Genesis 29

Genesis 29:1

watu wa mashariki

Hii ina maana ya watu wa Paddani Aramu, ambayo ni nchi mashariki mwa nchi ya Kaanani.

na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake

Neno "tazama" linaweka alama ya mwanzo wa tukio lingine katika simulizi kubwa.

Kwani kutoka katika hicho kisima

"Kwani kutoka katika kisima hicho". Msemo huu unaweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu jinsi wafugaji waliwanywesha mifugo"

wangeyanywesha

"wafugaji wangewanywesha" au "wale waliokuwa wakitunza kondoo wangewanywesha"

mdomo wa kisima

Hapa "mdomo" ni njia ya kuelezea uwazi. "uwazi wa kisima"

Genesis 29:4

Yakobo akawambia

"Yakobo aliwaambia wafugaji"

Ndugu zangu

Hii ni njia ya upole ya kumsalimia mgeni.

Labani mwana wa Nahori

Hapa "mwana" ina maana ya uzao wa kiume. Maana nyingine yaweza kuwa "Labani mjukuu wa Nahori".

na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo

"Tazama sasa! Raheli binti yake anakuja na kondoo"

Genesis 29:7

ni mchana

"jua bado lipo juu angani" au "jua bado linawaka kwa mwanga"

wakati wa kukusanya kondoo pamoja

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwako kukusanya mifugo"

kukusanya pamoja

Hii ina maana ya kuwakusanya pamoja ndani ya uzio ili wakae kwa usiku. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi.

kuwaacha wachunge

"waache wale nyasi shambani"

Hatuwezi kuwanywesha

"Inatubidi kusubiri ili kuwanywesha". Hii inahusu suala la muda, na sio ruhusa.

Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hadi pale wafugaji wengine watakapokusanya mifugo yao"

kutoka mlangoni mwa kisima

Hapa "mlangoni" ni njia ya kuelezea uwazi. "kutoka kwa kisima" au "kutoka kwa uwazi wa kisima"

na ndipo tutakapowanywesha kondoo

"kisha tutawanywesha kondoo"

Genesis 29:9

kaka wa mama yake

"mjomba wake"

mlangoni mwa kisima

Hapa "mdomo" ni njia ya kuelezea uwazi. "kisima" au "uwazi wa kisima"

Genesis 29:11

Yakobo akambusu Raheli

Nyakati za kale Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimu ndugu na busu. Ingawa, inafanywa baina ya wanamume.

akalia kwa sauti

Yakobo analia kwa sababu amefurahi sana. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

ndugu wa baba yake

"ana undugu na baba yake"

Genesis 29:13

mwana wa dada yake

"mpwa wake"

akamkumbatia

"alimkumbatia"

akambusu

Nyakati za kale Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimu ndugu na busu. Ingawa, inafanywa baina ya wanamume.

Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote

"kisha Yakobo alimwambia Labani kila kitu alichomuambia Raheli"

mfupa wangu na nyama yangu

msemo huu una maana zinaoana moja kwa moja. "ndugu yangu" au "mmoja wa familia yangu"

Genesis 29:15

Je unitumikie bure ... ndugu yangu?

Labani anatumia swali kusisitiza ya kwamba anatakiwa kumlipa Yakobo kwa kumtumika. Swali linawezakutafsiriwa kama kauli. Pia linaweza kuwekwa katika njia ya chanya. "Hakika ni sahihi ya kwamba nikulipe kwa kunitumikia ingawa wewe ni ndugu yangu."

Basi Labani alikuwa

Neno "basi" linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Labani na binti zake"

Macho ya Lea yalikuwa dhaifu

Maana zaweza kuwa 1) "Macho ya Lea yalikuwa mazuri" au 2) "Macho ya Lea yalikuwa ya kawaida"

Yakobo alimpenda Raheli

Hapa neno "alimpenda" lina maana ya mvuto wa kimahaba kati ya mwanamume na mwanamke.

Genesis 29:19

kuliko kumpa mwanamume mwingine

"kuliko kumpa kwa mwanamume mwingine"

nayo ilionekana kwake kama siku chache tu

"lakini muda ulionekana kwake kama siku chache tu"

kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake

"kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake" au "kwa sababu ya upendo wake kwake"

Genesis 29:21

Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia

Hapa "siku" ina maana ya muda mrefu zaidi. Msemo "zimetimia" unaweza kuwekwa katika hali ya chanya. Kauli hii ina mkazo. Nipatie Raheli ili kwamba niweze kumuoa, kwa maana nimekufanyia kazi miaka saba!"

kuandaa sherehe

"kuandaa sherehe ya harusi". Yawezekana Labani alikuwa na watu walioandaa sherehe hii. "alikuwa na watu waliondaa sherehe ya harusi"

Genesis 29:23

aliyelala naye

Inadokezwa ya kwamba Yakobo hakujua alikuwa na Lea kwa sababu ilikuwa giza na hakuweza kuona. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa ... mtumishi wake

Hapa mwandishi anatoa taarifa ya nyuma kuhusu Labani kumpa Zilfa kwa Lea. Inawezekana alimpa Zilfa kwa Lea kabla ya harusi.

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa Lea.

tazama, kumbe ni Lea

"Yakobo alishangazwa kuona ilikuwa ni Lea kitandani pamoja naye". Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yakobo alishtushwa na kile alichokiona"

Ni nini hiki ulichonifanyia?

"Yakobo alishangazwa kuona alikuwa Lea kitandani pamoja naye." Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yakobo alishtushwa na kile alichoona.

Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli?

Yakobo anatumia maswali haya kuonyesha maumivu yake ya kwamba Labani alimdanganya. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Nimekutumikia kwa miaka saba kumuoa Raheli"

Genesis 29:26

Siyo utamaduni wetu kumtoa

"Huwa hatutoi kwenye familia yetu"

Timiza juma la bibi arusi

"Kumaliza kusherehekea harusi ya Raheli"

na tutakupa yule mwingine pia

Maana kamila inaweza kuwekwa wazi. "na wiki ijayo tutakupatia Raheli pia"

Genesis 29:28

Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea

"Na Yakobo akafanya alichosema Labani, na akamaliza kusherehekea wiki ya harusi ya Lea"

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

Yakobo akalala na Raheli

Hii ni njia ya ustarabu ya kusema kuwa walikutana kimwili. "Yakobo akamuoa Raheli"

akampenda Raheli

Hii inamaanisha upendo wa kimahaba kati ya mwanamme na mwanamke.

Genesis 29:31

Lea hakupendwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yakobo hakumpenda Lea"

hakupendwa

Hii ni kuza jambo kusisitiza kuwa Yakobo alimpenda Raheli zaidi ya Lea. "alimpenda kwa uhafifu kuliko Raheli"

hivyo akalifungua tumbo lake

Mungu kumsababisha Lea kuwa na uwezo wa kuwa na mimba inazungumziwa kama kwamba Mungu alifungua tumbo lake.

hakuwa na mtoto

"hakuweza kuwa mjamzito"

Lea akashika mimba na kuzaa mwana

"Lea alipata mimba na kumzaa mwana wa kiume"

naye akamwita Rubeni

Jina Rubeni linamaanisha "Tazama, mwana wa kiume."

Yahwe ameliangalia teso langu

Lea alipitia uchungu wa hisia kwa sababu Yakobo alimkataa.. Nomino "teso" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "Yahwe aliona kuwa nateseka"

Genesis 29:33

Kisha akashika mimba

"Lea akawa mjamzito"

kuzaa mwana

"akazaa mwana wa kiume"

Yahwe amesikia kwamba sipendwi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe amesikia kuwa mme wangu hanipendi"

akamwita Simoni

Jina Simoni linamaanisha "kusikiwa."

mume wangu ataungana nami

"mume wangu atanikumbatia"

nimemzalia wana watatu

"nimezaa wana watatu wa kiume kwa ajili yake"

akaitwa Lawi

Jina Lawi linamaanisha "ambatishwa."

Genesis 29:35

Akashika mimba tena

"Lea akawa na mimba tena"

kuzaa mwana

"Akazaa mwana wa kiume"

akamwita jina lake Yuda

Jina Yuda linamaanisha "sifa."