Genesis 35

Genesis 35:1

panda kwenda Betheli

Msemo "panda" unatumika kwa sababu Betheli ipo sehemu ya juu kuliko Shekemu.

Unijengee madhabahu pale

Mungu anaongea kuhusu yeye mwenyewe katika lugha ya utatu. "Jenga madhabahu pale kwangu, Mungu wako"

akawambia nyumba yake

"akwaambia familia yake"

Wekeni mbali miungu yote ya kigeni iliyo kati yenu

"Tupa mbali sanamu zenu" au "Zitokomeze miungu yenu ya uongo"

jitakaseni wenyewe, na kubadili mavazi yenu

Hii ilikuwa utamaduni wa kujitakasa kimaadili na kimwili kabla ya kwenda kumuabudu Mungu.

kubadili mavazi yenu

Kuvaa mavazi mapya ilikuwa ishara ya kwamba walijifanya safi kabla ya kumkaribia Mungu.

katika siku ya shida yangu

Maana za "siku" zaweza kuwa 1) siku ambayo Yakobo alimtoroka Esau au 2) "siku" ina maana ya kipindi ambacho Yakobo alikuwa na mawazo. "nilipokuwa katika kipindi kigumu" au "nilipokuwa katika shida"

Genesis 35:4

Hivyo wakampa

"kwa hiyo kila mmoja katika nyumba ya Yakobo akatoa" au "kwa hiyo kila mtu katika familia na watumishi walitoa"

iliyokuwa mikononi mwao

Hapa "mikononi mwao" ina maana ya kile walichomiliki. "kilichokuwa mali yao" au "walivyokua navyo"

heleni zilizokuwa katika masikio yao

"heleni zao". Maana zaweza kuwa 1) dhahabu katika heleni zingeweza kutumika sanamu zingine au 2) walichukua heleni hizi kutoka kwenye mji wa Shekemu baada ya kuishambulia na kuwaua watu wote. Heleni zingewakumbusha juu ya dhambi yao.

Mungu akaifanya miji yote iliyokuwa karibu nao kuhofu

Mungu kusababisha watu wa miji kumuogopa Yakobo na familia yake inazungumziwa kana kwamba "hofu" ilikuwa kitu kilichoanguka juu ya miji. Nomino inayojitegemea "hofu" inaweza kuwekwa kama "kuogopa". "Mungu aliwafanya watu waliozunguka miji kumuogopa Yakobo na wote aliokuwa nao"

miji yote

Hapa "miji" ina maana ya watu wanaoishi katika miji.

wana wa Yakobo

Inasemekana ya kwamba hakuna mtu aliyeshambulia familia ya Yakobo. Lakini wana wawili, Simoni na Lawi walishambulia ndugu wa Wakaanani wa Shekemu baada ya kumkamata na kulala na binti wa Yakobo. Yakobo aliogopa wangelipiza kisasi katika 34:30. "Familia ya Yakobo" au "Nyumba ya Yakobo"

Genesis 35:6

Luzu

Hili ni jina la mji.

El Betheli

"Jina la El Betheli lina maana ya "Mungu wa Betheli"

Mungu alikuwa amejifunua kwake

"pale Mungu alijifunua kwa Yakobo"

Debora

Hili ni jina la mwanamke.

mlezi wa Rebeka

Mlezi ni mwanamke ambaye humtunza mtoto wa mwanamke mwingine. Mlezi aliheshimika na alikuwa muhimu sana kwa familia.

Akazikwa chini kutoka Betheli

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walimzika chini kutoka Betheli"

chini kutoka Betheli

Msemo "chini kutoka" unatumika kwa sababu walimzika katika eneo ambalo lilikuwa chini kwa mwinuko kuliko Betheli.

Aloni Bakuthi.

"Jina la Aloni Bakuthi lina maana ya "Mwaloni ambapo kuna maombolezo"

Genesis 35:9

Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba walikuwa Betheli. "Baada ya Yakobo kuondoka Padani Aramu, na wakati alipokuwa Betheli"

kumbariki

Hapa "kubariki" ina maana ya kutamka baraka maalumu juu ya mtu na kusababisha mambo mazuri kutokea juu ya mtu huyo.

lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena"

Genesis 35:11

Mungu akamwambia

"Mungu akamwambia Yakobo"

Uwe mwenye kuzaa na kuongezeka

Mungu akamwambia Yakobo kuzaa watoto ili kwamba waweze kuwa wengi wao. Neno "kuongezeka" unaelezea jinsi anavyotakiwa "kuzaa".

Taifa na wingi wa mataifa watakujia, na wafalme watatoka miongoni mwa uzao wako

Hapa "taifa" na "mataifa" yana maana ya vizazi vya Yakobo ambao wataunda mataifa haya.

Mungu akapanda kutoka

Hapa "akapanda kutoka" inatumika kwa sababu Mungu anapoishi inafikiriwa kuwa juu au juu ya dunia. "Mungu akamuacha"

Genesis 35:14

nguzo

Hii ni nguzo ya ukumbusho ambayo ilikuwa jiwe au jabali kubwa iliyowekwa mwishoni pake.

Akamimina juu yake sadaka ya kinywaji na akamimina mafuta juu yake

Hii ni ishara ya kwamba anaweka wakfu nguzo kwa Mungu.

Betheli

"Jina la Betheli lina maana ya "nyumba ya Mungu".

Genesis 35:16

Efrathi

Hili ni jina lingine la mji wa Bethelehemu.

akashikwa na uchungu

"Alikuwa na wakati mgumu wakati alipokuwa akimzaa mtoto"

Alipokuwa katika utungu mzito zaidi

"Uchungu ulipokuwa katika hatua mbaya zaidi"

mkunga

mtu anayemsaidia mwanamke anapojifungua mtoto

Hata alipokaribia kufa, kwa pumzi yake ya mwisho

"pumzi yake ya mwisho" ni pumzi ya mwisho ya mtu kabla mtu hajafa. "Hata kabla hajafa, alipovuta pumzi yake ya mwisho"

Benoni

"Jina la Benoni lina maana ya "mtoto wa majonzi yangu""

Benyamini

Watafsiri wanaweza kuweka maandishi mafupi yasemayo "Jina la Benyamini lina maana ya "mtoto wa mkono wa kuume". Msemo wa "mkono wa kulia" unalenga sehemu yenye upendeleo maalumu.

na kuzikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na wakamzika"

katika njia

"pembeni mwa barabara"

ndiyo alama ya kaburi la Raheli hata leo

"inaweka alama juu ya kaburi la Raheli mpaka siku hii"

hata leo

"mpaka wakati huu wa leo." Hii ina maana hadi wakati ambapo mwandishi alikuwa akiandika haya.

Genesis 35:21

Israeli akaendelea

Inasemekana ya kwamba familia ya Israeli na watumishi wake wako pamoja naye. Maana kamili ya taarifa hii inaweza kuwekwa wazi.

Bilha

Hii ni jina la mtumishi wa Raheli wa kike.

Basi Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili

Sentensi hii inaanza ibara mpya, ambayo inaendeleza mistari inayofuata.

wana kumi na mbili

"watoto 12"

Genesis 35:23

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa Raheli wa kike.

Genesis 35:26

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

waliozaliwa kwake huko Padani Aramu

Inasemekana ya kwamba hii haimjumlishi Benyamini aliyezaliwa katika nchi ya Kaanani karibu na Bethelehemu. Inataja Padani Aramu tu kwa maana hapo ndipo wengi wao walizaliwa. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi. "ambao walizaliwa kwake Padani Aramu, isipokuwa Benyamini ambaye alizaliwa katika nchi ya Kaanani"

Yakobo akaja kwa Isaka

Hapa "akaja" inaweza kuweka kama "akaondoka"

Mamre

Hili lilikuwa jina lingine la mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale. Hii ilikuwa jina la mwanamume aliyemiliki miti ya mwaloni.

Kiriathi Arba

Hili ni jina la mji.

Genesis 35:28

miaka mia moja na themanini

"miaka 180"

Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa

"Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa". Misemo ya "alivuta pumzi ya mwisho" na "akafa" ina maana ya kitu kimoja. "Abrahamu alikufa"

akapumua pumzi yake ya mwisho

Hii ni njia ya upole ya kusema mtu alikufa.

akakusanywa kwa wahenga wake

Hii ina maana ya kwamba baada ya Isaka kufa, roho yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alijiunga na familia yake waliokuwa wamekufa"

mtu mzee amejaa siku

Misemo ya "mtu mzee" na "amejaa siku" zina maan moja. Zinasisitiza ya kwamba Isaka aliishi muda mrefu sana. "baada ya kuishi muda mrefu sana na kuzeeka sana"