Genesis 26

Genesis 26:1

Basi

Neno hili linatumika kuweka alama kwa sehemu mpya ya simulizi.

njaa ikatokea

"kukawa na njaa" au "kukawa na njaa nyingine"

katika nchi

Unaweza kusema wazi ya kwamba nchi inayozungumziwa. "katika nchi ambayo Isaka na familia yake waliishi"

iliyotokea siku za Ibrahimu

Msemo "katika siku" ina maana ya wakati ambapo Abrahamu alikuwa hai. "ambayo ilitokea wakati wa uhai wa Abrahamu"

Genesis 26:2

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaanza kuzungumza na Isaka.

akamtokea

"akamtokea Isaka"

Usishuke kwenda Misri

Ilikuwa kawaida kuzungumzia kuondoka nchi ya ahadi kama "kushuka chini" kwenda sehemu nyingine.

kwani kwako wewe na uzao wako, nitawapa nchi hii yote

"kwa maana nitakupa nchi hizi zote kwako na kwa uzao wako"

nitatimiza kiapo nilichomwapia Ibrahimu baba yako

"Nitafanya kile nilichoahidi kwa Abrahamu baba yako kukifanya"

Genesis 26:4

Taarifa ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuzungumza na Isaka

Nitauzidisha uzao wako

"Nitasababisha uwe na uzao mwingi"

kama nyota za mbinguni

Hii inazungumzia kuhusu uzao wa Isaka kana kwamba walikuwa sawa na idadi ya nyota.

mbinguni

Hii ina maana ya kila kitu juu ya dunia ikijumlisha jua, mwezi na nyota.

mataifa yote ya dunia yatabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitabariki mataifa yote ya dunia"

Abrahamu aliitii sauti yangu na kutunza maelekezo yangu, amri zangu na sheria zangu

Misemo hii "alitii sauti yangu" na "kutunza maelekezo yangu, amri zangu na sheria zangu" zina maana moja. "Abrahamu alinitii na kufanya kila kitu nilichomuamuru kufanya"

aliitii sauti yangu

Hapa "sauti" ina maana ya Yahwe. "Alinitii"

Genesis 26:6

Hivyo Isaka akakaa Gerari

Isaka pekee ndiye aliyetajwa kwa sababu ni kiongozi wa familia, lakini familia yake yote ilikuwa pamoja naye. "Kwa hiyo Isaka na familia yake walikaa Gerari"

Aliogopa kusema

Hapa "aliogopa" ina maana ya hisia isiyofaa inayompata mtu wakati akipata tishio la kudhuriwa kwake au kwa wengine. "Aliogopa kusema"

wamchukue Rebeka

"ili kwamba wamchukue Rebeka"

Tazama, akamwona Isaka

Neno "tazama" linaonyesha ya kwamba kile alichokiona Abimeleki kilimshangaza. "Na alishangazwa kuona ya kwamba Isaka"

akimpapasa Rebeka

Maana zaweza kuwa 1) alikuwa akimgusa kwa njia ambayo mume humgusa mkewake au 2) alikuwa akicheka na kuzungumza pamoja naye kwa namna ambayo mume huzungumza na mkewe.

Genesis 26:9

Abimeleki akamwita Isaka kwake

Yawezekana Abimeleki alimtuma mtu kumwambia Isaka ya kwamba alihitaji kumuona. "Abimeleki alimtuma mtu kumleta Isaka kwake"

Kwa nini ulisema, 'Yeye ni dada yangu?"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuelezwa kama nukuu isiyokuwa moja kwa moja. "Kwa nini ulisema ya kwamba ni dada yako?"

amchukue

"ili amchukue"

Ni jambo gani hili ulilotufanyia?

Abimeleki alitumia swali hili kumkaripia Isaka. "Haukupaswa kufanya jambo hili kwetu!"

ungeweza kuleta hatia juu yetu

Hii inazungumzia kuhusu kumsababisha mtu kuwa na hatia kana kwamba "hatia" ilikuwa ni kitu kinachowekwa juu ya mtu. "ungeweza kusababisha tuwe na hatia ya kuchukua mke wa mtu"

juu yetu

Hapa "yetu" ina maana ya Abimeleki na watu wake.

Mtu yeyote atakayemgusa mtu huyu

Hapa "atakayemgusa" ina maana ya kumgusa kwa namna ya kumdhuru. "Yeyote atakayemdhuru mwanamume huyu"

hakika atauwawa

Inawezekana Abimeleki alikusudia kumwambia mtu kumuua yeyote ambaye angemdhuru Isaka au Rebeka. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitamuua" au "Nitawaamuru wanamume wangu kumuua"

Genesis 26:12

Taarifa ya Jumla

Hii inaanza sehemu mpya ya simulizi. Inabadilisha kutoka kueleza kuhusu Isaka kumuita Rebeka dada yake, na inaanza kuelezea kuhusu jinsi Isaka alivyokuwa tajiri na Wafilisti wakawa na wivu kwake.

katika nchi hiyo

"Gerari"

vipimo mia

Hii ina maana ya "mara mia zaidi ya alivyopanda"/Inaweza kuelezwa kwa ujumla zaidi kama "zao kubwa sana"

Mtu huyo akawa tajiri

"Isaka akawa tajiri" au "Akawa tajiri"

akaongezeka zaidi hata akawa mkuu sana

"na akapata zaidi na zaidi hadi akawa tajiri sana"

kondoo

Hii inaweza kujumuisha mbuzi pia.

familia kubwa

Hapa "familia" ina maana ya wafanya kazi au watumishi. "watumishi wengi"

Wafilisiti wakamwonea wivu

"Wafilisti walikuwa na wivu kwake"

Genesis 26:15

Basi

Hapa neno hili halimaanishi "katika kipindi hiki". Inaonyesha wapi matukio ya simulizi yanapoanzia. Inaweza kutafsiriwa kwa neno unganishi "Kwa hiyo" kuonyesha ya kwamba hii ni tokeo la kilichotokea katika 26:12.

katika siku za Ibrahimu baba yake

Msemo wa "katika siku za" ina maana ya maisha ya mtu. "wakati Abrahamu, baba yake, alipokuwa akiishi"

Abimeleki akamwambia

Maana zaweza kuwa 1) hili ni tukio lingine kumlazimisha Isaka na watu wake kuondoka. "Kisha Abimeleki akasema" au "Hatimaye Abimeleki akasema" au 2) Abimeleki alifanya uamuzi huu kwa sababu aliona ya kwamba watu wake walikuwa na wivu na walitenda uhasama dhidi ya Isaka. "Basi Abimeleki akasema"

nguvu kuliko sisi

"mwenye nguvu zaidi ya sisi"

Hivyo Isaka akaondoka

Isaka pekee ametajwa kwa sababu yeye ni kiongozi, lakini familia yake na watumishi wake walienda naye. "Kwa hiyo Isaka na nyumba yake waliondoka"

Genesis 26:18

Isaka akachimba

Hapa "Isaka" ina maana ya Isaka na watumishi wake. "Isaka na watumishi wake wakachimba"

vilivyokuwa vimechimbwa

"ambao watumishi wa Abrahamu walichimba"

siku za Abrahimu baba yake

Msemo "katika siku za" ina maana ya maisha yote ya binadamu. "ambapo Abrahamu, baba yake, alipokuwa anaishi"

Wafilisiti walikuwa wamevizuia

Hii ndio ilikuwa sababu ya Isaka kuvichimba. Njia kadhaa za kutafsiri hii ni 1) Kwa kuwa hili lilitokea kwanza, sentensi hii inaweza ikaja kabla ya sentensi juu ya Isaka kuvichimba au 2) Sentensi hii inaweza kuanza na "Isaka alifanya hivi kwa sababu Wafilisti waliwazuia"

wamevizuia

"walizijaza na udongo"

Genesis 26:19

maji yaliyokuwakuwa yakibubujika

Msemo huu una maana ya chemichemi ya maji ya asili waliyofunua walipokuwa wakichimba kisima kipya. Ilitoa maji safi ya muendelezo kwa ajili ya kunywa.

Wachungaji

"wanamume wanaotunza mifugo"

Haya ni maji yetu

Hapa "yetu" ina maana ya wafugaji wa Gerari"

Eseki

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Eseki lina maana ya "malumbano" au "mabishano".

Genesis 26:21

Wakachimba

"Kisha watumishi wa Isaka wakachimba"

wakakigombania

"wafugaji wa Gerari walibishana na wafugaji wa Isaka"

hivyo akakiita

"kwa hiyo Isaka akakiita"

Sitina

Watafsiri wanaweza kuweka maandishi mafupi yanayosema. "Jina la Sitna ina maana ya "kupinga" au "kushtaki"

Rehobothi

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Rehobothi lina maana ya "kuweka nafasi kwa ajili ya" au "nafasi wazi".

ametufanyia ... tutafanikiwa

Isaka alikuwa akijizungumzia mwenyewe na nyumba yake.

Genesis 26:23

Kisha Isaka akaenda Beersheba

Hapa "kwenda juu" inaweza kumaanisha kwenda kaskazini. "Isaka aliondoka pale na kwenda Beersheba"

kuvidisha vizazi vyako

"atasababisha vizazi vyako kuongezeka maradufu" au "atasababisha vizazi vyako kuwa wengi sana"

kwa ajili ya mtumishi wangu Abrahimu

"kwa mtumishi wangu Abrahamu" au unaweza kuweka maana yote wazi zaidi. "kwa sababu nilimuahidi mtumishi wangu Abrahamu kuwa nitafanya hili"

Isaka akajenga madhabahu pale

Unaweza kuweka wazi kwa nini Isaka alijenga dhabahu. "Isaka alijenga dhabahu pale kutoa sadaka kwa Yahwe"

akaliita jina la Yahwe

"Kuita" ina maana ya kuomba au kuabudu. Hapa "jina" lina maana ya Yahwe. "aliomba kwa Yahwe" au "alimuabudu Yahwe"

Genesis 26:26

akamwendea

"akaenda kwa Isaka"

Ahuzathi

Hili ni jina la mwanamume.

rafiki yake

Maana zaweza kuwa 1) "rafiki yake Abimeleki" au 2) "mshauri wa Abimeleki"

Fikoli

Hili ni jina la mwanamume.

Genesis 26:28

Nao wakasema

Hii ina maana ya Abimeleki, Ahuzathi na Fikoli. Mmoja wao aliongea na wengine wawili walikubaliana na kile alichosema. Haikumaanisha waliongea kwa wakati mmoja. "mmoja wao alisema"

Tumeona yakini

"Tunajua" au "Tuna uhakika"

Hivyo na tufanye agano

"Kwa hiyo tunataka kufanya agano"

na kama sisi tulivyokutendea vema wewe

Hii inaweza kutafsiriwa kama mwanzo wa sentensi mpya. "Tumetenda mema tu kwako"

umebarikiwa na Yahwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe amekubariki"

Genesis 26:30

Isaka akawaandalia sherehe, na wakala na kunywa

Kula chakula pamoja ilikuwa sehemu ya kufanya agano na mtu mwingine.

akawaandalia

Hapa "akawaandalia" ina maana ya "Abimeleki, Ahuzathi na Fikoli"

wakala

Hapa "wakala" ina maana ya Isaka, Abimeleki, Ahuzathi, na Fikoli. "walikula wote"

Wakaamuka mapema

"Waliamka mapema"

Genesis 26:32

Akakiita kile kisima Shiba

"Kwa hiyo alikiita kisima Shiba". Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Shiba linafanana na neno lenye maana ya "kiapo".

Beersheba

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Beersheba inaweza kumaanisha "kisima cha kiapo" au "kisima cha saba"

Genesis 26:34

Taarifa ya Jumla

Sehemu kubwa ya Mwanzo 26 inahusu Isaka. Mistari hii inamhusu mtoto wake mkubwa Esau.

arobaini

"40"

akajitwalia mke

"alioa". Unaweza kusema kwa uwazi ya kwamba alioa wanawake wawili. "alioa wake wawili"

Yudithi ... Basemathi

Haya ni majina ya wake wa Esau.

Beeri ... Eloni

Haya ni majina ya wanamume.

Mhiti

"vizazi vya Hethi" au "mzawa wa Hethi"

Wakamhuzunisha Isaka na Rebeka

Hapa "wakamhuzunisha" ina maana ya Yudithi na Basemathi. Kumhuzunisha au kumsikitisha mtu inazungumziwa kana kwamba "huzuni" ni chombo ambacho mtu anaweza kukileta kwa mtu. "Walimfanya Isaka na Rebeka wawe na huzuni" au "Isaka na Rebeka walimsikitisha kwa sababu yao"