Genesis 46

Genesis 46:1

Israeli alifanya nini Beersheba?

Israeli alitoa sadaza kwa Mungu wa baba yake Isaka.

Mungu alitoa ahadi gani kwa Israeli kule Beersheba?

Mungu aliahidi kumfanya Israeli kuwa taifa kubwa, na kwenda na Israeli Misri, na kumleta tena Israeli kutoka Misri, na kumfanya Yusufu afunike macho yake.

Genesis 46:5

Ni nani alikwenda Misri na Israeli?

Israeli na vizazi vyake vyote walikwenda Misri.

Genesis 46:12

Wana gani wa Yuda walikufa katika nchi ya Kaanani?

Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kaanani.

Genesis 46:26

Watu wangapi wa nyumba ya Yakobo walikuja Misri?

Watu sabini wa nyumba ya Yakobo walikuja Misri.

Genesis 46:28

Yusufu alifanya nini kukutana na baba yake?

Yusufu alikwenda na kibandawazi chake na kukutana na baba yake Israeli Gosheni.

Yusufu alifanya nini alipomwona baba yake?

Yusufu alimkumbatia shingo ya baba yake na kulia kwa muda mrefu.

Genesis 46:33

Yusufu aliwaambia nini ndugu zake kusema kwa Farao kuhusu kazi yao?

Ndugu walitakiwa kumwambia Farao ya kuwa walikuwa wafugaji wa mifugo tangu ujana wao.