Hili ni eneo la jangwa upande wa mashariki wa mpaka wa Misri.
"aliwafanya wanamume wake kumfuata Sara na kumleta kwake"
"Mungu akamtokea Abimeleki"
Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "Nisikilize"
Hii ni njia ya nguvu ya kusema mfalme atakufa. "hakika utakufa hivi karibuni" au "Nitakuua"
"mwanamke aliyeolewa"
Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya kubadilisha kutoka kwenye simulizi kwenda kwa taarifa kuhusu Abimeleki.
Hii ni njia ya upole ya kusema hakufanya ngono pamoja naye. "Abimeleki hakulala na Sara" au "Abimeleki hakumgusa Sara"
Hapa "taifa" lina maana ya watu. Abimeleki ana wasiwasi ya kwamba Mungu atawaadhibu sio yeye tu, lakini watu wake pia. "hata watu wasio kuwa na hatia"
Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Zinaweza kutajwa kwa nukuu isiyo dhahiri. "Je sio yeye mwenyewe aliyeniambia ya kwamba huyo ni dada yaek? Hata yeye mwenyewe alinimbia ya kwamba ni kaka yake"
Abimeleki alitumia swali la balagha kumkumbusha Mungu juu ya jambo alilokuwa akilifahamu tayari. Hii inaweza kufanywa kuwa kauli. "Abrahamu mwenyewe aliniambia 'Huyu ni dada yangu'" au "Abrahamu alisema ya kwamba ni dada yake".
Maneno "yeye mwenyewe" na "Sara mwenyewe" yanatumika kuweka msisitizo kuleta nadhiri kwa Abrahamu na Sara na kuwalaumu kwa kilichotokea.
Hapa "moyo" una maana ya mawazo yake au nia zake. Pia "mikono" hapa ina maana ya matendo yake. "Nimefanya hili kwa nia njema na matendo mema" au "Nimefanya hivi bila mawazo au matendo ya uovu"
"Mungu akasema kwa Abimeleki"
Hapa"moyo" una maana ya mawazo na nia zake. "ulifanya hivi kwa nia njema" au "ulifanya hivi bila kuwa na nia ya uovu"
Hii ni lugha ya upole kwa kufanya ngono na Sara. "kulala naye"
"Mke wa Abrahamu"
"Nitakuruhusu uishi"
"nyie watu wote"
"Aliwaambia kila kitu ambacho Mungu alimwambia"
Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumshtaki Abrahamu. "Umefanya jambo hili baya kwetu!" au "Tazama ulichokifanya kwetu!"
Neno "umetufanyia" hapa linajitegemea na halimhusu Abrahamu na Sara.
Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumkumbusha Abrahamu ya kwamba hakufanya dhambi dhidi ya Abrahamu. "Sijafanya jambo dhidi yako kusababisha wewe ulete ... dhambi."
Kumsababishia mtu awe na hatia ya kutenda dhambi inazungumzwa kana kwamba "dhambi" ilikuwa jambo linaloweza kuwekwa juu ya mtu. "ya kwamba umetufanya mimi na ufalme wangu kuwa na hatia kwa dhambi hii mbaya"
Hapa "ufalme" ina maana ya watu. "juu ya watu wa ufalme wangu"
"Usingefanya jambo hili kwangu"
"Nini kilisababisha ufanye hivi?" au "Kwa nini ulifanya hivi?" Kile ambacho Abrahamu alifanya kinaweza kuwekwa wazi. "Kwa nini uliniambia ya kwamba Sara ni dada yako?"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika nukuu tofauti. "Kwa sababu nilidhani ya kwamba kwa kuwa hakuna mwenye hofu ya Mungu hapa, mtu anaweza kuniua ili amchukue mke wangu"
Hapa "sehemu" ina maana ya watu. "hakuna mtu hapa Gerari mwenye hofu ya Mungu"
Hii ina maana ya kumheshimu Mungu sana na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii.
"Pia, ni kweli ya kwamba Sara ni dada yangu" au "Pia, Sara ni dada yangu ki ukweli"
"tuna baba mmoja, lakini mama tofauti"
Mstari wa 13 ni muendelezo wa jibu la Abrahamu kwa Abimeleki.
Hapa "nyumba" ina maana ya familia ya Abrahamu. "baba yangu na familia yangu yote" au "nyumba ya baba yangu"
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika nukuu tofauti. "Nilisema kwa Sara ya kwamba nataka awe mwaminifu kwangu kwa kuwaambia watu kila mahali tuendapo ya kwamba mimi ni kaka yake"
"Abimeleki akaleta baadhi"
"Abimeleki akasema kwa Abrahamu"
Hapa na katika mstari wa 16 neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.
Hii ni njia ya kusema "ninaifanya nchi yangu yote iwe wazi kwako"
"ishi popote upendapo"
"1,000"
Kutoa fedha kuthibitisha kwa wengine ya kwamba Sara hana hatia inazungumzwa kana kwamba anaweka mfuniko juu ya kosa ili mwingine asilione. "Ninampatia hili kwake, ili kwamba wale ulionao wajue haujafanya kosa"
Hapa "macho" ina maana ya mawazo na fikra za mtu.
Msemo huu wa "umemfanya kuwa na haki" unaweza kuwa katika hali ya kutenda. "kila mtu atajua ya kwamba huna hatia"
"kutoweza kupata watoto kabisa"
Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu Abimeleki alimchukua mke wa Abrahamu Sara"