Yusufu alimwambia mtunzaji wake wa nyumba kujaza magunia ya ndugu zake na chakula, na kuweka pesa yao ndani ya magunia, na kuweka kikombe chake cha fedha katika gunia la mdogo.
Yusufu alimwambia mtunzaji wa nyumba kuwauliza kwa nini walirudisha uovu kwa wema na kuwashtaki kuiba kikombe cha Yusufu.
Ndugu walisema mtu atakayekutwa na kikombe afe, na wengine wawe watumwa.
mtunzaji wa nyumba alisema ya kwamba yule ambaye kikombe kitakutwa naye atakuwa mtumwa wake, na wengine watakuwa hawana hatia.
mtunzaji wa nyumba alikuta kikombe katika gunia la Benyamini na ndugu zake wakararua nguo zao.
Ndugu waliinama chini mbele ya Yusufu hadi chini.
Yuda alisema ya kwamba Mungu aligundua dhambi yao.
Yuda alisema ndugu wote sasa watakuwa watumwa wa Yusufu.
Yusufu alisema ya kwamba mtu ambaye mkono ulikuwa na kikombe atakuwa mtumwa wake, na wengine wangeondoka kwa amani.
Yuda alisema ya kwamba ndugu yao mdogo alikuwa mtoto wa baba yake wa uzeeni, na mtoto pekee aliyebaki kwa mama yake.
Ndugu walikuwa na mashaka baba yao angekufa kama mdogo wao angemuacha.
Yuda alisema walilazimika kumleta Benyamini kwa sababu Yusufu alisema hadi pale ndugu yao mdogo aje, wasingeuona uso wa Yusufu.
Israeli alidhani ya kuwa hakika Yusufu aliraruliwa katika vipande.
Israeli alisema ya kwa ndugu wangeletea mvi kwa majonzi hadi kaburini.
Yuda alisema ya kwamba baba yake angekufa.
Yuda alisema ya kwamba kama hatamrudisha Benyamini kwa baba yake, atabeba hatia milele.
Yuda alimwomba Yusufu kumfanya awe mtumwa wa Yusufu, ili kwamba Benyamini aweze kurudi kwa baba yake.