Hapa msemo "kumsikiliza" una maana ya Yahwe kumsaidia Sara kupata mtoto. "Yahwe alimsaidia Sara"
"akamzaa mtoto wa kiume wa Abrahamu"
"Abrahamu alipokuwa mzee sana"
"katika muda haswa ambao Mungu alimwambia ingekuja kutokea"
"Abrahamu alimuita mtoto wake wa kiume, yule ambaye Sara alimzaa, Isaka" au "Abrahamu alimuita mtoto wao wa kiume Isaka"
"Mwanae Isaka alipofikisha umri wa siku nane, Abrahamu alimtahiri"
"siku 8"
"alimuamuru Abrahamu kufanya"
"100"
Sara alikuwa akicheka kwa sababu alishangazwa na alikuwa na furaha. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Mungu alinisababisha nicheke kwa furaha"
Kile ambacho watu wangesikia kinaweza kuwekwa wazi. "kila mtu asikiaye kuhusu kile Mungu amefanya kwangu"
Hili swali la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakuna ambaye angeweza kusema kwa Abrahamu ya kwamba Sara atalea watoto"
Hii ni lugha ya upole ikimaanisha kunyonyesha watoto. "mnyonyeshe mtoto maziwa yake mwenyewe"
"aliachishwa" ni lugha ya upole ya kusema mtoto alimaliza kunyonyeshwa. "Isaka akakua, na pale alipokuwa hahitaji tena kunyonya, Abrahamu aliandaa karamu kubwa"
Jina la mwana wa Hajiri linaweza kuwekwa wazi. "Ishmaeli, mwana wa Hajiri Mmisri na Abrahamu"
Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba alimzomea au alimcheka Isaka. "alimcheka Isaka"
"Sara akamwambia Abrahamu"
"mfukuze aende zake" au "mtoweshe"
Hii ina maana ya Hajiri na Ishmaeli. Sara hakuwatambua kwa majina kwa sababu alikuwa amekasirishwa nao.
"pamoja na mwanangu Isaka"
"Abrahamu alikuwa na huzuni kuhusu kile alichosema Sara"
"kwa sababu ilikuwa inahusu mwanawe" Inamaanisha mwanawe, Ishameli"
"Usifadhaike kuhusu mvulana na mjakazi wako"
Hapa "maneno" yana maana ya kile kinachosemwa. "Fanya kila kitu ambacho Sara anakuambia kuhusu wao"
Msemo "utaitwa" una maana ya wale watakaozaliwa kupitia Isaka ndio wale Mungu anawatambua kuwa uzao ambao alimuahidi Abrahamu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Isaka ndiye atakayekuwa baba wa uzao niliokuahidi kwako"
Neno "taifa" lina maana ya Mungu atampatia uzao mwingi ili kwamba wawe taifa kubwa la watu. "Nitamfanya mwana wa mwanamke mjakazi pia awe baba wa taifa kubwa"
Maana zaweza kuwa 1) hii inaweza kumaanisha chakula kwa ujumla au 2) hii ina maana ya mkate mahususi.
"mfuko wa maji". Chombo cha maji kilitengenezwa kwa ngozi ya mnyama.
"Mfuko wa maji ulipokuwa tupu" au "Walipokunywa maji yote"
Hii ina maana ya umbali ambao mtu anaweza kutupa mshale kwa upinde. Hiini kama mita 100.
Kitenzi hiki cha kujitegemea "kifo" kinaweza kuwekwa kama "kufa". "Sitaki kutazama mwanangu akifa"
Hapa "sauti" ina maana ya sauti ya kilio chake. "kupaza sauti yake" ina maana ya kulia kwa sauti kubwa. "alipaza kwa sauti kubwa na kulia" au "alilia kwa sauti"
"kilio cha kijana". Hapa "kilio" ina maana ya sauti ambayo kijana alilia au alizungumza. "sauti ya Ishmaeli"
"mjumbe kutoka kwa Mungu" au "Mjumbe wa Mungu"
Hapa "mbinguni" ina maana ya sehemu ambapo Mungu huishi.
"Tatizo ni nini" au "kwa nini unalia"
Hapa "kilio" ina maana ya sauti ambayo kijana alilia au alizungumza. "sauti ya kijana alipokuwa amelala pale chini"
"msaidie kijana asimame"
Kumfanya Ishamaeli kuwa taifa kubwa ina maana Mungu atampa uzao mwingi ambao utakua taifa kubwa. "Nitafanya uzao wake kuwa taifa kubwa" au "Nitamfanya awe baba wa taifa kubwa"
Mungu kumfanya Hajiri aweze kuona kisima inazungumzwa kana kwamba alimfungua macho kihalisia. "Mungu alisababisha Hajiri kuona" au "Mungu alimuonyesha Hajiri"
"chombo kilichoundwa na ngozi" au "mfuko"
"mvulana" au "Ishameli"
Hapa msemo wa "akawa pamoja" ni lahaja ambayo ina maana ya Mungu alimsaidia au alimbariki mvulana. "Mungu alimuongoza mvulana" au "Mungu alimbariki mvulana"
"akawa na uwezo sana wa kutumia upinde na mishale"
"akapata mke"
Msemo huu unaweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
Hili ni jina la mwanamume.
"kamanda wa jeshi lake"
neno "lake" lina maana ya Abimeleki.
Hapa msemo "yuko pamoja nawe" ni lahaja yenye maana ya Mungu husaidia au humbariki Abrahamu. "Mungu hubariki kila kitu ufanyacho"
Neno "Sasa" halimaanishi "katika muda huu", lakini linatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata. "Sasa basi"
Hii ni lahaja yenye maana ya kutoa kiapo cha dhati kinachoshuhudiwa na mamlaka ya juu, kwa hali hii ni Mungu. "niahidi mimi na Mungu kama shahidi"
"ya kwamba hutanidanganya"
Hii inaweza kuelezwa kwa njia ya chanya. "utanifanyia haki mimi na uzao wangu"
Wanamume wawili walifanya agano kati yao. Kitenzi kinachojitegemea "umaninifu" kinaweza kuelezwa kama "mwaminifu" au "mtiifu". "Uwe mwaminifu kwangu na kwa nchi kama nilivyokuwa kwako"
Hapa "nchi" ina maana ya watu. "kwa watu wa nchi"
Hii inaweza kuelezwa kwa taarifa iliyoeleweka. "Ninaapa kuwa mwaminifu kwako na kwa watu wako kama ulivyokuwa kwangu"
Maana zaweza kuwa 1) Abrahamu alikuwa akilalamika kuhusu kile kilichotokea au 2) "Abrahamu pia alimkaripia Abimeleki"
"kwa sababu watumishi wa Abimeleki walichukua kisima kimoja cha visima vya Abrahamu"
"kuchukua kutoka kwa Abrahamu" au "wamekitawala"
"Hii ni mara ya kwanza nimesikia kuhusu jambo hili"
Hii ni ishara ya urafiki na ya kwamba Abrahamu amekubali kuweka agano na Abimeleki.
"Abrahamu aligawanya kondoo saba wa kike kutoka kundini"
"7"
"Kwa nini umegawanya hawa kondoo saba kutoka kundini?"
"utachukua"
Hapa "mkononi" una maana ya Abrahamu. "kutoka kwangu"
Neno "iwe" ina maana ya zawadi ya kondoo saba.
Kitenzi kinachojitegemea "shahidi" kinaweza kuelezwa kama "kuthibitisha". "Kuthibitisha kwa kila mtu"
"Abrahamu akapaita mahali pale"
"Beerisheba inaweza kuwa na maana ya "kisima cha kiapo" au "kisima cha saba".
"Abrahamu na Abimeleki"
Hili ni jina la mwanamume.
"wakarudi katika nchi ya Wafilisti"
Huu ni mti wa kijani ambao unaota jangwani. Inaweza kusemwa kwa ujumla zaidi. "mti"
"Mungu aishiye milele"
Hii ina maana ya muda mrefu zaidi