Genesis 43

Genesis 43:1

Kwa nini Israeli aliwaambia wanawe kurudi tena na kununua chakula Misri?

Njaa ilikuwa kali sana na walikuwa wamekula nafaka waliokuwa wamenunua kutoka Misri katika safari ya kwanza.

Genesis 43:3

Yuda alisema ni lazima wawe na nini ili kwenda Misri tena?

Yuda alisema ni lazima wawe na ndugu yao Benyamini ili kushuka Misri.

Genesis 43:8

Ni kiapo gani alichofanya Yuda kwa baba yake Israeli?

Yuda alisema ya kwamba asipomrudisha Benyamini, angebeba lawama milele.

Genesis 43:11

Israeli aliwaambia nini ndugu kubeba nacho kwenda Misri?

Israeli aliwaambia ndugu kuchukua baadhi ya bidhaa za ardhi, na kubeba mara mbili ya pesa.

Genesis 43:13

Israeli alimwomba Mungu juu ya nini kuhusu safari hii?

Israeli alimwomba Mungu kuwapa ndugu neema kule Misri, ili kwamba ndugu wote waweze kuachiwa.

Genesis 43:18

Ndugu walichukuliaje walipochukuliwa katika nyumba ya Yusufu, na kwa nini?

Ndugu waliogopa wangekamatwa na kuchukuliwa kama watumwa kwa sababu ya pesa ndani ya magunia yao katika safari ya kwanza.

Genesis 43:21

Ndugu walimwambia nini mtunzaji wa nyumba wa nyumba ya Yusufu?

Ndugu walimwambia mtunzaji wa nyumba kuwa wameleta pesa iliyoachwa katika magunia yao, na pesa kwa ajili ya kununua chakula.

Mtunzaji wa nyumba alisema pesa iliyoachwa katika magunia yao ilitoka wapi?

Mtunzaji wa nyumba alisema pesa iliyoachwa katika magunia yao ilitoka kwa Mungu wao.

Genesis 43:26

Ndugu walifanya nini Yusufu alipokuja nyumbani?

Ndugu walileta zawadi katika nyumba, na kuinama chini mbele ya Yusufu hata chini.

Yusufu aliwauliza ndugu kuhusu nani?

Yusufu aliwauliza ndugu kuhusu hali ya baba yao.

Genesis 43:30

Kwa nini Yusufu aliharakisha kutoka chumbani, na alifanya nini baada ya kuondoka?

Yusufu aliharakisha kutoka chumbani kwa sababu aliguswa sana kuhusu Benyamini, na alikwenda chumbani kwake kulia.

Genesis 43:32

Kwa nini Wamisri na Waebrania walikula mahali tofauti?

Ilikuwa chukizo kwa Wamisri kula na Waebrania.

Ndugu walipangwa kwa namna gani katika meza?

Ndugu walipangwa katika meza kulingana na haki yao ya kuzaliwa na umri.

Kipi hakikuwa kawaida kuhusu kiasi cha chakula ndugu walichopewa?

Sehemu ya Benyamini ilikuwa mara tano zaidi ya yeyote wa ndugu zake.