Genesis 37

Genesis 37:1

Yakobo alikaa na kuishi wapi?

Yakobo aliishi katika nchi ya Kaanani.

Yusufu alileta nini kwa baba yake Yakobo alipochunga mifugo na ndugu zake?

Yakobo alileta taarifa mbaya kuhusu ndugu zake kwa baba yake.

Genesis 37:3

Israeli alionyeshaje ya kwamba anampenda Yusufu kuliko wanawe wengine?

Israeli alimshonea Yusufu vazi zuri.

Ndugu zake Yusufu walifikiri nini kuhusu Yusufu?

Ndugu zake Yusufu walimchukia na hawakuweza kuongea naye vyema.

Genesis 37:7

Yusufu aliona nini katika ndoto yake ya kwanza?

Yusufu aliona mganda umesimama wima wakati za ndugu zake zimeinama kwa mganda wake.

Ndugu zake na Yusufu walifikiri nini kuhusu Yusufu baada ya kuwaambia juu ya ndoto yake ya kwanza?

Ndugu zake Yusufu walimchukia tena zaidi.

Genesis 37:9

Yusufu aliona nini katika ndoto yake ya pili?

Yusufu aliona jua, mwezi, na nyota kumi na moja zikiinama chini kwake.

Katika ndoto ya pili ya Yusufu, jua, mwezi na nyota ziliwakilisha nini?

Jua, mwezi, na nyota ziliwakilisha baba, mama na kaka zake Yusufu

Genesis 37:12

Yakobo alimtuma Yusufu katika bonde la Hebroni kufanya nini?

Yakobo alimtuma Yusufu katika bonde la Hebroni kuona kama ndugu zake wako salama, na kuleta taarifa kwa Yakobo.

Genesis 37:18

Ndugu zake Yusufu walipanga kufanya nini walipomuona Yusufu akija?

Ndugu zake Yusufu walipanga kumuua Yusufu na kumtupa katika moja ya mashimo.

Genesis 37:21

Rubeni alitoa ushauri gani kwa ndugu zake, na kwa nini?

Rubeni alishauri ya kwamba ndugu wamtupe tu Yusufu katika shimo, ili kwamba aweze kumuokoa Yusufu baadae.

Genesis 37:27

Ndugu zake Yusufu walimuuza kwa nani na kwa kiasi gani?

Ndugu zake Yusufu walimuuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande ishiri vya fedha.

Yusufu alipelekwa wapi?

Yusufu alipelekwa Misri.

Genesis 37:31

Ndugu zake Yusufu walifanyaje ili ionekane kuwa Yusufu alikufa?

Ndugu zake Yusufu waliua mbuzi na kuchovya vazi la Yusufu ndani ya damu, na kumpatia Yakobo vazi hilo.

Genesis 37:34

Yakobo alifanya nini aliporidhia Yusufu alikufa?

Yakobo alirarua mavazi yake, akavaa mavazi ya magunia, na kuomboleza kwa ajili ya mwanawe kwa siku nyingi.

Yusufu aliuzwa kwa nani Misri?

Yusufu aliuzwa kwa Potifa, afisa wa Farao, huko Misri.