Genesis 28

Genesis 28:1

Usichukuwe

"Usichukue"

Inuka, nenda

"Nenda mara moja"

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine kwa ajili ya eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo sawa na Iraq ya sasa.

nyumba ya

Hii ina maana ya vizazi vya mtu au ndugu wengine. "familia"

Bethueli

Bethueli alikwa baba wa Rebeka.

baba wa mama yako

"babu yako"

mmojawapo wa binti

"kutoka kwa mabinti"

kaka wa mama yako

"mjomba wako"

Genesis 28:3

Taarifa ya Jumla:

Isaka anaendelea kuzungumza na Yakobo

akupe uzao na akuzidishe

Neno "kuongeza" unaelezea jinsi Mungu angemfanya Yakobo "azidishiwe". "akupe uzao na watoto wengi"

Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako

Hii inazungumzia kuhusu kubariki mtu kana kwamba baraka ni kitu ambacho mtu anaweza kutoa. Nomino inayojitegemea "baraka" inaweza lusemwa kama "bariki". "Na Mungu akubariki wewe na uzao vyako kama alivyombariki Abrahamu" au "Na Mungu akupatie wewe na uzao wako kile alichoahidi kwa Abrahamu"

kwamba uweze kumilki nchi

Mungu kutoa nchi ya Kaanani kwa Yakobo na uzao wake inazungumziwa kana kwamba mtoto alikuwa akirithi fedha au mali kutoka kwa baba yake.

nchi ambapo umekuwa ukiishi

"nchi ambayo ulikuwa ukiishi"

ambayo Mungu alimpa Abrahamu

"ambayo Mungu aliahidi kwa Abrahamu"

Genesis 28:5

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine kwa ajili ya eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo sawa na Iraq ya sasa.

Bethueli

Bethueli alikwa baba wa Rebeka.

Genesis 28:6

Taarifa ya Jumla:

Simulizi inabadilika kutoka kwa Yakobo kuelekea kwa Esau

Basi

Neno hili linatumiwa hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Esau.

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine kwa ajili ya eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo sawa na Iraki ya sasa.

kuchukua mke

"kuchukua mke kwa ajili yake"

akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki

"Esau aliona pia ya kwamba Isaka alimbariki Yakobo"

Usichukue

"Usichukue"

wanawake wa Kanaani

"binti wa Kaanani" au "wanawake wa Kaanani"

Genesis 28:8

Taarifa ya Jumla:

Hii inaendeleza taarifa ya nyuma kuhusu Esau.

Esau akaona

"Esau akagundua"

wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake

"baba yake Isaka hakuidhinisha wanawake wa Kaanani"

wanawake wa Kanaani

"binti wa Kaanani" au "wanawake wa Kaanani"

Hivyo

"Kwa sababu hiyo"

mbali na wake aliokuwa nao

"kwa kuongeza juu ya wake aliokuwa nao tayari"

Mahalathi

Hili ni jina la mmoja wa binti wa Ishmaeli.

Nebayothi

Hili ni jina la mmoja wa vijana wa Ishmaeli.

Genesis 28:10

Taarifa ya Jumla:

Simulizi inabadilika kurudi kwa Yakobo

Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa

"Akaja katika eneo fulani na kwa sababu jua lilikuwa limezama, aliamua kukaa usiku"

Genesis 28:12

Akaota

"Yakobo alipata ndoto"

imewekwa juu ya nchi

"chini yake ikigusa ardhini"

ilifika hata mbinguni

Hii ina maana ya sehemu ambapo Mungu anaishi.

Tazama

Neno la "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa ya kushtukiza inayofuata.

Yahwe amesimama juu yake

Maana zaweza kuwa 1) "Yahwe alikuwa amesimama juu ya ngazi" au 2) "Yahwe alikuwa amesima kando na Yakobo"

Abrahamu baba yako

Hapa "baba" ina maana ya "babu". "Abrahamu babu yako" au "Abrahamu babu yako"

Genesis 28:14

Taarifa ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Yakobo ndotoni.

Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi

Mungu analinganisha uzao wa Yakobo na vumbi la ardhi kuweka msisitizo ya idadi kubwa. "Utakuwa na uzao mkubwa zaidi ya utakavyoweza kuhesabu"

na utaenea mbali kuelekea magharibi

Hapa neno "utaenea" lipo katika hali ya upekee lakina lina maana ya uzao wa Yakobo. Inazungumzia kuhusu Yakobo kwa maana yeye ni kiongozi wa familia. "na uzao wako utasambaa hadi magharibi"

na utaenea mbali

Hii ina maana ya watu wataongeza mipaka ya ardhi yao na kukaa

katika maeneo makubwa zaidi.

kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini Misemo hii inatumika pamoja kumaanisha "pande zote". "katika pande zote"

Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitabariki familia zote juu ya dunia kupitia kwako na uzao wako"

Tazama

Hii inaongeza msisitizo kwa kile kinachosemwa baadae. "Tazama" au "Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachotaka kukuambia"

kwani sitakuacha. Nitafanya kila

"kwa kuwa sitakuacha mpaka nitende yote"

nitakulinda

"Nitakuweka salama" au "Nitakulinda"

Nitakurudisha katika nchi hii tena

"Nitakuleta katika nchi hii"

Genesis 28:16

akaamka katika usingizi

"aliamka kutoka katika usingizi wake"

nyumba ya Mungu ... lango la mbinguni

Msemo wa "lango la mbinguni" linaelezea ya kwamba sehemu hii ni kiingilio cha "nyumba ya Mungu" na "mlango wa mahali Mungu anapoishi"

Hili ni lango la mbinguni

Hii inazungumzia kuhusu mlango ambapo Mungu anaishi kana kwamba ilikuwa ni ufalme halisi ambao ulikuwa na lango ambalo mtu anatakiwa kufungua kuruhusu watu ndani.

Genesis 28:18

nguzo

Hii ni nguzo ya kumbukumbu, yaani, jiwe kubwa au jabali lililowekwa mwishoni pake.

kumimina mafuta juu yake

Tendo hili linaashiria ya kwamba Yakobo anaweka wakfu nguzo kwa Mungu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "alimwaga mafuta juu yake ili kuiweka wakfu nguzo kwa Mungu"

Betheli

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Betheli lina maana 'nyumba ya Mungu."

Luzu

Hili ni jina la mji.

Genesis 28:20

akatoa nadhiri

"akafanya kiapo" au "alimuahidi Mungu kwa dhati"

Ikiwa Mungu atakuwa ... ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu

Yakobo anazungumza na Mungu katika lugha ya mtu wa utatu. Hii inaweza kusemwa katika lugha ya upili wa mtu. "Iwapo uta ... basi wewe, Yahwe, utakuwa Mungu ambaye nitamuabudu"

katika njia nipitayo

Hii ina maana ya safari ya Yakobo kutafuta mke na kurudi nyumbani. "katika safari hii"

atanipa mkate wa kula

Hapa "mkate" una maana ya chakula kwa ujumla.

katika nyumba ya baba yangu

Hapa "nyumba" ina maana ya familia ya Yakobo. "kwa baba yangu na familia yangu iliyosalia"

jiwe takatifu

Hii ina maana ya kwamba jiwe litaweka alama ya sehemu ambayo Mungu alijitokeza kwake na itakuwa sehemu ambapo watu watamuabudu Mungu. "nyumba ya Mungu" au "sehemu ya Mungu"