Genesis 2

Genesis 2:1

Mungu alifanya nini katika siku ya saba?

Alipumzika kutoka kwa kazi yake yote, na kuibariki na kuitakasa siku hiyo.

Genesis 2:4

Kabla Yahwe hajasababisha mvua kunyesha, nchi ilikuwa inapataje maji?

Ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi.

Genesis 2:7

Yahwe alimuumbaje mtu?

Yahwe alimuumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi na kupuliza pumzi ya uhai kwake.

Yahwe alimweka wapi mtu wa kwanza?

Katika shamba la Edeni.

Genesis 2:9

Miti gani miwili ilikuwa miongoni mwa bustani?

Mti wa uzima na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Genesis 2:15

Mtu alipaswa kufanya nini bustanini?

Alipaswa kulima na kutunza bustani.

Yahwe alimpa mtu amri gani kuhusu kile alichopaswa kula?

Unaweza kula katika kila mti bustanini, isipokuwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Yahwe alisema nini kingetokea iwapo mtu angevunja amri hii?

Katika siku ambayo mtu atavunja amri hii, hakika atakufa.

Genesis 2:18

Yahwe alisema nini hakikuwa kizuri?

Alisema haikuwa vizuri ya kwamba mtu alikuwa peke yake.

Yahwe alimfanya mtu kutenda nini na kila kiumbe hai?

Mtu aliwapatia kila kiumbe hai jina.

Ni nini hakikupatikana miongoni mwa viumbe hai?

Msaidizi wa mtu atakayemfaa yeye.

Genesis 2:21

Yahwe alimuumbaje mwanamke?

Yahwe alimsababisha mwanamume kulala na kuchukua mbavu za mwanamume, na kumuumba mwanamke kutoka kwa ubavu ule.

Kwa nini mwanamume alimuita "mwanamke"?

Kwa sababu alichukuliwa kutoka kwa mwanamume.

Genesis 2:24

Mwanamume na mwanamke wanakuaje mwili mmoja?

Mwanamume anaungana na mwanamke kama mke wake.

Je mwanamume na mke wake walikuwa na aibu kuwa uchi?

Hapana.