Genesis 4

Genesis 4:1

Mwanume

"binadamu" au "Adamu"

akalala na

"akamjua"

nimezaa mwanaume

Neno la "mwanamume" linamuelezea binadamu wa kiume, tofauti na mtoto mchanga au kijana. Kama hiyo italeta kuchanganya, inaweza kutafsiriwa kama "kijana wa kiume" au "mvulana" au "mtoto mchanga wa kiume" au "

Kaini

Watafsiri wanaweza kuweka taarifa fupi ambayo inasema "Jina la Kaini linafanana na neno la Kiebrania linalmaanisha "zaa". Hawa alimuita Kaini kwa sababu alimzaa.

Kisha akazaa

Hatujui ni muda gani ulipita katikati ya kuzaliwa kwa Kaini na Habili. Yawezekana walikuwa mapacha, au Habili alizaliwa baada ya Hawa kupata mimba tena. Kama

alilima

Hii ina maana alifanya kila kitu alichopaswa kufanya ili kwamba mimea iweze kuota vizuri.

Genesis 4:3

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi. Kama lugha yakoin njia ya kufanya hivi, basi tumia njia hii.

baada ya muda

Maana yake yaweza kuwa 1) "baada ya muda kupita" au 2) "kwa muda sahihi"

mazao ya ardhi

Hii inamaanisha chakula kilichotoka kwa mimea aliyoitunza."mazao" au "mavuno"

sehemu zilizonona

Hii inamaanisha sehemu zilizonona za kondoo alizoua, ilikuwa ni sehemu bora zaidi ya mnyama. "baadhi ya sehemu zao zilizonona"

akamkubali

"alipendezwa naye" au "alifurahishwa naye"

alikasirika sana

Baadhi la lugha zina lahaja kwa neno hasira kama "aliwaka" au "hasira yake iliwaka".

ukakunjamana

Hii ina maana muonekano wa uso wake ulionyesha ya kuwa alikuwa amekasirika au ana wivu. Baadhi ya lugha zina lugha ambayo inaelezea sura inavyoonekana anapokuwa na hasira.

Genesis 4:6

kwa nini umekasirika na kwa nini uso wako umekunjamana?

Mungu alitumia maswali haya la balagha kumwambia Kaini ya kwamba hakuwa sahihi kuwa na hasira na kukunjamana sura. Yawezekana yalitumika kumpatia Kaini nafasi ya kutubu makosa yake.

Kama ... je hutapata kibali?

Mungu alitumia swali hili la balagha kumkumbusha Kaini juu ya jambo ambalo Kaini alipaswa kulifahamu. "Unajua ya kwamba ukifanya lilio sahihi, nitakukubali"

lakini kama hutafanya ... inakupasa uishinde

Mungu anazungumzia dhambi kana kwamba ni binadamu. "Lakini kama hutafanya kilicho sahihi, utatamani kufanya dhambi zaidi, na kisha utatenda matendo ya dhambi. Unatakiwa kukataa kuitii"

dhambi iko inakuotea ... kukutawala

Hapa dhambi inazungumziwa kama mnyama mwitu hatari anayesubiri nafasi ya kumshambulia Kaini. "utakuwa na hasira sana utashindwa kuizuia dhambi"

dhambi

Lugha ambazo hazina nomino yenye maana ya "dhambi" zaweza kutafsiri hii kama "tamaa yako kutenda dhambi" au "mambo mabaya unayotaka kufanya".

inakupasa uishinde

Yahwe anazungumzia tamaa ya Kaini kutenda dhambi kana kwamba ni mtu ambaye Kaini anapaswa kumtawala. "unapaswa kuitawala ili usitende dhambi"

Genesis 4:8

Kaini akamwambia Habili ndugu yake

Baadhi ya lugha zinahitaji kuongeza taarifa inayojitokeza ya kwamba Kaini alizungumza na ndugu yake kuhusu kwenda mashambani.

ndugu

Habili alikuwa ndugu yake Kaini. Baadhi ya lugha zinaweza kutumia neno kwa ajili ya "ndugu mdogo"

aliinuka dhidi

"alimshambulia"

Ndugu yako Habili yuko wapi?

Mungu alijua ya kwamba Kaini alimuua Habili, lakini alimuuliza Kaini swali hili ili Kaini aweze kujibu.

Je mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?

Kaini alitumia swali hili la balaghaili kukwepa kusema ukweli. Hii yaweza kutafsiriwa katika msemo. "Mimi sio mlinzi wa ndugu yangu!" au "Kumtunza ndugu yangu sio kazi yangu!"

Genesis 4:10

umefanya nini?

Mungu alitumia swali la balagha kumkaripia Kaini. Hii yaweza kutafsiriwa kama msemo. "Ulichofanya ni kibaya"

damu ya ndugu yako inaniita mimi

Damu ya Habili ni lugha kwa ajili ya kifo chake, kana kwamba ni mtu anayemwita Mungu kumuadhibu Kaini. "Damu ya ndugu yako ni kama mtu akiniita kumuadhibu yule aliyemuua"

sasa umelaaniwa wewe kutoka ardhini

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Ninakulaani ili usiweze kuotesha chakula kutoka ardhini"

ambayo imefungua kinywa chake kupokea damu ya ndugu yako

Mungu anazungumzia ardhi kana kwamba ni mtu awezaye kunywa damu ya Habili. "ambayo imelowa kwa damu ya ndugu yako"

kutoka mikononi mwako

Mungu anazungumzia mkono wa Kaini kana kwamba umemwaga damu ya Habili katika "mdomo" wa ardhi. "iliyomwagwa ulipomuua" au "kutoka kwako"

ilima

Hii inamaanisha kufanya kila liwezekanalo ili mimea iweze kuota vizuri.

haita kuzalia wewe nguvu yake

Ardhi inapewa utu kana kwamba ni binadamu anayepoteza nguvu. "ardhi haitakuzalia chakula cha kutosha kwa ajili yako"

mkimbizi na mtu asiye na makao

Unaweza kuunganisha maneno haya pamoja. "mkimbizi asiye na makao"

Genesis 4:13

sitaonekana mbele ya uso wako

Msemo wa "uso wako" unawakilisha uwepo wa Mungu. "Sitaweza kuzungumza na wewe"

mkimbizi na mtu nisiye na makao

mtu asiye na makao

kisasi kitakuwa juu yake mara saba

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitachukua kisasi juu yake mara saba" au "Nitamuadhibu mtu yule mara saba kwa ukali kama navyokuadhibu"

asimshambulie

"hatamuua Kaini"

Genesis 4:16

akatoka mbele ya uwepo wa Yahwe

Ingawa Yahwe yupo kila mahali, lahaja hii inamzungumzia Kaini kana kwamba alienda mbali sana. "aliondoka kutoka mahali ambapo Yahwe alizungumza naye"

Nodi

Neno Nodi linamaana ya "mkimbizi"

akamjua

akamjua

Akajenga mji

"Kaini akajenga mji"

Genesis 4:18

Kwa Henoko akazaliwa Iradi

Inasemekana ya kwamba Henoko alikuwa na kuoa mwanamke. "Henoko alikua na kuoa na akawa baba kwa mtoto ambaye alimuita Iradi"

Iradi akamzaa Mehuyaeli

"Iradi alipata mtoto na kumuita Mehuyaeli"

Ada ... Sila

majina ya wanawake

Genesis 4:20

Ada ... Sila

majina ya wanawake

alikuwa baba yao na wale walioishi hemani

Maana yake yaweza kuwa 1) "Alikuwa binadamu wa kwanza kuishi hemani" au 2) "Yeye na uzao wake waliishi hemani"

walioishi hemani ambao wanafuga wanyama

watu wanaoishi hemani na kufuga wanyama

alikuwa baba yao na wale wapigao kinubi na filimbi

Maana yake yaweza kuwa 1) "Alikuwa mtu wa kwanza kupiga kinubi na filimbi" au 2) "Yeye na uzao wake walipiga kinubi na filimbi".

Tubal Kaini, mfua vyombo vya shaba na chuma

"Yubal Kaini. alitengeneza vyombo vya shaba na chuma"

chuma

Hii ni metali yenye nguvu sana iliyotumika kutengeneza vyombo, vifaa na silaha.

Genesis 4:23

Ada .. Sila

majina ya wanawake

sikieni sauti yangu ... sikilizeni nisemacho

lameki alisema jambo moja mara mbili kuonyesha msisitizo. Sauti yake ni lugha nyingine kwa utu wake wote. "nisikilizeni kwa makini"

mtu ... kijana

Lameki alimuua mtu mmoja tu

kwa kunijeruhi ... kwa kunichubua

"kwa sababu alinijeruhi ... kwa sababi alinichubua" au "kwa sababu aliniumiza"

Ikiwa Kaini atalipiwa kisasi mara saba, ndipo Lameki

Lameki anajua ya kwamba Mungu atalipa kisasi kwa ajili ya Kaini mara saba. "Kwa maana Mungu atamuadhibu yeyote atakayemuua Kaini mara saba, Lameki"

ndipo Lameki atalipiwa kisasi mara sabini na saba

mara saba** - Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "yeyote atakayeniua, Mungu atamuadhibu mara sabini na saba"

sabini na saba

saba** - 77

Genesis 4:25

akamjua

akamjua

na akasema, " Mungu amenipatia mtoto mwingine wa kiume

Hii ni sababu ya yeye kumuita Sethi. Hii inaweza kuwekwa dhahiri. "na ikaeleza, 'Mungu amenipa mtoto mwingine'"

Sethi

Hili jina linaonekana kama neno la Kiyahudi lenye maana ya "amenipatia"

Mtoto wa kiume alizaliwa kwa Seth

Hii inaweza kuwekwa dhahiri. "mke wa Sethi alimzalia mtoto wa kiume"

kuliitia jina la Yahwe

Hii ni mara ya kwanza watu wanamuita Mungu kwa jina la Yahwe. Hii inaweza kuwekwa dhahiri. "kumuabudu Mungu kwa kutumia jina la Yahwe"