Sura 2

1 Basi wewe mwana wangu, ukuwe hodari kwa njia ya neema uliyopata katika kuungana kwako na Kristo Yesu. 2 Wewe umesikia mafundisho niliyotoa mbele ya washuhuda wengi. Nawe sasa uyafundishe kwa watu waaminifu watakaoweza vilevile kuyatoa kwa watu wengine. 3 Ushiriki katika mateso kama vile askari mwema wa Kristo Yesu. 4 Askari anapokuwa katika vita, hapaswi kushugulika na mambo ya kawaida ya maisha ya wakaaji kama anataka kumupendeza mkubwa wa kundi lake. 5 Vilevile mtu yeyote anayeshindana katika michezo hawezi kupata zawadi ya ushindi kama asipotii kanuni za michezo. 6 Tena mulimaji anayetumika kazi ngumu ndiye anayepaswa kupata sehemu ya kwanza ya mavuno. 7 Ufikiri juu ya maneno hayo ninayosema, kwa maana Bwana atakupa uwezo kwa kuyaelewa yote. 8 Umukumbuke Yesu Kristo aliyekuwa wa ukoo wa mfalme Daudi, na aliyefufuka sawa vile inavyotangazwa na Habari Njema hii ninayohubiri. 9 Mimi ninateswa na kufungwa sawa mutenda maovu kwa sababu ninahubiri Habari Njema hii. Lakini Neno la Mungu halifungwi. 10 Ni kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya watu ambao Mungu alijichagulia kuwa wake, kusudi wao vilevile wapate kuokoka na kupata utukufu wa milele unaopatikana kwa njia ya Kristo Yesu. 11 Maneno haya ni ya kuaminiwa: Kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye vilevile. 12 Kama tunaendelea kuvumilia, tutatawala pamoja naye vilevile. Kama tunamukana, naye atatukana vilevile. 13 Kama tunakosa kuwa waaminifu, yeye anabaki mwaminifu. Kwa maana hawezi kujikana yeye mwenyewe. 14 Uwakumbushe watu maneno hayo yote na kuwaonya wazi mbele ya Mungu waache kubishana juu ya maneno. Mabishano hayana faida kwa maana yanawapoteza wale wanaoyasikia. 15 Ufanye juhudi kusudi upate kuhesabiwa mbele ya Mungu kama mtu anayemupendeza, ukiwa kama mtumishi asiyesikia haya juu ya kazi yake, lakini anayetangaza kwa haki ujumbe wa kweli wa Mungu. 16 Uepuke masemi yasiyokuwa na maana na ya kidunia, kwa maana wale wanaoyafuata wanazidi kupotoka katika ibada ya uongo. 17 Maneno yao yanaambukiza kama vile kidonda chenye kuoza kinavyoharibu mwili wote. Kati yao kuna Himeneo na Fileto. 18 Hao wamepotoka mbali na ukweli, wamepotosha imani ya watu wengi wakisema kwamba ufufuko tunaongojea umekwisha kufanyika. 19 19 Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule Bwana anajua wale wanaokuwa wake, na haya mengine: «Kila mtu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.» 20 Ndani ya nyumba kubwa, hamuna vyombo vya zahabu na feza tu, lakini muko vilevile vyombo vya miti na vya udongo. Vimoja ni vya matumizi ya kipekee na vingine ni vya matumizi ya kawaida. 21 Basi kama mtu atajitakasa kwa kujitenga na maovu hayo yote atakuwa chombo cha matumizi ya kipekee, kitakatifu cha mwenye nyumba na chenye mafaa kwake na kuwa tayari kwa kila kazi njema. 22 Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi. 23 Ukatae mabishano ya kipumbafu na yasiyokuwa na maana; unajua wewe mwenyewe kwamba yanaleta magomvi. 24 Basi, mtumishi wa Bwana hapaswi kugombana. Anapaswa kuwa mupole kwa watu wote, anayejua kufundisha na muvumilivu. 25 Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli. 26 Kwa njia hiyo wanaweza tena kupata ufahamu na kuponyoka katika mitego ya Shetani, aliyewanasa na kuwafanya watimize mapenzi yake.