Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya kuonyesha mapumziko kwa simulizi kuu. Hapa mwandishi anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi.
Abrahamu alikuwa akitaka kumuliza mtumishi wake kuapa kufanya jambo. Kuweka mkono chini ya paja la Abrahamu ingeonyesha ya kwamba hakika angefanya kile alichotaka kuapa kukifanya.
Hii inaweza kuelezwa kama amri. "apa"
Msemo "uape kwa" una maana ya kutumia jina la kitu au mtu kama msingi au nguvu ambayo kiapo kinafanywa. "niahidi mimi pamoja na Yahwe kama shahidi wako"
"Mungu wa mbingu na nchi". Maneno "mbingu" na "nchi" yanatumika pamoja kumaanisha kila kitu ambacho Mungu aliumba. "Mungu wakila kitu mbinguni na nchini"
Hii ina maana ya sehemu ambayo Mungu anaishi.
"kutoka kwa wanawake wa Kanaani" au "kutoka kwa Wakaanani". Hii ina maana ya wanawake wa Kanaani.
"miongoni mwao wale namoishi" Hapa "nikaapo" ina maana ya Abrahamu na familia yake yote na watumishi. "miongoni mwao tunapoishi"
Hii inaweza kuelezwa kama amri. "Apa ya kwamba utakwenda" au "Lakini ondoka"
"familia yangu"
"nitafanyaje iwapo"
"hatanifuata" au "akikataa kurudi pamoja nami"
"Je nimchukue mwanao kuishi katika nchi ambayo umetoka"
Msemo "hakikisha" unasisitiza amri inayofuata. "Kuwa mwangalifu usimpeleke mwanangu kule" au "Hakika hautakiwi kumpeleka mwanangu kule"
Hapa "nyumba" ina maana ya watu katika familia. "aliyenichukua kutoka kwa baba na familia yangu yote"
"aliapa kiapo kwangu"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "akisema kwamba angempataia nchi hii kwa uzao wake"
Maneno "atatuma" na ":wake" yana maana ya Yahwe.
Mstari wa 8 ni muendelezo wa maelekezo Abrahamu alimpatia mtumishi wake.
"Lakini kama mwanamke anakataa kurudi pamoja nami." Abrahamu alikuwa akijibu swali la mtumishi wake kutoka 24:5.
"utafunguliwa kutoka kwa kiapo ulichokifanya kwangu". Kutokamilisha kiapo inazungumziwa kana kwamba mtu anakuwa huru kutoka kwa kitu ambacho kimemkamata. "hautapaswa kufanya kile ulichoapa kwangu ambcho ulipaswa kufanya"
Hii ilikuwa ikionyesha ya kwamba hakika angefanya kile alichoapa kufanya.
"akafanya kiapo kwake"
"kuhusu ombi la Abrahamu" au "ya kwamba angefanya kile alichoambiwa na Abrahamu"
Sentensi inayoanza na "Akachukua pia" inatupa taarifa ya nyongeza kuhusu nini mtumishi alichukua katika safari. Alivikusanya kabla ya kuondoka.
Hii ina maana alichukua pia vitu vingi ambavyo bwana wake alitaka akawapatie familia ya mwanamke.
"akajiandaa na kuondoka" au "aliondoka na kwenda"
Maana zaweza kuwa 1) "mji ambapo Nahori aliishi" au 2) "mji ulioitwa Nahori".
Ngamia ni wanyama warefu wenye miguu mirefu. Aliwafanya wainamishe miguu yao na kushusha miili yao ardhini. "Aliwafanya ngamia kulala chini"
"kisima cha maji" au "kisima"
"kufuata maji"
"Kisha mtumishi akasema"
Unaweza kuiweka hii kwa neno kiunganishi "kwa". Hii inaonyesha kwa uwazi jinsi mtumishi anataka Mungu amuonyeshe uaminifu wake. "Onyesha agano la uaminifu kwa bwana wangu Abrahamu kwa kunipatia mafanikio leo"
"nipatie mafanikio". Mtumishi alitaka kupata mke mwema kwa mwana wa Abrahamu. Nomino inayojitegemea ya "mafanikio" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "nisaidie nifanikiwe" au "nifanye niweze kufanya kile nilichokuja kukifanya"
Huu ni uaminifu kwa sababu ya agano ambalo Mungu alifanya na Abrahamu. Nomino inayojitegemea ya "uaminifu" inaweza kuelezwa "uwe mwaminifu". "Uwe mwaminifu kwa bwana wangu Abrahamu kwa sababu ya agano lako"
Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.
"chemichemi" au "kisima"
"wanawake vijana wa mji ule"
"Na itokee kwa namna hii" au "Fanya hii ifanyike"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Hii inaweza kuelezwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Ninapomuuliza msichana aniruhusu kunywa maji kutoka kwenye mtungi wake"
Wanawake walibeba mitungi juu ya mabega yao. Alitakiwa kushusha na kumpatia mwanamume anywe.
chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.
Nomino inayojitegemea "uaminifu" inawezakuelezwa kama "alikuwa mwaminifu". "ya kwamba ulikuwa mwaminifu kwa bwana wangu kwa sababu ya agano lako"
Msemo huu unatumika hapa kuweka alama
Neno "tazama" hapa linatuamsha kusikiliza taarifa ya kushangaza inayofuata.
chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.
"Baba yake Rebeka alikuwa Bethueli. Wazazi wa Bethueli walikuwa Milka na Nahori. Nahori alikuwa kaka yake Abrahamu"
Bethueli alikuwa baba yake Rebeka.
Hili ni jina la mwanamume.
Milka alikuwa mke wa Nahori na mama yake Bethueli.
Kisima kilikuwa sehemu ya chini katika muinuko wa chini ambapo mtumishi alikuwa amesimama.
"kukutana na yule msichana"
"maji kiasi"
chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.
"bwana". Hapa mwanamke anatumia msemo huu wa heshima kwa mwanamume, ingawa yeye sio mtumwa wake.
"alishusha mtungi wake haraka". Alikuwa akibeba mtungi juu ya bega lake. Ilimbidi ahushe ili apate maji kwa ajili ya mtumishi.
"Nitafuata maji"
"Kwa hiyo aliyatoa maji ndani ya mtungi haraka"
"chombo cha kunywshea wanyama". Chombo cha kunyweshea wanayma ni chombo kilicho wazi kinachoshikilia maji kwa ajili ya wanyama kunywa.
"Mtumishi"
"akamtazama Rebeka" au "alimtazama yule msichana"
Kujifunza jambo huwa kunazungumzwa kana kwamba kinaweza kuona. "kujua" au "kukusudia"
"Kutimiza lengo la safari yake" au "alifanya safari yake iwe ya mafanikio". Unaweza kuiweka wazi nini mtumishi alijaribu kukusudia. "alimwonyesha mwanamke nani ambaye angekuwa mke wa Isaka"
unaweza kuweka kwa uwazi taarifa inayoeleweka. "au kutofanikiwa katika safari yake"
"pete ya pua ya dhahabu ambayo ilikuwa na uzito wa gramu sita". Uzito unaonyesha thamani ya pete hiyo. "pete ya pua ya dhahabu ya gharama"
"bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa gramu 110". Uzito unaonyesha ukubwa na thamani yao. "bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake"
"Nani baba yako"
"Je kuna nafasi katika nyumba ya baba yako"
Ni wazi ya kwamba wanamume wengine walikuwa katika safari hii na mtumishi wa Abrahamu. Hapa "yetu" ina maana mtumishi na wale aliokuwa amesafiri pamoja naye.
"kukaa usiku huu" au "kukaa usiku wa leo"
"rebeka alisema" au "msichan yule alisema"
"kwa mtumishi"
"Bethueli ni baba yangu, na wazazi wake ni Milka na Nahori"
Inaeleweka ya kwamba malisho na chakula yalikuwa kwa ajili ya ngamia. "Tuna malisho na chakula cha kutosha kwa ajili ya ngamia"
"kwa ajili yako kulala usiku" au "ambapo utalala kwa usiku huu"
Hapa "yako" ina maana ya mtumishi na wale aliosafiri naye"
"mtumishi"
Hii ni ishara ya unyenyekevu mbele za Mungu.
"hakuacha kuonyesha agano lake la uaminifu na kweli kwa bwana wangu." Nomino zinazojitegemea "uaminifu" na "kweli" zinaweza kuelezwa kama "kuwa mwaniminfu na mkweli". "ameendelea kuwa mwaminifu na mkweli kwa sababu ya agano lake na bwana wangu"
Hii inaweza kuelezwa kwa namna ya chanya. "anaendelea kuonyesha"
"familia" au "ukoo"
Hapa "nyumba" ina maana ya watu waliokuwa wakiishi katika nyumba ya mama yake. "alikimbia katika nyumba na kumwambia mama yake na kila mtu pale"
"kila kitu ambacho kilitokea"
Neno hili linatumika hapa kuweka alama kuweka mapumziko katika simulizi kuu. hapa mwandishi anaelezea taarifa ya nyuma kuhusu Rebeka. Mwandishi anamtambulisha kaka yake, Labani, katika simulizi.
Mambo haya yalitokea kabla hajakimbia nje kwa mwanamume. Hii inatuambia kwa nini Labani alikimbia nje kwa mwanamume yule.
Hii inaweza kuelezwa kama nukuu isiyokuwa moja kwa moja. "alipokuwa amesikia ya kuwa dada yake Rebeka amemwambia nini mwanamume amekisema kwake"
"naam". Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.
"Njoo ndani" au "Ingia"
"wewe ambaye Yahwe amekubariki"
Hapa neno la "uliye" lina maana ya mtumishi wa Abrahamu.
Labani alitumia swali hili kumkaribisha mtumishi wa Abrahamu katika nyumba yake. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hauhitaji kubaki nje"
Neno "akaingia" linaweza kutafsiriwa kama "akaenda"
Haipo wazi nani alifanya kazi hii. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtumishi wa Labani alishusha mizigo kutoka kwa ngamia" au "ngamia walishushwa mizigo"
Hii haisemi nani alifanya kazi hii. Iwapo utaweka hii katika hali ya kutenda basi sema "watumishi wa Labani" kama jambo. "Watumishi wa Labani waliwapa malisho na chakula ngamia, na wakatoa maji"
"kwa watumishi wa Abrahamu na wanamume waliokuwa naye kuosha miguu yao"
Hapa neno "wakaandaa" lina maana ya watu wa familia ya Labani au watumishi wa nyumbani.
"kumpatia mtumishi chakula"
"kuzungumza maneno yangu" au "nimekuambia kwa nini nipo hapa"
Hapa neno "amekuwa" lina maana ya Abrahamu.
"amekuwa tajiri sana"
Neno "amempatia" lina maana ya Yahwe.
Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.
"alimzaa mtoto wa kiume"
"bwana wangu amempatia ... kwa mtoto wake wa kiume"
"Bwana wangu amenifanya niape ya kwamba nitafanya kile alichonimabia kufanya. Alisema"
Hii ina maana ya wanawake wa Kaanani. "kutoka kwa wanawake wa Kaanani" au "kutoka kwa Wakaanani"
"miongoni mwa wale ninamoishi". Hapa "ninamoishi" ina maana ya Abrahamu na familia yake yotena watumishi wake. "miongoni mwa wale tuishipo"
"kwa ukoo wangu"
Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.
Hili ni jambo ambalo linaweza kutokea. "Je kama mwanamke hatakuja pamoja nami" au "Nitafanyaje iwapo mwanamke huyu hatakuja pamoja nami?"
Kumtumikia Yahwe inazungumzwa kana kwamba Abrahamu alikuwa akitembea ndani ya uwepo wa Yahwe. "ambaye namtumikia"
"atafanya safari yako kufanikiwa"
"familia"
Hii ni nadharia tete ambayo Abrahamu alifikiri isingeweza kutokea. Maana zaweza kuwa 1) "Kuna njia moja tu ya kuwa huru na kiapo changu: iwapo utakuja kwa ndugu zangu na hawatakupatia mwanamke kwako, basi utakuwa huru kutoka kwa kiapo changu" au 2) kujengea mstari wa 40, "iwapo utaenda kwa familia ya baba yangu na kumuuliza msichana, utakuwa umefanya kile nilichokuomba ufanye. Iwapo hawatakupatia msichana kwako, basi utakuwa huru kwa kipao ulichoapa kwangu"
"utafunguliwa kutoka kwa kiapo ulichofanya kwangu". Kushindwa kutimiza kiapo inazungumzwa kana kwamba mtu yupo huru na kitu kilichomfunga. "hautapaswa kufanya kile ulichoapa kwangu ambacho ungefanya"
Lugha zinatumia maneno "njoo" na "kwenda" tofauti. "iwapo utafika kwa nyumba ya ndugu zangu" au "utakapokwenda kwa ndugu zangu"
Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.
"kisima"
Mtumishi alikatisha kile alichokuwa akimuuliza Mungu kwa kuvuta nadhari ya Mungu kwa pale alipokuwa amesimama.
Mtumishi alirudia kueleza ombi lake, na alikuwa na mambo matatu kusema juu ya mwanamke ambayo alitumaini yangekuja.
"kuchukua maji"
chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.
Mtumishi alikamilisha ombi lake.
Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.
Kuomba kimoyo moyo katika akili ya mtu inazungumzwa kana kwamba alikuwa akizungumza ndani ya moyo wake. Neno "moyo" lina maana ya mawazo yake na fikra zake. "kuomba" au"kuomba kimya kimya"
"naam" au "ghafla". Neno "tazama" hapa linatuamsha kusikiliza taarifa inayoshangaza inayofuata.
chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.
Msemo "akashuka chini" unatumika kwa sababu kisima kilikuwa sehemu ya chini zaidi ya mahali watumishi walipokuwa wamesimama.
"kisima"
"wakawapa ngamia maji"
Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.
"Baba yangu Bethueli. Wazazi wake ni Nahori na Milka"
Katika simulizi hii, vitu vyote hivi vilikuwa vya dhahabu.
Hii ni ishara ya unyenyekevu mbele za Mungu.
"amenileta hapa"
Neno la kiunganishi "kwa sababu" linaweza kutumika kuonyesha hii ni sababu mtumishi alimuabudu Mungu. "kwa sababu Yahwe aliniongoza"
Hii ina maana ya Bethueli, mwana wa Abrahamu kaka yake Nahori.
Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.
"Kwa hiyo". Hapa "kwa hiyo" haimaanishi "katika muda huu", lakini unatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimi linalofuata.
Namna gani wangeonyesha uaminifu wao na ukweli inaweza kuelezwa kwa uwazi. "niambie kama utakuwa mwaminifu na mkweli kwa bwana wangu kwa kunipatia Rebeka awe mke wa mwana wake"
Neno "mko" ina maana ya Labani na Bethueli.
Hizi nomino zinazojitegemea zinaweza kuelezwa kama "umanifu na ukweli"
Huu ni uaminifu wa watu wa familia
Taarifa inayoeleweka inaweza kuelezwa kwa uwazi. "Lakini kama haujajiandaa kumtendea bwana wangu kwa uaminifu na ukweli wa familia"
Maana zaweza kuwa 1) kuamua nini cha kufanya kunazungumzwa kana kwamba mtu atageuka upande mmoja au mwingine. "ili kwamba nijue nini cha kufanya" au 2) mtumishi anataka kujua kama anahitaji kusafiri sehemu nyingine. "ili kwamba niendelee na safari yangu"
Huyu alikuwa baba wa Labani na Rebeka.
"Yahwe alisababisha haya yote kutokea"
Wanasema hawana mamlaka ya kuamua kwamba aliyofanya Mungu ni mema au mabaya. "hatuthubutu kuhukumu kile ambacho Yahwe anatenda"
Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.
"Huyu hapa Rebeka"
"Maneno ya Labani na Bethueli". Hapa "maneno" ina maana ya kile walichosema. "kile ambacho Labani na Bethueli walisema"
Kuinama chini mbele ya Mungu ni ishara ya kumuabudu yeye.
"vipande vya fedha na dhahabu" au "vitu vilivyotengenezwa kwa fedha na dhahabu"
"zawadi za gharama" au "zawadi za thamani"
"Watumishi wa Abrahamu na wanamume wake"
"walilala pale usiku ule"
"waliamka asubuhi iliyofuata"
"Niruhusu niondoke na kurudi"
"angalau siku kumi zaidi"
"10"
"Kisha"
"Mtumishi wa Abrahamu akasema"
"kwa kaka wa Rebeka na mama yake"
"Msinikawize" au "Msinifanye nisubiri"
Hapa "njia" ina maana ya safari. "Yahwe amefanya nifanikiwe katika lengo la safari yangu"
"Niruhusu niondoke"
"Kwa hiyo familia ilimpeleka Rebeka"
Rebeka alikuwa dada wa Labani. "ndugu yao" au "dada wa Labani"
Hii ina maana ya mtumishi wa kike ambaye alimlisha Rebeka alipokuwa mtoto mchanga, akamtunza alipokuwa mtoto, na alimtumikia.
Rebeka hakuwa adad kwa kila mtu katika familia yake. Lakini walimuita kwa jinsi hii kuonyesha walimpenda. "Dada yetu Rebeka"
Hapa "mama" ina maana ya mama. "na uwe mama wa mamilioni wa watu" au "na uwe na uzao mkubwa"
Hii ina maana ya idadi kubwa au idadi isiyohesabika.
Majeshi huvunja katika malango ya miji ya adui zao na kuwashinda watu. "na uzao wako wawashinde kabisa wale wawachukiao"
"Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake wakawapakia ngamia"
"Katika njia hii mtumishi wa Abrahamu alimchukua Rebeka pamoja naye na kurudi naye mahali alipotoka"
Neno hili linaweka alama ya kubadili simulizi. Ilikuwa inaeleza juu ya mtumishi kutafuta mke, na sasa itaanza kueleza kuhusu Isaka.
Hili ni jina la maji ya kisima kule Negebu.
"jioni moja Isaka alitoka shambani kufikiri". Hii inaweza kuwa muda mrefu baada ya mtumishi na Rebeka kuondoka nyumbani kwake kwa maana walisafiri umbali mrefu.
Hili neno "tazama" hapa linatumasha kusikiliza kwa taarifa ya kushangaza inayofuata. "Alipotazama juu akashangaa kuona ngamia wakija"
"Rebeka akatazama juu"
"alishuka juu ya ngamia haraka"
"Kwa hiyo alijifunika uso na shela yake". Hii ni ishara ya heshima na adabu kwa mwanamume atakayemuoa. Maana kamili inaweza kuelezwa wazi.
Kipande cha kitambaa kilichotumika kufunika kichwa cha mtu, mabega na uso.
Misemo hii miwili ina maana ya kwamba Isaka alimuoa Rebeka. "na akamuoa Rebeka" au "na akamchukua kama mke wake"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa hiyo Rebeka alimfariji Isaka"