Genesis 47

Genesis 47:3

Ndugu watano wa Yusufu walimwambia Farao kazi yao ilikuwa ipi?

Ndugu watano walimwambia Farao kazi yao ilikuwa ufugaji.

Ndugu walisema wao walikuwa wakazi wa aina gani katika nchi ya Misri?

Ndugu walisema walikuwa wakazi wa muda katika nchi ya Misri.

Genesis 47:5

Farao alimwambia nini Yusufu kufanya na familia ya Yusufu?

Farao alimwambia Yusufu kuwaweka familia ya Yusufu katika sehemu nzuri, nchi ya Gosheni.

Genesis 47:7

Yakobo alifanya nini kwa Farao alipokutana naye na alipotoka katika uwepo wake?

Yakobo alimbariki Farao alipokutana naye na alipotoka katika uwepo wake.

Yakobo alikuwa ameishi muda gani alipokutana na Farao?

Yakobo aliishi miaka mia moja na thelathini.

Yakobo alisema maisha yake yalikuaje kulinganisha na baba zake?

Yakobo alisema maisha yake hayakuwa marefu kama maisha ya baba zake.

Genesis 47:13

Yusufu aliweza kufanya nini kwa kuuza nafaka?

Yusufu aliweza kukusanya pesa yote katika nchi ya Misri na katika nchi ya Kaanani.

Genesis 47:15

Yusufu kisha aliweza kufanya nini kwa kubadilishana chakula na Wamisri?

Yusufu aliweza kubadili chakula kwa wanyama wote wa Wamisri.

Genesis 47:18

Baada ya pesa na wanyama kuwa wametolewa kwa Farao kwa kubadilisha na chakula watu wa Misri walitoa nini kama kubadilisha kwa chakula zaidi?

Watu wa Misri walitoa ardhi zao na wao wenyewe kama watumishi wa Farao kwa kubadilishana kwa chakula zaidi.

Genesis 47:23

Yusufu alihitaji sehemu gani ya mavuno yote kupewa kwa Farao?

Yusufu alihitaji moja ya tano ya mavuno iweze kupatiwa Farao.

Genesis 47:27

Kwa njia zipi watu wa Israeli walifanikiwa katika nchi ya Misri?

Watu wa Israeli walipata mali katika nchi ya Misri, na waliongezeka na kuzaana kwa wingi.

Yakobo alikufa katika umri gani?

Yakobo alifariki katika umri wa miaka mia moja na arobaini na saba.

Genesis 47:29

Israeli alimwomba Yusufu aape kufanya nini?

Israeli alimwomba Yusufu kuapa ya kuwa atabeba mifupa ya Israeli katika eneo la baba zake.