Ndugu kumi wa Yusufu, bila Benyamini, walikwenda Misri kununua mazao.
Ndugu wa Yusufu waliinama chini kwake nyuso zao kuelekea ardhini.
Yusufu alijibadili na kuongea kwa ukali na ndugu zake.
Yusufu aliwashtaki ndugu zake kuwa wapelelezi.
Ndugu zake Yusufu walisema ndugu yao mdogo alikuwa na baba yao katika nchi ya Kaanani.
Ndugu zake Yusufu walisema ndugu yao aliyepotea hakuwa hai tena.
Yusufu alisema ndugu zake hawataondoka Misri, hadi pale ndugu yao mdogo aje Misri.
Yusufu aliwaweka ndugu zake kifungoni kwa siku tatu.
Yusufu aliwaambia kuruhusu mmoja wa ndugu kuwekwa gerezani, wakati wengine wakichukua mazao hadi Kaanani na kumleta ndugu yao mdogo.
Waliamini ya kwamba damu ya Yusufu ilidaiwa kwao kwa kile walichofanya kwa Yusufu.
Yusufu aliposikia ndugu zake wakizungumza kuhusu kile walichofanya kwake, Yusufu akatoka kwao na kulia.
Yusufu alirudihsa pesa ya kila ndugu ndani ya gunia lake.
Mioyo yao ilizimia na wakasemeshana kati yao wakitetemeka.
Ndugu walimlaumu Mungu, wakiuliza kwa nini Mungu alifanya hivi kwao.
Waligundua ya kwamba pesa ya kila mtu ilikuwa ndani ya gunia lake.
Yakobo aliogopa ya kwamba Simoni na Benyamini watachukuliwa kutoka kwake.
Rubeni aliapa kumrudisha benyamini kwa Yakobo kutoka Misri; la sivyo watoto wawili wa Rubeni wanaweza kuuwawa.
Hapana, Yakobo hakumruhusu Rubeni kumpeleka Benyamini Misri.
Yakobo alisema ya kuwa angeshuka na majonzi kaburini kama Benyamini angekufa.