Njaa ilikuwa kali sana na walikuwa wamekula nafaka waliokuwa wamenunua kutoka Misri katika safari ya kwanza.
Yuda alisema ni lazima wawe na ndugu yao Benyamini ili kushuka Misri.
Yuda alisema ya kwamba asipomrudisha Benyamini, angebeba lawama milele.
Israeli aliwaambia ndugu kuchukua baadhi ya bidhaa za ardhi, na kubeba mara mbili ya pesa.
Israeli alimwomba Mungu kuwapa ndugu neema kule Misri, ili kwamba ndugu wote waweze kuachiwa.
Ndugu waliogopa wangekamatwa na kuchukuliwa kama watumwa kwa sababu ya pesa ndani ya magunia yao katika safari ya kwanza.
Ndugu walimwambia mtunzaji wa nyumba kuwa wameleta pesa iliyoachwa katika magunia yao, na pesa kwa ajili ya kununua chakula.
Mtunzaji wa nyumba alisema pesa iliyoachwa katika magunia yao ilitoka kwa Mungu wao.
Ndugu walileta zawadi katika nyumba, na kuinama chini mbele ya Yusufu hata chini.
Yusufu aliwauliza ndugu kuhusu hali ya baba yao.
Yusufu aliharakisha kutoka chumbani kwa sababu aliguswa sana kuhusu Benyamini, na alikwenda chumbani kwake kulia.
Ilikuwa chukizo kwa Wamisri kula na Waebrania.
Ndugu walipangwa katika meza kulingana na haki yao ya kuzaliwa na umri.
Sehemu ya Benyamini ilikuwa mara tano zaidi ya yeyote wa ndugu zake.