Genesis 13

Genesis 13:1

Baada ya kuondoka Misri, Abramu alisafiri kwenda wapi?

Abramu alisafiri kwenda Negebu.

Abramu alibeba nini pamoja naye?

Abramu alibeba wanyama wengi, na fedha na dhahabu nyingi.

Genesis 13:5

Kwa nini kulikuwa na ugomvi kati ya wachungaji wa Abramu na wa Lutu?

Kulikuwa na ugomvi kwa sababu nchi haikuweza kuwatunza Abramu na Lutu walipoishi karibu pamoja na mali zao zote.

Genesis 13:8

Abramu alitoa ahadi gani kwa Lutu

Abramu alimwambia Lutu kuchagua wapi pa kuishi, na kisha Abramu angetafuta mahali pake pa kuishi tofauti na Lutu.

Genesis 13:10

Lutu alichagua kusihi wapi na kwa nini?

Lutu alichagua kuhama mashariki na kuishi katika nchi tambarare za Yordani kwa sababu zilikuwa na maji kila mahali.

Genesis 13:12

Abramu alikuwa akiishi wapi?

Abramu aliishi katika nchi ya Kaanani.

Aina gani ya watu walikuwa wakiishi Sodoma?

Watu wa Sodoma walikuwa wenye dhambi waovu dhidi ya Yawhe.

Genesis 13:14

Katika kipindi hiki, Yahwe alisema angempatia nini Abramu?

Yahwe aliahidi ya kwamba nchi yote ambayo Abramu aliweza kuiona pale alipokuwa amesimama ingepewa kwake.

Genesis 13:16

Yahwe alimwambia Abramu atakuwa na vizazi vingapi?

Yahwe alimwambia Abramu ya kuwa angekuwa na vizazi zaidi ya uwezo wa kuhesabu, "wengi kama mavumbi ya nchi"

Abramu alikwenda karibu na mji upi?

Abramu alikwenda karibu na mji wa Hebroni.