Genesis 48

Genesis 48:1

Yusufu aliskia ujumbe gani kuhusu baba yake, na kisha alifanya nini?

Yusufu alisikia ya kuwa baba yake alikuwa mgonjwa, kwa hiyo akachukua wanawe wawili.

Genesis 48:3

Yakobo alimkumbusha Yusufu ahadi gani kutoka kwa Mungu?

Yakobo alimkumbusha ya kwamba Mungu alimuahidi kuongezeka na kuzaana, atakuwa kusanyiko la mataifa, na nchi ya Kaanani itakuwa milki ya milele kwa uzao wake.

Genesis 48:5

Yakobo alisema angewafikiriaje wana wawili wa Yusufu katika urithi?

Yakobo alisema angewafikiria wana wawili wa Yusufu kama wanawe.

Genesis 48:8

Kwa nini Israeli hakutambua wana wa Yusufu?

Israeli hakuwatambua wana wa Yusufu kwa sababu macho yake yalikuwa yanashindwa kwa sababu ya umri wake.

Genesis 48:14

Nani alikuwa mwana wa kwanza wa Yusufu?

Manase alikuwa mwana wa kwanza wa wana wa Yusufu.

Israeli aliweka mkono wake wa kulia juu ya nani, na wa kushoto kwa nani?

Israeli aliweka mkono wake wa kulia juu ya Efraimu, na wa kushoto kwa Manase.

Genesis 48:17

Kwa nini Yusufu alijaribu kubadili nafasi ya mikono ya Israeli?

Yusufu alitegemea mkono wa kulia wa Israeli kuwa juu ya Manase kwa sababu alikuwa mzaliwa wa kwanza.

Genesis 48:19

Kwa nini Israeli alikataa kubadili nafasi ya mikono yake juu ya wana wawili wa Yusufu?

Israeli alikataa kwa sababu ndugu mdogo angekuwa mkubwa kuliko mzaliwa wa kwanza.

Israeli alisema watu wa Israeli watatamka baraka gani?

Israeli alisema watu wa Israeli watatamka baraka ya, "Mungu na akufanye kama Efrahimu na kama Manase"

Genesis 48:21

Israeli alisema nini kingetokea kwa Yusufu?

Israeli alisema ya kwamba Yusufu atarudishwa katika nchi ya baba zake.