Genesis 5

Genesis 5:1

Taarifa ya jumla:

Huu ni mwanzo wa orodha ya uzao wa Adamu.

katika mfano

Msemo huu unamaanisha ya kwamba Mungu aliumba binadamu amfanane yeye. Mstari huu hausemi ni kwa namna gani Mungu aliumba wanadamu wawe kama yeye. Mungu hana mwili, kwa hiyo haimaanishi watu wangekuwa kama Mungu. "kuwa kama sisi"

walipoumbwa

Hii inaweza kufanywa katika hali ya kutenda. "alipowaumba"

Genesis 5:3

130 ... mia nane

Watafsiri wanaweza kuandika tarakimu "130" na "800" au maneno "mia moja na thelathini" na "mia nane".

akamzaa mwana katika sura yake

"akamzaa mwana wa kiume"

katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake

Misemo hii miwili inamaana moja. Inatumika kama kumbukumbu ya kwamba Mungu alimuumba binadamu katika mfano wake.

Sethi

Sethi

Akawazaa wana wengi waume na wake

"Akawa na wana zaidi wa kiume na kike"

kisha akafariki

Msemo huu utarudiwa katika sura yote. "Kisha akaafa"

Adamu akaishi miaka 930

Watu walikuwa wakiishi muda mrefu sana. "Adamu aliishi jumla ya miaka 930"

Genesis 5:6

akawa baba wa Enoshi

Hapa "baba" inamaana ya baba mzazi, na sio babu. "akamzaa mwana wake wa kiume Enoshi"

Enoshi

Hili ni jina la mtu

naye akawa baba wa wana wengi waume na wake

"na akawa na wana zaidi wa kiume na kike"

Sethi akaishi miaka 912

"Sethi aliishi jumla ya miaka 912"

kisha akafariki

"Kisha akafa"

Genesis 5:9

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:12

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:15

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:18

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:21

akawa baba wa Methusela

"akapata mwana wake wa kiume Methusela"

Methusela

Hili ni jina la mwanamume

Henoko akaenenda na Mungu

Kuenenda na mtu ni sitiari ya kuwa na uhusiano wa karibu na yeye. "Henoko alikuwa na uhusiano wa karibu na Mungu" au "Henoko aliishi kwa umoja na Mungu"

Akawa baba wa wana zaidi wa kiume na kike

"Akawa na wana zaidi wa kiume na kike"

Henoko aliishi miaka 365

"Henoko aliishi jumla ya miaka 365"

kisha alitoweka

Neno "alitoweka" linamaanisha Henoko. Hakuwa duniani tena.

kwa kuwa Mungu alimtwaa

Hii inamaana Mungu alimtwaa Henoko awe naye.

Genesis 5:25

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Lameki

Lameki huyu ni tofauti na Lameki wa 4:18

Genesis 5:28

akawa baba wa mwana wa kiume

"akapata mwana wa kiume"

Nuhu

Jina hili linafanana na jina la Kiyahudi lenye maana ya "pumziko".

katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu

Lameki anasema jambo hilo hilo mara mbili kusisitiza jinsi kazi ilivyo ngumu. "kwa kufanya kazi sana kwa mikono yetu"

Genesis 5:30

Lameki aliishi miaka 595

"Lameki aliishi jumla ya miaka ya 777"

Genesis 5:32

akawa baba wa

"akazaa watoto wake wa kiume". Hii haituambii kama wana wa kiume walizaliwa katika siku moja au mika tofauti.

Shemu, Hamu, na Yafethi

Yawezekana wana hawa wa kiume hawajaorodheshwa kufuata kuzaliwa kwao. Kuna mjadala kuhusu nani alikuwa mkubwa. Epuka kutafsiri haya majina na kuonyesha ya kwamba orodha ipo katika mpangilio wa umri wao.