Genesis 36

Genesis 36:1

Vizazi vya Esau vinaitwa kwa jina gani lingine?

Vizazi vya Esau pia vinaitwa Edomu.

Esau alipata wake zake kutoka wapi?

Esau alipata wake zake kutoka kwa Wakaanani.

Genesis 36:6

Kwa nini Esau aliondoka kutoka kwa ndugu yake Yakobo?

Esau aliondoka kutoka kwa ndugu yake Yakobo kwa sababu nchi haikuweza kuwatunza wote wawili kwa kuwa mali zao zilikuwa nyingi sana.

Esau alikaa wapi?

Esau alikaa katika kilima cha nchi ya Seiri.

Genesis 36:9

Jina la mwana wa kiume aliyezaliwa na Timna, suria wa mwana wa kwanza wa Esau Elipfazi lilikuwa nani?

Jina la mwana aliyezaliwa na Timna alikuwa Amaleki.

Genesis 36:20

Ni nani alikuwa baba wa wakazi wa nchi ambayo Edomu aliishi?

Seiri Mhori alikuwa baba wa wakazi wa nchi ambayo Edomu aliishi.

Genesis 36:31

Watu wa Edomu walikuwa na nini kabla Israeli kuwa nao?

Watu wa Edomu walikuwa na wafalme kabla mfalme yeyote hajatawala juu ya Waisraeli.

Genesis 36:40

Ni nani alikuwa baba wa Waedomu?

Esau alikuwa baba wa Waedomu.