo lilitokea kipindi kimoja, baadhi ya watafsiri wanaweza kuanza na msemo wa "Siku moja, Yakobo alipika".
"alichemsha chakula kiasi" au "alipika mchuzi kiasi". Mchuzi ulipikwa kwa dengu za kuchemsha.
"alikuwa dhaifu kwa sababu alikuwa na njaa sana" au "alikuwa na njaa sana"
"Nimechoka kwa sababu ya njaa" au "Nina njaa sana"
Jina Edomu lina maana ya "nyekundu"
"haki ya mwana wa kwanza kurithi sehemu kubwa ya utajiri wa baba yake"
Esau alitiachumvi kuweka msisitizo jinsi alivyokuwa na njaa. "Nina njaa mno nahisi kama vile ntakufa"
Esau alitumia swali kuweka msisitizo ya kwamba kula ilikuwa muhimu zaidi ya haki ya mzawa wa kwanza. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Urithi wangu haunisaidii iwapo nitakufa kwa njaa!"
Kile ambacho Yakobo alimtaka Esau aape kinaweza kuwekwa wazi. "kwanza apa kwangu ya kwamba utaniuzia haki yako ya mzaliwa wa kwanza"
Haya ni kama maharage, lakini mbegu zake ni ndogo sana, na kama vile tambarare.
"Esau alionyesha ya kwamba hakuthamini haki yake ya kuzaliwa"