Genesis 23

Genesis 23:1

Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba

miaka saba - 'Sara aliishi miaka 127"

Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara

Baadhi ya watafsiri hawajumlishi sentensi hii.

Kiriathi Arba

Hili ni jina la mji.

Abraham akaomboleza na kumlilia Sara

"Abrahamu alikuwa na huzuni sana na akalia kwa sababu Sara alikufa"

Genesis 23:3

akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa

"akasimama na kuacha mwili wa mke wake"

watoto wa kiume wa Hethi

Hapa "watoto" ina maana ya wale waliotokana na Hethi. "uzao wa Hethi" au "Wahiti"

miongoni mwenu

Wazo hili linaweza kuelezwa kwa lugha ya eneo. "katika nchi yako" au "hapa"

Tafadhari nipatieni mahali

"Niuzie sehemu ya nchi" au "Niruhusu kununua kipande cha nchi"

wafu wangu

Kivumishi kidogo "wafu" kinaweza kuelezwa kama kivumishi au kitenzi. "mke wangu aliyekufa" au "mke wangu ambaye amekufa"

Genesis 23:5

Wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale waliotokana na Hethi. "uzao wa Hethi"

bwana wangu

Msemo huu unatumika kuonyesha heshima kwa Abrahamu.

mwana wa Mungu

Hii ni lahaja. Hii yaweza kuwa na maana ya "mwanamume mwenye mamlaka" au "kiongozi mwenye nguvu"

wafu wako

Kivumishi kidogo cha "wafu" kinaweza kusemwa kama kitenzi au kwa njia ya urahisi kama "mke". "mke wako ambaye amekufa" au "mke wako"

katika makaburi yetu utakayochagua

"sehemu bora kabisa ya makaburi yetu"

atakaye kuzuilia kaburi lake

"kuzuia sehemu ya makaburi kwako" au " kukataa kukupatia makaburi"

Genesis 23:7

kusujudu

Hii ina maana ya kuinama au kupiga goti chini kabisa kwa kuonyesha unyenyekevu wa heshima na taadhima kwa mtu.

kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi

"kwa wana wa Hethi waliokuwa wakiishi katika eneo lile"

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

wafu wangu

Kivumishi kidogo "wafu" kinaweza kuelezwa kama kivumishi au kitenzi. "mke wangu aliyekufa" au "mke wangu ambaye amekufa"

Efroni .... Sohari

Haya ni majina ya wanamume.

pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake

"pango lake ambalo lipo mwishoni mwa shamba lililoko Makpela"

pango la Makpela

"pango lililoko Makpela". Makpela ilikuwa jina ya eneo au sehemu. Efroni alimiliki shamba katika Makpela na pango ambalo lilikuwa katika shamba.

ambalo analimiliki

Hii inatueleza jambo kuhusu pango lile. Efroni alimiliki pango lile.

ambalo liko mwishoni mwa shamba lake

Hii pia inatumabia jambo kuhusu pango lile. Pango lilikuwa mwishoni mwa shamba la Efroni.

aniuzie waziwazi

"niuzie mbele yenu wote" au "niuzie mbele ya uwepo wenu"

kama miliki

"kama kipande cha nchi ambacho nitamiliki na kutumia"

Genesis 23:10

Sasa Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi

Hapa "Sasa" inatumika kuweka alama ya badiliko ya habari kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Efroni.

Efroni

Hili ni jina la mwanamume.

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale ambao wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

alipowasikia wana wa Hethi

Nomino inayojitegemea "alipowasikia" inaweza kuwekwa kama "kusikia" au "kusikiliza". "ili kwamba wana wote wa Hethi waweze kumsikia" au "wakati wana wote wa Hethi walipokuwa wakimsikiliza"

wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake

Hii inaelezea ni wana wapi wa Hethi walikuwa wakisikiliza. "wale wote waliokusanyika langoni mwa mji"

langoni mwa mji wake

Lango la mji ilikuwa mahali ambapo viongozi wa mji walikutana kufanya maamuzi muhimu.

mji wake

"mji ambao aliishi". Msemo huu unaonyesha ya kwamba Efroni alikuwa wa mji ule. Haimaanishi ya kwamba aliumiliki.

bwana wangu

Huu msemo umetumika kuonyesha heshima kwa Abrahamu.

mbele ya wana wa watu wangu

Hapa "mbele ya" ina maana ya watu waliokuwa kama mashahidi. "pamoja na wananchi kama mashahidi"

wana wa watu wangu

Hii ina maana ya "wananchi wenzangu" au "Wahiti wenzangu"

watu wangu

"watu wangu". Msemo huu unaonyesha ya kwamba efroni alikuwa sehemu ya kundi la watu. Haimaanishi ya kwamba alikuwa kiongozi wao.

Ninakupatia uzike wafu wako

"Ninakupatia. Zika wafu wako"

wafu wako

Kivumishi kidogo "wafu" kinaweza kuelezwa kama kitenzi. "mke wangu aliyekufa" au "mke wangu ambaye amekufa"

Genesis 23:12

akasujudu chini

Hii ina maana ya kuinama au kupiga goti chini kabisa kwa kuonyesha unyenyekevu wa heshima na taadhima kwa mtu.

watu wa nchi

"watu wanaoishi katika eneo lile"

watu wa nchi ile wakisikiliza

Nomino inayojitegemea "wakisikiliza" inaweza kusemwa kama "sikia" au "sikiliza". "ili kwamba watu wanaoishi katika eneo lile waweze kusikia" au "wakati watu waliokuwa wakiishi katika eneo lile wakisikiliza"

ikiwa uko radhi

Neno "lakini" linaonyesha tofauti. Efroni alitaka kutoa shamba kwa Abrahamu; Abrahamu alitaka kulipia. "hapana, lakini kama upo tayari" au "Hapana, lakini kama unakubaliana na hili"

Nitalipia shamba

"Nitakupa fedha kwa ajili ya shamba"

wafu wangu

Kivumishi cha "wafu" kinaweza kuelezwa kama kitenzi au "mke". "Mke wangu aliyekufa" au "mke wangu"

Genesis 23:14

Efroni

Hili ni jina la mwanamume.

Tafadhali bwana wangu, nisikilize

"Nisikie, bwana wangu" au "Nisikilize, bwana mwema"

bwana wangu

Msemo huu unatumika kuonyesha heshima kwa Abrahamu.

Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe?

Efroni alimaanisha ya kwamba kwa kuwa yeye na Abrahamu walikuwa matajiri wote, shekeli 400 za dhahabu zilikuwa kiwango kidogo. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Kipande cha shamba kina thamani cha shekeli mia nne za fedha tu. Kwako na mimi, hii si kitu"

shekeli mia nne za fedha

Hii ni kama kilogramu 4.5 za fedha

mia nne

"400"

wazike wafu wako

Kivumishi cha "wafu" kinaweza kuelezwa kama kitenzi au "mke". "Nenda kamzike mke wako ambaye amekufa"

Abrahamu akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema

"Abrahamu alipima fedha na kumpatia Efroni kiwango" au "Abrahamu alimhesabia Efroni kiwango cha fedha"

kiwango cha fedha alizosema

"kiwango cha fedha ambacho Efroni alikitaja"

wana wa Helthi wakisikiliza

Nomino inayojitegemea "wakisikiliza" inaweza kusemwa kama "sikia" au "sikiliza". "ili kwamba wana wa Hethi walimsikia" au "wakati wana wa Hethi walikuwa wakisikiliza"

wana wa Helthi

Hapa "watoto" ina maana ya wale waliotokana na Hethi. "uzao wa Hethi"

kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara

"kwa kutumia viwango vya vipimo vya uzito ambao wafanyabiashara walitumia." Hii inaweza kuelezwa kama sentensi mpya. "Alipima fedha kwa njia ile ile ambayo wafanyabiashara walikuwa wakitumia kupima"

Genesis 23:17

Makpela

Makpela lilikuwa jina la eneo au mahali.

Mamre

Hii ilikuwa jina jingine kwa mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale"

shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote

Msemo huu unafafanua kile ambacho mwandishi alimaanisha alipoandika "shamba la Efroni". Halikuwa shamba tu, lakini pia pango na miti katika shamba.

kwa Abraham kwa njia ya manunuzi

"ikawa mali ya Abrahamu alipoinunua" au "ikawa ya Abrahamu baada ya kuinunua"

mbele ya wana wa Hethi

Hapa "mbele ya" ina maana ya watu kutumika kama mashahidi. "pamoja na watu wa Hethi wakitazama kama mashahidi"

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

wote waliokuja malangoni pa mji wake

Hii inaeleza ni wana wapi wa Hethi waliomwona Abrahamu akinunua mali ile. "wale wote waliokusanyika langoni mwa mji"

malangoni pa mji wake

Malango ya mji palikuwa pale ambapo viongozi wa mji walikutana kufanya maamuzi muhimu.

mji wake

"mji aliokuwa akiishi". Msemo huu unaonyesha Efroni alikuwa wa mji ule. Haimaanishi ya kwamba aliumiliki.

Genesis 23:19

Baada ya haya

"Alipomaliza kununua shamba lile"

pango la shamba

"pango katika shamba lile"

shamba la Makpela

"shamba katika Makpela"

ambayo ni Hebroni

Maana zaweza kuwa 1) Mamre lilikuwa jina lingine la Hebroni au 2) Hebroni alikuwa akijulikana kama Mamre au 3) Mamre alikuwa karibu sana na mji mkubwa wa Hebroni, kwa hiyo watu waliuita Hebroni mara kwa mara.

kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia

"ikawa mali ya Abrahamu ya makaburi aliponunua kutoka kwa wana wa Hethi"

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"