Genesis 14

Genesis 14:10

Nini kilitokea kwa Sodoma kama matokeo ya vita ya wafalme katika bonde la Sidimu?

Mali zote za Sodoma zilichukuliwa, na Lutu pamoja na mali zake zilichukuliwa pia.

Genesis 14:13

Abramu alifanya nini alipoambiwa ya kwamba Lutu alichukuliwa?

Abramu alikusanya wanamume wake waliofunzwa 318 kuwafuata.

Genesis 14:15

Abramu alipigana karibu na mji gani mkubwa, na nini kilikuwa matokeo ya vita hii?

Abramu alipigana wafalme wa kaskazini mwa Dameski, na alirudisha mali, Lutu, na watu wengine.

Genesis 14:17

Wafalme gani wawili walikutana na Abramu aliporudi?

Mfalme wa Sodoma na Melkizedeki, mfalme wa Salemu, alikutana na Abramu aliporudi.

Mahusiano ya Melkizedeki na Mungu yalikuwaje?

Melkizedeki alikuwa kuhani wa Mungu wa Juu Sana.

Melkizedeki alileta nini pamoja naye alipokutana na Abramu?

Melkizedeki alileta mkate na divai pamoja naye alipokutana na Abramu.

Genesis 14:19

Melkizedeki alimwambia nini Abramu?

Melkizedeki alimbariki Abramu, na kumbariki Mungu Aliye Juu Sana.

Abramu alifanya nini baada ya Melkizedeki kuzungumza naye?

Abramu alimpatia Melkizedeki moja ya kumi ya kila kitu.

Genesis 14:21

Mfalme wa Sodoma alitoa ahadi gani kwa Abramu?

Mfalme wa Sodoma aliahidi kumruhusu Abramu kukaa na mali zote, kama Abramu atawapa watu kwa mfalme.

Kwa nini Abramu hakutaka mali yoyote ile?

Abramu alikuwa ameinua mkono wake kwa Yahwe, Mungu aliye Juu Sana, na hakutaka mfalme wa Sodoma kuweza kusema ya kwamba amemfanya Abramu kuwa tajiri.

Abramu aliitikiaje kwa ahadi ya mfalme wa Sodoma?

Abramu alisema ya kwamba hakutaka mali yoyote ile, isipokuwa kile walichokula vijana na sehemu kwa ajili ya wanamume waliokwenda naye.