Neno hili linatumika kuweka alama sehemu mpya ya simulizi.
"Nenda kutoka nchini kwako, kutoka katika familia yako"
Hapa "nitakufanya" ni umoja na ina maana ya Abramu, lakini Abramu anawakilisha vizazi vyake. "Nitaanzisha taifa kubwa kupitia kwako" au "Nitawafanya vizazi vyako kuwa taifa kubwa"
Neno "jina" linawakilisha sifa ya mtu. "na kukufanya uwe maarufu"
neno "jina" linawakilisha sifa ya mtu. "na kukufanya uwe maarufu"
"Nitamlaani yeyote atakayekutendea jambo kwa njia ya aibu" au "iwapo kuna mtu atakayekutendea jambo lisilofaa, nitamlaani"
Hii inaweza kufanywa katika hali ya kutenda. "Nitabariki familia za nchi kupitia kwako"
"Kwa sababu yako" au "Kwa sababu nimekubariki"
Hii inajumlisha wanyama na mali isiyokuwa na uhai
Maana yaweza kuwa 1) "watumwa ambao wamewakusanya" au 2) "watu ambao wamewakusanya kuwa pamoja nao"
Ni jina la Abramu pekee linatajwa kwa sababu alikuwa kichwa cha familia. Mungu alimpatia amri ya kuchukua familia yake na kwenda kule. "Kwa hiyo Abramu na familia yake walikwenda katikati ya nchi"
"nchi ya Kanaani"
Yawezekana More ilikuwa jina ya sehemu
"Yahwe, kwa sababu alimtokea"
Abramu alikuwa na watu wengi pamoja naye alipokuwa akisafiri. Watu waliokuwa wakihama kutoka sehemu moja hadi nyingine waliishi ndani ya mahema. "walitengeneza mahema yao"
"waliomba kwa jina la Yahwe" au "kumuabudu Yahwe"
"Kisha Abramu alichukua hema lake na kuendelea na safari"
"kuelekea eneo la Negebu" au "kuelekea kusini" au "kusini ya jangwa la Negebu"
Mazao hayakuota vizuri msimu huo.
"katika eneo" au "katika nchi ambapo Abramu alikuwa akiishi"
Maana zaweza kuwa 1) "alikwenda kusini zaidi" au 2) "aliondoka mbali na Kaanani kuingia". Ingependeza kutafsiri kwa kutumia maneno ya kawaida ya kutoka eneo la juu kuelekea eneo la chini.
Sababu watakayomuua Abramu inaweza kufanywa wazi. "wataniua ili kwamba wakuoe"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba, kwa sababu yako, hawataniua mimi"
Maana zaweza kuwa 1) Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya wapi tukio linaanza, na kama lugha yako ina namna ya kufanya hivi basi tumia njia hiyo, au 2) "Na hivyo ndivyo kilichotokea"
"Wakuu wa Farao walimwona Sarai" au "wakuu wa Farao walimwona"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Farao akamchukua mpaka nyumbani kwake" au "Farao aliwaamuru askari wake kumpeleka nyumbani kwake"
Sarai
Maana zaweza kuwa 1)"Familia ya Farao", yaani kama mke au 2) "Nyumba ya Farao" au "Hekalu la Farao" ni tasifida ya Farao kumfanya awe mmoja wa wake zake.
"kwa ajili ya Sarai" au "kwa sababu yake"
Hii inaweza kufanywa kwa uwazi zaidi. "Kwa kuwa Farao alitaka kumchua Sarai , mke wa Abramu, aweze kuwa mke wake mwenyewe"
"Farao akamuita Abramu" au "Farao akamuamuru Abramu kuja kwake"
Farao alitumia lugha hii ya balagha kuonyesha jinsi gani alivyokasirika juu ya kile Abramu alichomfanyia. Inaweza kuelezeka kwa namna ya mshangao. "Umedanya jambo baya kwangu!"
"Kisha Farao akawaongoza wakuu wake kuhusu Abramu"
"na wakuu wakamfukuza Abramu kutoka kwa Farao, pamoja na mke wake na alivyokuwa navyo"