Sura 2

1 Napenda mutambuwe yakama vita ninayo pigana juu yenu ni kubwa sana,kwa walaodisia na kwa wengine wenye hawajaniona. 2 Natumika kusudi Roho yao ijazwe na nguvu sababu wanakutana katika ukweli wa siri iliyo dani ya upendo wa Mungu. 3 Katika Kristo, utajiri, hekima na akili vimejificha. 4 Namwambia hivi kusudi mutu asiwadanganye na maneno ya uwongo. 5 Hata kama kimwili hatuko pamoja lakini kiroho tuko pamoja. Ninafurahi kuona utaratibu wenu na imani yenu katika Kristo 6 Kama vile mulimuamini Kristo Bwana wetu, mutembee naye pamoja. 7 Muwe na misingi ndani yake, mujengwe juu yake na mubaki katika imani kupitiya maneno muliyofundishwa , na mumushukuru Mungu sana. 8 Angalieni, mutu asiwadanganye kwa elimu yake ya uwongo na ya udanganyifu kutoka kuasili ya watu, yenye haifanane na amri ya Kristo. 9 Kwa sababu ndani yake ukumilifu wa Mungu unaishi . 10 Munajazwa na utukufu kwake, ni yeye aliye mkuu mwenye nguvu na mamlaka yote. 11 Kwake mulitahiriwa, siyo na watu katika mwili, lakini kutahiriwa na Kristo. 12 Mulizikwa pamoja naye kupitia ubatizo, na mulifufuka naye kwa imani, katika nguvu ambayo Mungu alimufufua nayo Kristo toka wafu. 13 Wakati muli kuwa mumekufa kwa ajili ya zambi zenu na kwa sababu ya kutokutahiriwa, aliwaongoza ku njia ya uzima na kusamehe zambi zenu zote ku njia ya musalaba. 14 Alizimisha maamuzi ya madeni yetu yote yenye iliandikiwa kwa kutuhukumu. Aliiondowa na kuileteya haya kwa kuitpigiliya musalabani. 15 Aliondowa uwezo na nguvu, na kuifezelesha kupitiya musalaba mbele ya watu. 16 Kwa sababu, hii mutu asiwahukumu juu ya chakula, aojuu ya kinywaji wala kwa ajili ya siku kuu Fulani, kuandama kwa mwezi, wala juu ya sabato. 17 Vyote vilikuwa kinvuli cha maneno yatakayokuja, lakini uhakika wa yote ni katika Kristo. 18 Mutu asiwadanganye, kwa ku nyenyekvu wa wanafiki wala kwa ibada ya wamalaika, juu wanyanganye ushindi wenu. Kwa maana mutu wanamuna ile ni mwenye maonyo mbaya na mwenye kiburi cha mwili. 19 Watu wa namuna hii hawana mapatano na Yesu, kwa maana mwili muzima unajengwa na vyungo vyote vinaunga nishwa na kukomazwa na Mungu. 20 Kama mulikufa na Kristo, kwa sababu ya zambi, sababu gani kuendeleya kuishi tena katika sheriya ya dunia ya zambi ? 21 «Musikamate, musionje, musiguse!» 22 Vyote ni vtu vinavyo haribika wakati vinatumiwa, kufatana na mafundisho ya watu wa dunia. 23 Hii mafundisho inakuwa na hali ya hekima ya kidini, inatuma tutumikishe mwili wetu nguvu sana. Lakini haina hata heshima moja kuhusu mapenzi ya mwili.