Genesis 25

Genesis 25:1

Taarifa ya Jumla:

Taarifa kuhusu Abrahamu.

Hawa wote

Hii ina maana ya watu waliotajwa katika mistari ya 2-4.

Genesis 25:5

Abrahamu akampatia Isaka vitu vyote alivyokuwa navyo

"Isaka alirithi kila kitu alichomiliki Abrahamu". Ilikuwa kawaida kwa baba kugawanya utajiri wake alipokuwa mzee na sio kuacha hivyo kwa wengine kufanya baada ya yeye kufariki.

Genesis 25:7

Hizi ndizo zilikuwa siku za miaka ya uhai wake Abrahamu alizoishi, miaka 175

"Abrahamu aliishi miaka 175"

Abrahamu akapumua pumzi ya mwisho na akafa

"Abrahamu alivuta pumzi yake ya mwisho na akafa". Misemo ya "alivuta pumzi ya mwisho" na "akafa" ina maana ya kitu kimoja. "Abrahamu alikufa"

akapumua pumzi ya mwisho

Hii ni njia ya upole ya kusema mtu alikufa.

katika uzee mwema, mzee aliye shiba siku

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Abrahamu aliishi muda mrefu sana. "alipomaliza kuishi muda mrefu na akawa mzee sana"

mzee aliye shiba siku

Kuishi maisha marefu sana inazungumzwa kana kwamba maisha yalikuwa chombo kinachoweza kujaa.

akakusanywa kwa watu wake

Hii ina maana ya kwamba Abrahamu alikufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "aliwaunga familia yake ambao walikuwa wameshakufa"

Genesis 25:9

pango la Makipela, katika shamba la Efroni

Efroni alimiliki shamba Makpela na pango ambalo lilikuwa ndani ya hilo shamba. Abrahamu alinunua shamba lile kutoka kwa Efroni.

Makpela

Makpela lilikuwa jina la eneo au sehemu.

Efroni ... Soari

Haya ni majina ya wanamume.

lililokuwa karibu na Mamre

Makpela ilikuwa karibu na Mamre.

Mamre

Hii ilikuwa jina jingine kwa mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale"

Shamba hili Abrahamu alilinunua

"Abrahamu alinunua shamba hili"

watoto wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

Abrahamu akazikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walimzika Abrahamu"

mwanae

"Mwana wa Abrahamu"

Beerlalahairoi

Jina hili lina maana ya "kisima cha yule aliye hai anionaye mimi"

Genesis 25:12

Na sasa

Hili neno linatumika kutambulisha sehemu mpya ya simulizi na taarifa kuhusu Ishameli.

Genesis 25:13

Taarifa ya Jumla:

Taarifa ya jumla

Hawa ndio walikuwa wana wa Ishimaeli, na haya ndiyo majina yao, kwa vijiji vyao, na katika vituo vyao; Maseyidi kumi na wawili kufuatana na kabila zao

Hii inaweza kuwekwa kama sentensi mbili. "Haya yalikuwa majina ya wana kumi na wawili wa Ishmaeli. Waliongoza kabila ambazo ziliitwa baada yao, na kila mmoja wao alikuwa na vijiji vyao na kambi zao"

kumi na wawili

"12"

Maseyidi

Hapa neno "maseyidi" ina maana ya wanamume waliokuwa viongozi au watawala wa makabila; haimaanishi ya kwamba walikuwa watoto wa mfalme.

Genesis 25:17

Hii ndiyo ilikuwa miaka ya Ishimaeli, miaka 137

"Ishmaeli aliishi miaka 137"

akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa

Msemo "akapumua pumzi yake ya mwisho" na "akafa" zina maana moja. "alikufa"

akakusanywa pamoja na watu wake

Hii ina maana ya kwamba ishmaeli alikufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alijiunga na familia yake ambao tayari walikuwa wamekufa"

Walioshi

"Uzao wake walikaa"

toka Havila mpaka Shuri

"kati ya Havila na Shuri"

Havila

Havila Ilikuwa mahali katika jangwa la Arabia.

kama yule aelekeaye mbele

"katika upande wa"

Waliishi kwa uadui kati yao

Maana zaweza kuwa 1) "hawakuishi kwa amani pamoja" au 2) "waliishi mbali kutoka kwa ndugu zao wengine"

Genesis 25:19

Haya ndiyo yalikuwa matukio kumuhusu Isaka

Sentensi hii inatambulisha habari ya uzao wa Isaka katika Mwanzo 25:19-35:29. "Hii ni habari ya uzao wa Isaka, mwana wa Abrahamu"

umri wa miaka arobaini

"umri wa miaka 40"

alipomuoa Rebeka kuwa mke wake

"alipomuoa Rebeka"

Bethueli

Bethueli alikuwa baba wa Rebeka.

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine la eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo lile lile na Iraq ya sasa.

Genesis 25:21

alikuwa tasa

"hakuwa na uwezo wa kupata mimba"

Rebeka mkewe akabeba mimba

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba Rebeka alikuwa mimba na watoto wawili katika wakati mmoja. "Rebeka, mke wake, akawa mimba na mapacha"

Watoto hawa walipokuwa tumboni mwake wakasumbuka,

"watoto ndani mwake wakaendelea kugusana baina yao" au "Watoto walisukumana dhidi yao wenyewe ndani mwake"

Watoto ... tumboni mwake

Rebeka alikuwa mimba na mapacha.

Akaenda kumuuliza Yahwe kuhusu jambo hili

"Alienda kumuuliza Yahwe kuhusu suala hili". haipo wazi alienda wapi. Inawezekana alienda sehemu ya siri kuomba, au alienda sehemu kutoa sadaka.

Genesis 25:23

akamwambia

"akamwambia Rebeka"

Mataifa mawili ... atamtumikia mdogo

Hii ni lugha ya kishairi.

Mataifa mawili yako katika tumbo lako

Hapa "mataifa mawili" yana maana ya watoto wawili. Kila mtoto atakuwa baba wa taifa moja. "Mataifa mawili yatakuja pamoja kutoka kwa mapacha ndani yako"

na mataifa haya mawili yatatengana ndani yako

Hapa "mataifa mawili" ina maana ya watoto wawili. Kila mtoto atakuwa baba wa taifa moja. Hii inaweza kutafsiriwa kama kitenzi cha kutenda. "na utakapozaa hawa watoto wawili watakuwa wapinzani"

mkubwa atamtumikia mdogo

Maana zaweza kuwa 1) "mkubwa atamtumika mdogo" au 2) "uzao wa mkubwa utamtumikia uzao wa mdogo"

Genesis 25:24

tazama

Neno la "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "naam"

mwekundu mwili wote kama vazi la nywele

Maana zaweza kuwa 1) ngozi yake ilikuwa nyekundu na alikuwa na nywele nyingi katika mwili wake au 2) alikuwa na nywele nyingi nyekundu katika mwili wake. "nyekundu na yenye nywele kama nguo iliyotengenezwa na nywele ya mnyama"

Esau

"Jina Esau linafanana na neno "nywele"

umeshika kisigino cha Esau

"kushika sehemu ya nyuma ya mguu wa Esau"

Yakobo

"Jina Yakobo lina maana ya "anashika kisigino"

umri wa miaka sitini

"umri wa miak 60"

Genesis 25:27

akawa mwindaji hodari

"akawa hodari katika uwindaji na kuua wanyama kwa chakula"

mtu mkimya

"mtu wa amani" au"mtu asiyekuwa na mambo mengi"

aliye tumia muda wake akiwa katika mahema

Hii inazungumzia kuhusu muda kana kwamba ilikuwa bidhaa ambayo mtu angetumia. "aliyebaki katika mahema sehemu kubwa ya muda"

Kisha

Neno hili linatumika kuweka alama ya kubadili mwelekeo, kutoka katika simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Isaka na Rebeka.

Isaka akampenda

Hapa neno "akampenda" ina maana "alimpendelea" au "kumpenda zaidi"

kwa sababu alikula wanyama ambao alikuwa anawinda

"kwa sababu alikula wanyama ambao Esau aliwinda" au "kwa sababu alifurahia kula wanyama pori ambao Esau alikamata"

Genesis 25:29

Yakobo akapika

Kwa kuwa huu ni mwanzo wa simulizi kuhusu jambo lilitokea kipindi kimoja, baadhi ya watafsiri wanaweza kuanza na msemo wa "Siku moja, Yakobo alipika".

akapika mchuzi

"alichemsha chakula kiasi" au "alipika mchuzi kiasi". Mchuzi ulipikwa kwa dengu za kuchemsha.

akiwa dhaifu kutokana na njaa

"alikuwa dhaifu kwa sababu alikuwa na njaa sana" au "alikuwa na njaa sana"

nimechoka

"Nimechoka kwa sababu ya njaa" au "Nina njaa sana"

Edomu

Jina Edomu lina maana ya "nyekundu"

Genesis 25:31

haki yako ya mzaliwa wa kwanza

"haki ya mwana wa kwanza kurithi sehemu kubwa ya utajiri wa baba yake"

nakaribia kufa

Esau alitiachumvi kuweka msisitizo jinsi alivyokuwa na njaa. "Nina njaa mno nahisi kama vile ntakufa"

Ni nini kwangu haki ya mzaliwa wa kwanza?

Esau alitumia swali kuweka msisitizo ya kwamba kula ilikuwa muhimu zaidi ya haki ya mzawa wa kwanza. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Urithi wangu haunisaidii iwapo nitakufa kwa njaa!"

Kwanza uape kwangu mimi

Kile ambacho Yakobo alimtaka Esau aape kinaweza kuwekwa wazi. "kwanza apa kwangu ya kwamba utaniuzia haki yako ya mzaliwa wa kwanza"

dengu

Haya ni kama maharage, lakini mbegu zake ni ndogo sana, na kama vile tambarare.

Esau akawa ameidharau haki yake

"Esau alionyesha ya kwamba hakuthamini haki yake ya kuzaliwa"