miaka mia tisa na tisa - Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
"Mungu mwenye uweza wote" au "Mungu ambaye ana uwezo wote"
Kuenda ni sitiari kwa ajili ya kuishi, na "mbele yangu" au "katika uwepo wangu" hapa ni sitiari kwa ajili ya kutii. "Ishi kwa namna nayotaka uishi" au "Kunitii"
"Iwapo utafanya hivi, basi nitathibitisha"
"Nitatoa agano langu" au "Nitafanya agano langu"
Katika agano hili Mungu anamuahidi kumbariki Abramu lakini pia anataka Abramu amutii.
"nitazidisha kwa wingi idadi ya vizazi vyako" au "nitakupatia vizazi wengi sana"
"Abramu alijirusha uso chini ya ardhi" au "Abrahamu aliinama chini mara moja uso ukiwa ardhini." Alifanya hivi kuonyesha ya kuwa alimheshimu Mungu na angemtii.
Mungu alitumia msemo huu kutambulisha kile alichoenda kukifanya kwa Abramu kama sehemu ya agano lake na Abramu.
Neno "tazama" hapa linasema ya kwamba kinachofuata ni cha uhakika: "agano langu na wewe ni la uhakika"
"baba wa idadi kubwa ya mataifa" au "yule ambaye mataifa mengi yatajiita"
Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi yafuatayo: Jina "Abramu" lina maana ya "baba aliyeinuliwa" na jina "Abrahamu" linafanana na "baba wa kundi"
"Nitakusababisha uwe na vizazi vingi sana"
"Nitasababisha vizazi vyako kuwa mataifa"
"miongoni mwa vizazi vyako kutakuwa na wafalme" au "baadhi ya vizazi vyako kutakuwa na wafalme"
Mungu anaendelea kuzungumza na Abrahamu.
"katika kila kizazi"
"kama agano ambalo litadumu milele"
"kuwa Mungu wako na vizazi vyako" au "agano"
"Kanaani, kama miliki ya milele" au"Kanaani, kuimiliki milele"
Mungu anatumia msemo huu kutambulisha kile Abramu alichokuwa akielekea kufanya kama sehemu ya agano la Mungu na yeye.
"fuata agano langu" au "heshimu agano langu" au "tii agano langu"
"Hili ni hitaji la agano langu" au "Hii ni sehemu ya agano langu". Sentensi hii inatambulisha sehemu ya agano ambayo Abramu ilimpasa afanye.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Unapaswa kutahiri kila mwanamume miongoni mwako"
Hii ina maana ya wanadamu wa kiume
Baadhi ya jamii inaweza kutumia lugha nyepesi zaidi kama "Unatakiwa kutairiwa." Iwapo tafsiri yako ya "fanya tohara" inajumlisha neno la govi la ngozi ya mbele, hauhitaji kurudia.Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Unatakiwa kuwatahiri wanamume wote miongoni mwenu"
"ishara inayoonyesha ya kwamba agano lipo"
Maana zaweza kuwa 1) "ishara" au 2) "ishara". Maana ya kwanza inaonyesha kulikuwa na ishara moja, na maana ya pili inaonyesha kulikuwa na ishara zaidi ya moja. Hapa neno "ishara" ina maana ya ukumbusho kuhusu jambo ambalo Mungu aliahidi.
Mungu anaendelea kuzungumza na Abrahamu.
"Hii ina maana ya wanadamu wa kiume"
"katika kila kizazi"
Hii ina maana ya watumwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mwanamume yeyote utakayemnunua"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utaweka alama ya agano langu juu ya mwili wako"
"kama agano la kudumu". Kwa sababu iliwekwa juu ya mwili, hakuna aliyeweza kuifuta.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda, na unaweza kuacha maneno ambayo yanaweza kuleta maana mbaya katika lugha yako. "mwanamume ambaye haujamtahiri"
Maana zaweza kuwa 1) "nitamtenga mwanamume yeyote asiyetahiriwa ... govi la mbele kutoka kwa watu wake" au 2)"Ninataka umtenge mwanamume yeyote asiyetahiriwa ... govi la mbele kutoka kwa watu wake"
Maana zaweza kuwa 1) "aliuawa" au 2) "kufukuzwa kutoka kwenye jamii".
"Hajatii amri za agano langu." Hii ni sababu itakayomfanya atengwe kutoka kwa watu wake.
Maneno "kwa habari ya" zinatambulisha mtu anayefuata ambaye Mungu anamzungumzia.
"Nitamfanya azae mtoto kupitia kwake"
"atakuwa mama wa mataifa mengi" au "uzao wake watakuwa mataifa"
"Wafalme wa watu watatokana kwake" au "Baadhi ya uzao wake watakuwa wafalme wa watu"
"akawaza mwenyewe" au "akasema mwenyewe kimya kimya"
Abrahamu alitumia swali hili la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. "Hakika mwanamume mwenye umri wa miaka mia moja hawezi kuwa baba wa mtoto!"
Tena Abrahamu alitumia swali la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. msemo "ambaye ana umri wa miaka tisini" unasema kwa nini Abrahamu hakuamini ya kwamba Sarai hataweza kuzaa mtoto. "Sarai ana umri wa miaka tisini. Hakika hawezi kuzaa mtoto wa kiume!"
"Tafadhali muache Ishmaeli arithi agano ulilofanya pamoja na mimi" au "Huenda Ishmaeli anaweza kupokea baraka ya agano lako" Abrahamu alipendekeza jambo ambalo aliamini lingeweza kutokea"
Mungu alisema hili kusahisha imani ya Abrahamu juu ya Sarai kupata mtoto.
Neno "utamwita" linamlenga Abrahamu.
Maneno "na kwa habari" yanaonyesha ya kwamba Mungu anabadilisha maongezi kuhusu mtoto ambaye angezaliwa na kumuongelea Ishmaeli.
"Angalia" au "Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini kwa kile nachotaka kukuambia"
Hii ni lahaja inayokuwa na maana ya "nitamsababisha awe na watoto wengi"
"na nitamsababisha awe na uzao mwingi"
"machifu" au "watawala". Hawa viongozi sio wana kumi na mbili na wajukuu wa Yakobo ambao wataongoza makabila kumi na mbili ya Israeli.
Mungu anarudi kuongelea juu ya agano lako na Abrahamu na kusisitiza ya kwamba atatimiza ahadi yake na Isaka, na sio Ishmaeli.
"Mungu alipomaliza kuzungumza na Abrahamu"
"Mungu akamuacha Abrahamu"
"kila binadamu wa kiume katika nyumba ya Abrahamu" au "kila mtu wa kiume katika nyumba ya Abrahamu". Ina maana ya wanadamu wa kiume wa umri wote: watoto wachanga, wavulana na wanamume.
"Hii inajumlisha wale waliozaliwa katika nyumba yake na wale walionunuliwa kutoka kwa wageni"
Hii ina maana ya watumishi au watumwa
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wale ambao amekwisha wanunua"