Genesis 39

Genesis 39:1

Ni nani alimnunua Yusufu Misri?

Potifa, afisa wa Farao, alimnunua Yusufu Misri.

Genesis 39:3

Kwa nini Yusufu alifanikiwa Misri?

Yusufu alikuwa na mafanikio kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye.

Genesis 39:5

Potifa aliweka nini chini ya usimamizi wa Yusufu?

Potifa aliweka kila kitu alichokuwa nacho chini ya usimamizi wa Yusufu.

Genesis 39:7

Mke wa Potifa alimwambia Yusufu kufanya nini?

Mke wa Potifa alimwambia Yusufu kulala naye.

Yusufu alijibuje kwa ombi la mke wa Potifa?

Yusufu alikataa na kusema hawezi kufanya uovu mkubwa namna hii na kutenda dhambi dhidi ya Mungu.

Genesis 39:10

Yusufu alifanya nini pale mke wa Potifa alipomkamata nguo zake?

Yusufu aliacha nguo zake mikononi mwake na kukimbia nje.

Genesis 39:13

Mke wa Potifa alitoa mashataka gani dhidi ya Yusufu?

Alimshtaki kwa kujaribu kulala naye kinyume na ridhaa yake.

Genesis 39:19

Potifa alifanya nini aliposikia mashtaka dhidi ya Yusufu?

Potifa alipata hasira sana na kumweka Yusufu gerezani.

Genesis 39:21

Kwa kipindi hiki, Yahwe alionyesha nini kwa Yusufu?

Yahwe alionyesha agano lake la uaminifu kwa Yusufu katika kipindi hiki.

Mlinzi wa gereza aliweka nini chini ya usimamizi wa Yusufu?

Mlinzi wa gereza aliwaweka wafungwa wote chini ya usimamizi wa Yusufu.

Matokeo ya kila jambo aliyofanya Yusufu yalikuwa ni nini, na kwa nini?

Yahwe alifanikisha kila kitu alichofanya Yusufu.