Genesis 3

Genesis 3:1

Nyoka aliuliza swali gani la kwanza kwa mwanamke?

Nyoka alimuuliza mwanamke, "Je ni kweli Mungu amesema, 'Msile matunda kutoka kwenye mti wowote bustanini'?"

Genesis 3:4

Mwanamke aliposema Mungu aliwaambia ya kuwa watakufa iwapo watakula kutoka kwenye mti katikati ya bustani, nyoka alisema nini?

Nyoka alisema, "hakika hamtakufa"

Nyoka alisema nini kingetokea kwa mwanamume na mwanamke iwapo watakula tunda lile?

Nyoka aliwaambia ya kuwa watakuwa kama Mungu, kujua mema na mabaya.

Nini kilimvutia mwanamke kwa tunda la mti?

Aliona kuwa tunda ni zuri kwa chakula, na kuwa linapendeza macho, na kwamba linatamanisha kumfanya mtu awe na hekima.

Ni nani alikula tunda lile?

Mwanamke alikula , na kumpatia sehemu kwa mumewe ambaye alikula pia.

Genesis 3:7

Nini kilitokea kwao walipokula lile tunda?

Walipokula, macho yao yalifumbuliwa na wakajua ya kwamba wapo uchi.

Mwanamume na mwanamke walifanya nini Mungu alipokuja bustanini?

Walijificha kutoka kwa Mungu.

Genesis 3:9

Kwa nini mwanamume alijificha kutoka kwa Mungu alipokuja bustanini?

Mwanamume alijificha kutoka kwa Mungu kwa sana alikuwa uchi na hivyo kuogopa.

Genesis 3:12

Mwanamume alisema ni nani alihusika kumpatia tunda lile?

Mwanamume alisema mwanamke ndiye aliyehusika.

Mwanamke alisema ni nani alihusika kumpatia tunda lile?

Mwanamke alisema ya kwamba nyoka alihusika.

Genesis 3:14

Mungu alisema ni aina gani ya mahusiano yangekuwa kati ya nyoka na mwanamke?

Mungu alisema angesababisha wao kuchukiana.

Genesis 3:16

Ni laana gani Mungu alimpatia mwanamke kuhusu kuzaa watoto?

Mungu alizidisha uchungu wa mwanamke maradufu wakati wa kuzaa watoto.

Genesis 3:17

Mungu alimpatia laana gani mwanamume kuhusu kazi yake?

Mungu alilaani ardhi ili kwamba iwe kwa kazi ya maumivu ndipo mwanamume atakula kutoka pale.

Genesis 3:20

Mwanamume alimpatia jina gani mwanamke, na kwa nini?

Mwanamume alimpatia mwanamke jina la Hawa, kwa sababu alikuwa mama wa viumbe wote hai.

Mungu alitengeneza nini kwa ajili ya Adamu na Hawa, na kwa nini?

Mungu alitengeneza mavazi ya ngozi ili kuwavisha.

Genesis 3:22

Kwa nini Mungu alisema ya kwamba sasa Adamu hapaswi kula katika mti wa uzima wa milele?

Mungu alisema ya kwamba kwa kuwa Adamu sasa anajua mema na mabaya hapaswi kula katika mti wa uzima, kwa sababu ataweza kuishi milele.

Mungu alifanya nini kumzuia Adamu kula kutoka katika mti wa uzima?

Mungu alimfukuza mtu kutoka katika bustani na kuweka upanga wa moto pale kulinda njia ya kuelekea mti wa uzima.