Maeneno katika 14:1 yote ni miji inayojitegemea
Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.
"katika muda wa"
"walienda vitani" au "walianzisha vita" au "walijiandaa kwa vita"
Taarifa ya kwamba majeshi yao walikuwa pamoja nao inaweza kuwekwa wazi. "Wafalme hawa watano wa nyuma na majeshi yao waliungana"
Matukio katika mistari ya 4-7 yalitokea kabla ya mstari wa 3. Lugha yakoinaweza kuwa na namna ya kuonyesha hivi.
Inawezekana walitakiwa kumlipa kodi na kumtumikia jeshini. "walikuwa chini ya utawala wa Kedorlaoma"
"walikataa kumtumikia" au "walisitisha kumtumika"
Walifanya hivi kwa sababu wafalme wengine waliasi.
Haya ni majina ya makundi ya watu.
Haya ni majina ya sehemu.
Huu msemo unasaidia wasomaji kuelewa El parani ilikuwa wapi. Inaweza kutafsiriwa katika sentensi tofauti kama italazimu. "El Parani. El Parani ipo karibu na jangwa"
Mistari ya 8 na 9 inarudia kile kilichosemwa katika 14:3 na kuendelea kueleza yaliyojiri baada ya wafalme kukutana pamoja kupigana.
Neno "wakarudi" lina maana ya wafalme wanne wageni ambao walikuwa wakishambulia eneo la Kanaani. Majina yao yalikuwa Amrafeli, Arioko, Kadorlaoma na Tidali. "wakageuka na kuondoka"
Msemo huu unaelezea juu ya watu wa Waamori walioshindwa. Hawa walikuwa Waamori wengine walioishi katika maeneno mengine.
Mji wa Bela pia ulikuwa unaitwa Soari. Taarifa hii inaweza kuwekwa mwishoni mwa sentensi. "na mfalme wa Bela akaondoka na kujiandaa kwa vita. Bela pia inaitwa Soari.
"kujiunga vitani" au "kuanza mistari ya vita" Baadhi ya watafsiri wanaweza kusema kuwa majeshi yalipigana.
Kwa kuwa wafalme watano waliorodheshwa kwanza, baadhi ya lugha inaweza kutafsiri hii kama "wafalme watano dhidi ya wanne".
Neno hili linatambulisha taarifa ya nyuma kuhusu bonde la Sidimu. Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kutambulisha taarifa hii ya nyuma.
"ilikuwa na mashimo ya lami mengi". Haya yalikuwa mashimo katika ardhi ambayo yalikuwa na lami ndani mwao.
kimiminiko kinene, kinachonata, cheusi kinachotoka ardhini.
Huu ni usemi mwingine kwa ajili ya wafalme na majeshi yao. "wafalme wa Sodoma na Gomora na majeshi yao"
Maana zaweza kuwa 1) baadhi ya wanajeshi wao walianguka ndani ya mashimo ya lami au 2) wafalme wenyewe walianguka ndani ya mashimo ya lami. Kwa kuwa 14:17 unasema ya kwamba mfalme wa Sodoma alikwenda kukutana na Abramu, maana ya kwanza yaweza kuwa sahihi zaidi.
"Wale ambao hawakufa vitani na hawakuanguka ndani ya mashimo"
Hii ina maana ya mfalme Kedorlaoma na wafalme wengine na majeshi yao aliokuwa nao waliokuwa wakishambulia Sodoma na Gomora.
Maneno "Sodoma" na "Gomora" ni lugha nyingine kwa ajili ya watu walioishi katika miji ile. "utajiri wa watu wa Sodoma na Gomora" au "mali za watu wa Sodoma na Gomora"
"chakula na vinywaji vyao"
"wakaenda njia zao"
Misemo ya "mwana wa kaka wa Abramu" na "aliyekuwa akiishi Sodoma" unamkumbusha msomaji juu ya mambo yaliyoandikwa mapema kuhus Lutu. "walimchukua Lutu pia, pamoja na na mali zake zote. Lutu alikuwa mwana wa kaka wa Abramu na alikuwa akiishi Sodoma kwa kipindi hicho"
"Mwanamume alitoroka vitani na kuja"
"Abramu alikuwa anaishi" Hii inatambulisha taarifa ya nyuma.
"walikuwa washirika wa mkataba na Abramu" au "alikuwa na makubaliano ya amani na Abramu"
Hii inahusu mpwa wa Abramu Lutu
"wanamume waliofunzwa kupigana"
"wanamume waliozaliwa nyumbani mwa Abramu". Walikuwa watoto wa watumishi wa Abramu.
"akawafukuza"
Huu ni mji wa kaskazini wa Kanaani, mbali ya kambi ya Abramu.
Yawezekana hii ina maana ya mipango ya vita. "Abramu aliwagawa wanamume katika makundi kadhaa, na wakawashambulia maadui zao katika pande zote"
Hii ina maana ya vitu ambavyo maadui waliiba kutoka miji ya Sodoma na Gomora.
"na mali za Lutu ambazo maadui waliiba kutoka kwa Lutu"
"pamoja na wanawake na watu wengine ambao wafalme wanne waliwakamata"
Taarifa inayodokezwa kuhusu wapi alipokuwa anarudi inaweza kuwekwa wazi. "alirudi hadi pale alipokuwa akiishi"
Hii ni mara ya kwanza mfalme huyu anatajwa.
Watu hula mkate na divai mara kwa mara.
Mfalme Melkizedeki alimbariki Abramu.
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi, ambariki Abramu"
Hii ina maana ya sehemu ambayo Mungu huishi.
"Mungu aliye juu sana, kwa sababu amekupatia". Msemo unaoanza na "ambaye amekupatia" unatueleza jambo zaidi kuhusu Mungu aliye juu sana.
Hii ni njia ya kumsifu Mungu.
"ndani ya utawala wako" au "ndani ya uwezo yako"
Msemo "watu" unaweza kuwa na maana ya watu wa Sodoma ambao maadui waliwakamata. Abramu aliwaokoa alipomuokoa Lutu.
Hii ina maana "nimetoa kiapo" au "nimefanya ahadi".
"Ninachukua kutoka kwako kile tu vijana wangu walishakwisha kula". Abramu alikuwa akikataa kupokea chochote kwa ajili yake, lakini alikiri kuwa wanajeshi wake wamekula sehemu ya akiba wakati wa safari ya kurudi Sodoma baada ya vita.
Maana kamili ya kauli hii yawezwa kuwekwa wazi. "sehemu ya mali iliyokombolewa iliyokuwa ya wanamume walionisaidia kurudi"
Hawa ni washirika wa Abramu (14:13). Kwa kuwa walikuwa washirika wa Abramu walipigana vita pamoja naye. Maana kamili ya kauli inaweza kufanywa wazi. "washirika wangu Aneri, Eskoli na Mamre"