Genesis 38

Genesis 38:1

YUda alichukua mke kutoka kwa nani?

YUda alichukua mke kutoka mtu wa Kaanani.

Genesis 38:6

Yahwe alifanya nini na mwana wa kwanza wa Yuda, na kwa nini?

Yahwe alimuua Eri kwa sababu alikuwa muovu.

Genesis 38:8

Ni kwa namna gani mwana wa Onani wa pili hakutimiza wajibu wa shemeji wa kumpatia mtoto Eri?

Onani alimwaga mbegu zake juu ya ardhi alipolala na Tamari.

Yahwe alifanya nini na mwana wa Yuda wa pili Onani, na kwa nini?

Yahwe alimuua Onani kwa sababu alichofanya kilikuwa kiovu.

Genesis 38:11

Yuda kisha alitoa ahadi gani kwa Tamari?

Yuda alimuahidi Tamari mwanawe wa tatu Shela kuwa mumewe pale Shela atakapokua.

Genesis 38:12

Baada ya muda mrefu, kwa nini Yuda alitakiwa kufarijiwa?

Yuda alifarijiwa kwa sababu mke wake alifariki.

Tamari alifanya nini aliposikia ya kwamba Yuda alikuwa akielekea Timna?

Tamari alivua nguo zake za kijane, na kuvaa shela na kujifunika, na kukaa njiani kwenda Timna.

Kwa nini Tamari alifanya hivi?

Tamari alifanya hivi kwa sababu mwana wa Yuda wa tatu Shela alikua, lakini hakupewa kwake kama mke.

Genesis 38:17

Tamari alichukua nini kama rehani kwa malipo kabla Yuda hajalala naye?

Yuda alimpatia Tamari mhuri wake, mshipi, na fimbo kama rehani ya malipo.

Genesis 38:21

Yuda alipojaribu kurejesha rehani yake kwa kumlipa kahaba kwa mbuzi mdogo, alijifunza nini?

Yuda alijifunza ya kwamba hapakuwa na kahaba wa hekalu katika eneo lile.

Genesis 38:24

Yuda alitaka kufanya nini aligundua ya kwamba Tamari alikuwa mimba?

Yuda alitaka kumchoma Tamari kwa sababu alipata mimba kwa njia ya ukahaba.

Tamari alifanya nini alipoletwa nje kwa Yuda?

Alisema ya kwamba alipata mimba kwa mwanamume aliyemiliki mhuri, mshipi na fimbo alizokuwa nazo.

Yuda alijibuje alipoona mhuri, mshipi na fimbo yake?

Yuda alisema ya kwamba Tamari alikuwa mwenye haki kuliko yeye, kwa sababu hakumpatia Tamari kwa Shela awe mke wake.

Genesis 38:27

Tamari alizaa watoto wangapi?

Tamari alipata mapacha.

Mkunga alifanya nini pale mmoja wa mapacha wa Tamari alipotoa mkono wake nje mwa tumbo la Tamari?

Pale ambapo mmoja wa mapacha wa Tamari alipotoa mkono wake nje ya tumbo la Tamari, mkunga alichukua kamba ya rangi ya zambarau na kufunga mkononi mwake na kusema, "Huyu ametoka wa kwanza".