Hii ni baraka ya Mungu. Alimwambia Nuhu pamoja na familia yake kuzaliana wanadamu wengine kama wao, ili kwamba wawe wengi wa aina yao. Neno "mkaongezeke" linafafanua jinsi gani wanapaswa "kuzaana"
Mwandishi anazungumzia hofu na utisho kana kwamba ni vitu vya mwili ambavyo vingeweza kuwa juu ya wanyama. "Kila mnyama hai ... na samaki wote wa baharini watakua na hofu kubwa sana juu yako"
maneno "hofu" na "utisho" zina maana moja na husisitiza jinsi wanyama walivyokuwa wanaogopa binadamu. "Hofu ya utisho kwako" au "Hofu ya kutisha kwako"
Hili ni moja kati ya makundi manne ya wanyama ambayo mwandishi ameorodhesha, na sio ufupisho wa wanyama waliosalia atakaowataja hapo baadae
Huu ni msemo wa jumla kwa vitu vinavyopaa. "wanyama warukao" au "vitu vinavyoruka"
Hii inajumuisha aina yote ya wanyama.
Mkono ni lugha mbadala kwa mamlaka ambayo mkono ulikuwa nayo. Hii inaweza kuwa katika hali ya kutenda. "Vimetolewa katika mamlaka yako" au "Nimeviweka chini ya mamlaka yako"
Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu pamoja na watoto wake.
"Damu ni alama ya uhai". "Mungu alikuwa akiwaamuru watu wasile nyama ambayo bado ina damu ndani yake. Walipaswa kutoa kwanza damu"
Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu pamoja na watoto wake.
Hii inatofautisha damu ya mwanadamu na damu ya wanyama
Inaonyesha ya kwamba damu imemwagwa, au imemwagika, au mwagikia. "iwapo yeyote atasababisha damu yako kumwagika" au "iwapo yeyote atamwaga damu yako" au "iwapo yeyote atakuua"
Hii ina maana ya uhai wa mwili.
Malipo haya yana maana kifo kwa yule muuaji, sio fedha. "Nitataka yeyote atakayekuua kulipa"
Hapa neno "mkono" lina maana ya yule mtu anayehusika na jambo kutendeka.
"Nitataka mnyama yeyote atakayetoa uhai wako kulipa"
"Nitataka mtut yeyote atakayetoa uhai wa mtu mwingine kulipa"
Msemo huu una maana ya mtu katika hali ya ukaribu sana. "Kutoka kwa mtu huyo kabisa"
Hapa "ndugu" inatumika kama kumbukumbu ya jumla kwa jamaa, kama wanajumuiya wa kabila moja, ukoo au kikundi cha watu.
Kumwaga kwa damu ni sitiari kwa ajili ya kuua mtu. Hii ina maanisha kama mtu atamuua mtu, mtu mwingine anapaswa kumuua muuaji. japokuwa, "damu" ina umuhimu sana katika kipengele hichi na inapaswa kutumiwa katika tafsiri ikiwezekana.
"kwa sababu Mungu aliumba watu wafanane na yeye" au "kwa sababu niliumba watu katika mfano wangu"
Hii ni baraka ya Mungu. Alimwambia Nuhu na familia yake kuzaa wanadamu wengine kama wao wenyewe, ili kusudi waweze kuwa wengi zaidi. Neno "kuongezeka" linafafanua jinsi ya wao "kuzaa"
Mungu alikuwa akizungumza nao tayari. Msemo huu unaweka alama ya mabadiliko juu ya kile Mungu alichokuwa akienda kukizungumzia. "Mungu aliendelea kuzungumza na Nuhu pamoja na watoto wake" au "Kisha Mungu akaendelea kusema"
Msemo huu unatumika kwa Kiingereza kuweka alama ya mabadiliko juu ya kile Mungu alichokuwa akizungumzia juu ya Nuhu na wanawe walichopaswa kufanya na kuzungumzia juu ya nini Mungu angefanya.
"fanya agano kati yako na mimi"
Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu na wanawe.
"kwa kusema hivi, ninafanya agano langu pamoja na wewe"
Maana zaweza kuwa 1) binadamu wote au 2) wenye viumbe wote, kujumlisha binadamu na wanyama.
"Hakutakuwa tena na gharika ambalo litaangamiza nchi". Kutakuwa na gharika, lakini hazitaangamiza dunia nzima.
Hii ina maana ya ukumbusho wa jambo lililoahidiwa.
Agano hili linamhusu Nuhu na familia yake na pia vizazi vyote vitakavyofuata.
Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu na wanawe.
"Itakapokuwa". Ni jambo ambalo hutokea mara nyingi.
Haipo wazi ni nani atauona upinde wa mvua, lakini kwa sababu agano upo kati ya Yahwe na watu, iwapo utataka kusema nani atauona upinde wa mvua, ni vyema kuwataja wote Yahwe na watu. Hii inaweza kutafsiriwa katika hali ya kutenda. "watu pamoja na mimi tunauona upinde wa mvua"
mstari wa rangi wenye mwanga unaojitokeza katika mvua ambapo jua hungaa kutoka nyuma ya mtazamaji.
Hii haimaanishi ya kwamba Mungu angesahau kwanza. "Nitafikiria juu ya agano langu"
Neno "ninyi" ni wingi. Mungu anazungumza na Nuhu na wana wa Nuhu.
"kila aina na kiumbe hai"
Maana zaweza kuwa 1) binadamu wote au 2) wenye viumbe wote wenye mwili, kujumlisha binadamu na wanyama.
Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu na wanawe.
"ili kwamba nikumbuke" au "ili kwamba nitafikiria juu ya"
Mungu anazungumza hapa. "kati yangu na kila kiumbe hai"
"kila aina ya kiumbe hai"
Mungu alikuwa tayari anazungumza na Nuhu. Msemo huu unaweka alama ya sehemu ya mwisho ya kile Mngu alichokuwa akisema. "Mungu alimalizia kwa kusema kwa Nuhu" au "Kwa hiyo Mungu akasema kwa Nuhu"
Mistari ya 18-19 inatambulisha wana watatu wa Nuhu, ambao watakuwa sehemu muhimu katika simulizi ifuatayo.
Hamu alikuwa baba wa Kaanani wa halisi.
"mtu wa ardhi"
"alikunywa divai nyingi sana"
Maandishi haisemi jinsi gani mwili wa Nuhu ulikuwa uchi alipokuwa amelala kalewa. Mapokeo ya wanawe yalionyesha ya kwamba ilikuwa suala la aibu.
Hii ina maana ya Nuhu.
Katika mistari ya 25-27 Nuhu anatamka laana juu ya mwana wa Hamu na baraka juu ya ndugu za hamu. Kile alichokisema Nuhu juu yao pia iliwahusu uzao wao.
Misemo tofauti katika mistari hii inakusudiwa kuonyesha ya kwamba hii ilikuwa shairi.
"akawa mtulivu"
Hii ina maana ya Hamu. "mwanawe mdogo, Hamu"
"Ninakulaani Kaanani" au "Na mambo mabaya yafanyike kwako Kaanani"
Huyu alikuwa mmoja wa wana wa Hamu. "mwana wa Hamu Kaanani"
"mtumishi wa chini wa kaka zake" au "mtumishi mwenye umuhimu wa chini kabisa kati ya ndugu zake"
Hii inaweza kumaanisha ndugu zake Kaanani au ndugu zake kwa ujumla.
Hii ni shairi.
"Yahwe na asifiwe, Mungu wa Shemu" au "Yahwe, Mungu wa Shemu, anastahili sifa" au "Ninamsifu Yahwe, Mungu wa Shemu"
"Na Kaanani awe mtumishi wa Shemu". Hii inajumlisha uzao wa Kaanani na Shemu.
Maana zaweza kuwa 1) "Mungu na afanya mipaka ya Yafethi mikubwa" au 2) "Mungu na asababishe Yafethi kuwa na uzao mwingi"
"na mfanye aishi kwa amani na Shemu". Hii inajumlisha uzao wa Yafethi na Shemu.
"Na Kaanani awe mtumishi wa Yafethi". Hii inajumlisha uzao wa Kaanani na Yafethi.