"Hii ni habari ya wana wa Nuhu." Sentensi hii inatambulisha habari ya vizazi vya Nuhu katika Mwanzo 10:1-11:9
"Wana wa yafethi na vizazi vyake waligawanyika na kuhamia pwani na visiwani"
Hii ina maana ya watu waliokuwa wakiishi kando ya pwani na visiwani.
"makazi yao". Hizi ni sehemu ambazo watu waliohama waliishi.
"Kila kundi la watu lilizungumza lugha yake" au " Makundi ya watu walijigawa kulingana na lugha zao"
Misraimu ni jina la Kihebrania la "Misri".
Maana zaweza kuwa 1) "hodari mwenye nguvu" au 2) "mwanamume mwenye nguvu" au 3) "mtawala mwenye uwezo".
Maana zaweza kuwa 1) "machoni pa Yahwe" au 2) "kwa msaada wa Yahwe"
Hii inatambulisha methali. Lugha yako yaweza tambulisha methali na misemo kwa namna tofauti. "Hii ni sababu watu husema"
Maana zaweza kuwa 1) miji ya kwanza aliyoijenga au 2) miji muhimu.
Nimrodi alikwenda Ashuru
orodha ya vizazi vya Nuhu inaendelea.
Misraimu alikuwa mmoja wa wana wa Hamu. Vizazi vyake vikawa watu wa Misri. Misraimu ni jina la Kihebrania la Misri.
Majina haya yana maana ya makundi makubwa ya watu walioshuka kutoka Kanaani.
"eneo" au "mpaka wa eneo"
Mwelekeo wa kusini waweza elezwa wazi kama itahitajika. "Kutoka mji wa Sidoni magharibi hata mji wa Gaza, ambao uko karibu na Gerari"
Mwelekeo ni "mashariki" au "bara" inaweza kuelezwa wazi kama itahitajika. "kisha mashariki mwa miji ya Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hata Lasha"
Neno "hawa" lina maana ya watu na makundi ya watu waliorodhoshwa katika mistari ya 10:6
"waligawanyika kulingana na lugha zao tofauti"
"katika makazi yao"
Arfaksadi alikuwa mmoja wa wana wa Shemu.
Jina Pelegi lina maana ya "mgawanyiko"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu wa duniani walijigawa wenyewe" au "watu wa duniani waligawanyika kati yao" au "Mungu aligawanya watu wa duniani"
Yoktani alikuwa mmoja wa wana wa kiume wa Eberi.
Hapa "hawa" ina maana ya wana wa kiume wa Yoktani.
"ardhi walioitawala" au "ardhi walipoishi"
Neno "hawa" ina maana ya vizazi vya Shemu.
Hii inarudi nyuma kwa watu wote waliorodheshwa katika 10:1
"imeorodheshwa kwa"
"kutoka kwa koo hizi mataifa yaligawanyika na kusambaa nchini kote" au "Koo hizi ziligawanyika baina yao na kuunda mataifa ya dunia"
Hii inaweza kuelezwa dhahiri au kwa uwazi zaidi. "baada ya gharika kuangamiza nchi"