Genesis 30

Genesis 30:1

Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto

"Wakati Raheli alipogundua ya kwamba hawezi kupata mimba"

nitakufa

Raheli anatumia ukuzaji kuonyesha jinsi alivyohuzunika ya kuhusu kutopata watoto. "Nitajisikia sina maana yoyote kabisa"

Nipe watoto

"Nisababishie kupata mimba"

Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli

Hasira ya Yakobo inazungumziwa kana kwamba ilikuwa moto. "Yakobo alimkasirikia sana Raheli"

Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?

Hili ni swali la balagha ambalo Yakobo anatumia kumkaripia Raheli. Inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mimi si Mungu! Mimi siye ninayekuzuia kupata watoto"

Genesis 30:3

Akasema

"Raheli akasema"

Tazama

"Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachotaka kukuambia". Hii inaongeza msisitizo kwa kile Raheli anachosema baadae"

kuna mjakazi wangu Bilha ... nami nitapata watoto kwake

Katika kipindi hicho, njia hii ilikuwa inakubalika kwa mwanamke tasa kupata watoto ambao kisheria wangekuwa wa kwake. Maana kamili inaweza kuwekwa wazi.

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

magotini pangu

Hii ni namna ya kusema ya kwamba mtoto ambaye Bilha anamzaa atakuwa wa Raheli. "wa kwangu"

nami nitapata watoto kwake

"na kwa njia hii atanifanya niwe na watoto"

Genesis 30:5

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

kumzalia Yakobo mwana

"akazaa mtoto wa kiume kwa Yakobo"

akamwita jina lake

"Raheli akmpatia jina"

akamwita jina lake Dani

"Jina la Dani lina maana ya "alihukumu".

Genesis 30:7

Bilha ... akashika mimba tena

"Bilha ... akawa mimba tena"

na kumzalia Yakobo mwana wa pili

"na akazaa mtoto wa kiume wa pili kwa Yakobo"

Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu

Msemo huu "mashindano nimeshindana" ni msemo unaotumiwa kwa msisitizo. Pia ni sitiari inayozungumzia jaribio la Raheli kupata mtoto kama dada yake kana kwamba alikuwa akigombana kimwili na Lea. "nimepambana sana kupata watoto kama dada yangu, Lea"

na kushinda

"na nimeshinda" au "nimefaulu"

Akamwita jina lake Naftali

"Jina la Naftali lina maana ya 'mapambano yangu'"

Genesis 30:9

Lea alipoona kwamba

"Lea alipopata ufahamu wa jambo hilo"

akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake

"alimpatia Zilpa, mtumishi wake, kwa Yakobo kama mke"

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

akamzalia Yakobo mwana

"akazaa mtoto wa kiume kwa Yakobo"

Hii ni bahati njema!

"Bahati gani!" au "Bahati gani hii!"

akamwita jina lake Gadi

"Jina la Gadi lina maana ya "mwenye bahati"

Genesis 30:12

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

akamzalia Yakobo mwana wa pili

"akazaa mtoto wa pili wakiume kwa Yakobo"

Nina furaha!

"Jinsi nilivyobarikiwa!" au "Jinsi nilivyo na furaha!"

mabinti

"wanawake" au "wanawake wadogo"

akamwita jina lake Asheri

"Jina la Asheri lina maana ya "furaha"

Genesis 30:14

Rubeni akaenda

"Rubeni alitoka nje"

Siku za mavuno ya ngano

Hapa msemo "siku za" ni sitiari yenye maana ya majira au kipindi cha mwaka. "katika kipindi cha mwaka cha mavuno ya ngano" au "wakati wa mavuno ya ngano"

tunguja

Hili ni tunda ambalo linasemekana kuongeza uwezo wa kuzaa na kuongeza hamu ya mtu kulala na mpenzi wake. "tunda la upendo"

Je ni jambo dogo kwako ... mme wangu?

"Je haujali ... mume wangu?" Hili ni swali la balagha limetumika kumkaripia Raheli. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli, "ni mbaya sana .. mume wangu"

Je na sasa unataka ... pia?

Hili ni swali la balagha limetumika kumkaripia Raheli. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli, "Na sasa unataka ... pia?"

Basi atalala nawe

"Basi Yakobo atalala" au "Basi nitamruhusu Yakobo alale"

Genesis 30:16

kwa tunguja za mwanangu

"kwa bei ya tunguja za mwanangu"

akashika mimba

"akawa mimba"

na kumzalia Yakobo mwana wa tano

"na akazaa mtoto wa kiume wa tano kwa Yakobo"

Mungu amenipa ujira wangu

Mungu kumzawadia Lea inazungumzwa kana kwamba alikuwa bosi anayelipa mshahara kwa mtu anayefanya kazi kwake. "Mungu amenipa stahiki yangu" au "Mungu amenizawadia"

Akamwita jina lake Isakari

"Jina la Isakari lina maana ya "kuna dhawabu"

Genesis 30:19

Lea akashika mimba tena

"Lea akawa mimba tena"

na kuzaa mwana wa sita kwa Yakobo

"na kuzaa mtoto wa kiume wa sita kwa Yakobo"

Akamwita jina lake Zabuloni

"Jina la Zabuloni lina maana ya "heshima"

na kumwita jina lake Dina

Hili ni jina la binti wa Lea.

Genesis 30:22

Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza

Msemo huu "akamkumbuka" una maana kukumbuka. Hii haimaanishi Mungu alimsahau Raheli. Ina maana alimfikiria juu ya ombi lake. "Mungu alimfikiria Raheli na kumpatia kile alichokitaka"

Mungu ameiondoa aibu yangu

Mungu kusababisha Raheli kutosikia aibu tena inazungumziwa kana kwamba "aibu" ni kitu ambacho mtu anaweza kukichukua kutoka kwa mtu mwingine. Nomino inayojitegemea "aibu" inaweza kuwekwa kama "kuona aibu". "Mungu amenisababishia nisione aibu tena"

Akamwita jina lake Yusufu

"Jina la Yusufu maana yake ni "na aongeze"

Yahwe ameniongeza mwana mwingine

watoto wa kwanza wa Raheli walitokana na mtumishi wa kike wa Bilha.

Genesis 30:25

Baada ya Raheli kumzaa Yusufu

"Baada ya Raheli kumzaa Yusufu"

na uniache niondoke

"ili niondoke"

unafahamu nilivyokutumikia

Yakobo anamkumbusha Labani kuhusu mkataba wake (29:26) Nomino inayojitegemea "huduma" inaweza kusemwa kama "kutumika". "unafahamu ya kwamba nimekutumikia muda wa kutosha"

Genesis 30:27

Labani akamwambia

"Labani akamwambia Yakobo"

Ikiwa nimepata kibali machoni pako

Msemo wa "machoni pako" ni lugha inayomaanisha mawazo na maoni ya Yakobo. Iwapo nimepata kibali na wewe" au "Iwapo unapendezwa na mimi"

nimepata kibali

Hii ni lahaja yenye maana ya mtu amekubalika na mtu mwingine.

subiri, kwa sababu

"tafadhali kaa, kwa sababu"

nimejifunza kwa kutumia uaguzi

"Nimegundua kwa desturi yangu ya kiroho na uchawi"

kwa ajili yako

"kwa sababu yako"

Taja ujira wako

Hii inaweza kuwekwa wazi. "Niambie nahitaji kukulipa kiasi gani kukuweka hapa"

Genesis 30:29

Yakobo akamwambia

"Yakobo alimwambia Labani"

jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami

"jinsi mifugo wako walivyokuwa vizuri tangu nimeanza kuwatunza"

Kwani walikuwa wachache kabla sijaja

"mifugo wako walikuwa wadogo kabla sijakutumikia"

na wameongezeka kwa wingi

"lakini sasa utajiri wako umeongezeka sana"

Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?

"Basi ni lini nitatunza familia yangu?" Yakobo anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba anataka kujitoa kwa familia yake. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "basi ninataka kutunza familia yangu!"

Genesis 30:31

Je nikulipe nini

"Nitakulipa nini" au "Nikupatie nini". Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "Nitakulipa nini ili kwamba ubaki na kunitumikia"

Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu

Neno la kiunganishi "ikiwa" inaweza kuongezwa kuonyesha ya kwamba hili ni jambo moja ambalo Yakobo anataka. "Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu"

nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza

"nitalisha na kuwatunza mifugo wako"

kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi

"na kutoa kila kondoo wa madoia, kila kondoo mweusi, na kila mbuzi mwenye madoa"

Hawa watakuwa ujira wangu.

"Hii itakuwa gharama ya kuniweka hapa"

Genesis 30:33

Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye

Neno "uadilifu" lina maana ya "uaminifu". Hii inazungumzia kuhusu uadilifu kana kwamba ni mtu ambaye anaweza kushuhudia kwa ajili au dhidi ya mtu mwingine. "Na baadae utajua kama nimekuwa mwaminifu na wewe au la"

Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Iwapo utakuta mbuzi yeyote asiyena madoa au kondoo yeyote ambaye sio mweusi, utawahesabu kuwa wameibiwa"

Na iwe kama yalivyo maneno yako

Hapa "neno" ina maana ya kitu kilichosemwa. "Itakuwa kana kwamba unasema" au "Tutafanya kile ulichosema"

Genesis 30:35

yaliyokuwa na milia na madoa

"ambazo zilikuwa na milia na madoa"

yaliyokuwa na milia na madoa

"yaliyokuwa na madoa"

kila aliyekuwa mweupe

"kila mbuzi ambaye alikuwa na weupe ndani yake"

na weusi wote katika kondoo,

"na kondoo wote weusi"

akawakabidhi katika mikono

Hapa "mikono" ina maana ya kutawala au kutunza. "akawafanya wanawe kuwatunza"

Genesis 30:37

mipopla .... mlozi ... mwaramoni

Hii yote ni miti ya mbao nyeupe

akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane

"na kutoa maganda ya mti ili kwamba mbao nyeupe ya chini ionekane"

mabirika yakunyweshe

vyombo virefu vya wazi vinavyoshikilia maji kwa ajili ya wanyama kunywa

Genesis 30:39

Wanyama wakapandana

"Wanyama wa mifugo walizalishana" au "Wanyama walipandana"

wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa

"wakazaa watoto weney milia na madoa"

Yakobo akawatenga

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba hii ilitokea katika kipindi cha miaka kadhaa. "Katika kipindi cha miaka kadhaa iliyofuata, Yakobo akawagawanya"

kuelekea

"kutazama kuelekea"

kayatenga makundi yake mwenyewe pekee

"aliwatenganisha mifugo wake"

Genesis 30:41

mbele ya macho ya kundi

Hapa "macho" ina maana ya "kuona". "ili kwamba mifugo waweze kuona"

kati ya fito

"mbele ya fito"

wanyama waliodhaifu

"wanyama wenye nguvu chache"

Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo

"Kwa hiyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wale wenye nguvu wakawa wa Yakobo". Unaweza kuiweka wazi zaidi. "Kwa hiyo wanyama dhaifu hawakuwa na milia au madoa na wakawa wa Labani, na wale wenye nguvu hawakuwa na milia au madoa na wakawa wa Yakobo"

Genesis 30:43

Mtu huyo

"Yakobo"

akastawi sana

"akafanikiwa sana" au "akawa tajiri sana"