Genesis 49

Genesis 49:1

Kwa nini Yakobo alikusanya wanawe pamoja?

Yakobo alikusanya wanawe pamoja kuwaambia nini kingetokea kwao na vizazi vya vya baadae.

Genesis 49:3

Rubeni alikuwa ni sifa gani nzuri?

Rubeni alikuwa aliyesalia mwenye heshima na nguvu.

Kwa nini Rubeni hangekuwa na umaarufu ingawa alikuwa mzawa wa kwanza?

Rubeni hangekuwa na umaarufu kwa sababu alinajisi kitanda cha baba yake.

Genesis 49:7

Yakobo alilaani nini juu ya Simoni na Lawi?

Yakobo alilaani ukali na hasira ya ukatili ya Simoni na Lawi.

Genesis 49:8

Yakobo alisema wanawe wengine watafanya nini mbele ya Yuda?

Yakobo alisema wanawe wengine watainama chini mbele ya Yuda.

Genesis 49:10

Ahadi gani kuhusu miaka ya baadae ilifanya kwa Yuda?

Yuda aliahidiwa ya kwamba fimbo ya utawala haitatoka kutoka kwake hadi Shilo atakapokuja, na kwamba mataifa watamtii yeye.

Genesis 49:13

Yakobo alisema vizazi vya Zebuloni vitaishi wapi?

Yakobo alisema vizazi vya Zebulono vitaishi katika fukwe ya bahari.

Genesis 49:16

Yakobo alisema Dani atakuwa kama mnyama gani?

Yakobo alisema Dani angekuwa kama nyoka mwenye sumu.

Genesis 49:19

Yakobo alisema Asheri atajulikana kwa jambo gani?

Yakobo alisema Asheri atajulikana kwa kutoa vyakula vya kifalme.

Genesis 49:22

Yakobo alisema Yusufu angekuwa kama aina gani la mmea?

Yakobo alisema Yusufu angekuwa kama tawi lizaalo ambaye matawi yake hupanda juu ya ukuta.

Genesis 49:24

Yakobo alisema ni nani angetunza upinde wa Yusufu imara na mikono yake hodari?

Yakobo alisema mikono ya mwenye nguvu wa Yakobo, Mwamba wa Israeli atatunza upinde wa Yusufu imara na mikono yake hodari.

Genesis 49:31

Ni nani aliyekuwa amezekwa katika sehemu ambayo Yakobo alitamani kuzikwa?

Abrahamu, Sara, Isaka, Rebeka, na Lea walikuwa wamezikwa kule.

Yakobo alifanya nini baada ya kutoa baraka zake na maelekezo kwa wanawe?

Yakobo alipumua pumzi yake ya mwisho na kwenda kwa watu wake.